Roho ya Leweyathani/mamba(leviathan spirit)

Roho ya Leweyathani/mamba(leviathan spirit)

a sinner saved by Christ

JF-Expert Member
Joined
Feb 19, 2017
Posts
3,322
Reaction score
3,792
*Roho chafu ya LEWIYATHANI(LEVIATHAN Spirit, *MAMBA wa kwenye maji

Isaya 27:1 Mwenyezi-Mungu atautwaa upanga wake mkubwa, mkali na imara, na kuliadhibu dude Lewiyathani joka lirukalo na danganyifu; Mwenyezi-Mungu ataliua joka liishilo baharini

*AYUBU 45
Yeye hutazama kila kitu kilicho juu;Ni mfalme juu ya wote wenye kiburi

Hakuna mwanadamu wala malaika hata Mikaeli anayeweza kushindana naye isipokuwa Mungu mwenyewe peke yake

29 Marungu huhesabiwa kama mabua; Naye hucheka mshindo wa mkuki ukitupwa.

27 Yeye huona chuma kuwa kama nyasi, Na shaba kama mti uliooza

26 Mtu akimpiga kwa upanga, haumwingii; Wala fumo, wala mshale, wala mkuki wenye ncha.

21 Pumzi zake huwasha makaa, Na miali ya moto hutoka kinywani mwake.

19 Mienge iwakayo hutoka kinywani mwake, Na macheche ya moto huruka nje.
Je! Waweza wewe kumvua mamba kwa ndoana? Au, kuufunga ulimi wake kwa kamba?

2 Je! Waweza kutia kamba puani mwake? Au kutoboa taya yake kwa kulabu?

DALILI ZA MTU ALIYESHAMBULIWA NA ROHO hii chafu ya mamba LEWIYATHANI

1)KIBURI/KUJIKWEZA,KUJITUKUZA,KUJISIFU,KUJIGAMBA,KUJISHIBA KUJIKINAI MWENYEWE
Hasa elimu ya dini Kiburi cha kiroho dini,KUJIHESABIA HAKI mwenyewe MAFARISAYO--na kiburi cha aina yoyote--maana ya kiburi KUJIONA wewe ni bora kuliko mwingine katika jambo lolote.

Ayubu kuna wakati alijihesabia haki sana nafsini mwake, hali iliyomfanya aone kama mateso yake hayana sababu ya msingi au ni ya udhalimu.

angeweza kuwa mnyenyekevu hata katika mateso kama BWANA wetu Yesu,au Stefano..au hata nabii ELISHA..Nabii Elisha aliugua ugonjwa mbaya uliosababisha kifo chake,(2 Wafalme 13:14-21)
Hata baada ya kufa na kuzikwa, nguvu za Mungu zilionekana kupitia mifupa yake; mtu aliyetupwa kwenye kaburi lake alifufuka mara tu alipogusa mifupa ya Elisha.

*Ayubu alitubu mbele za Mungu baada ya Mungu kuzungumza naye kutoka katika upepo wa tufani na kumweleza ukuu Wake na udogo wa mwanadamu.

Ayubu 42:5-6, Ayubu alikiri kwamba alikuwa amemhukumu Mungu kwa sababu ya mateso na shaka zake. Alisema:
Nilikuwa nimesikia habari zako, kwa kusikia kwa masikio; Bali sasa jicho langu linakuona. Kwa sababu hiyo najichukia nafsi yangu, na kutubu Katika mavumbi na majivu.
Baada ya toba hii na unyenyekevu wake, Mungu alimbariki Ayubu mara mbili ya utajiri wake wa awali na kumrejeshea afya yake.

KIBURI/MAJIVUNO iwe moyoni,nafsini, na *kukosa unyenyekevu ndio dalili ya kwanza

2)KUBADILISHA KUPINDISHA na KUGEUZA MANENO,MATENDO udanganyifu

katika mtindo wa kupindisha tasfiri ya maneno yaliyotamkwa au kitendo kilichofanywa na kuzua TAHARUKI,kutokuelewana ,kuvunja mahusiano ya watu kuwaganya na kutengeneza migongano na malumbano na kuwatenganisha watu na ndoa na maelewano.

Mfano unatamka maneno mazuri halafu roho hii chafu inayageuza geuza kabla hayajafika masikioni pa msikilizaji wako,na pindi yakofika anaelewa tofauti na ulichokimaanisha,anakuelewa vibaya ,anakutafsiri vibaya tofauti na lengo lako na makusudi yako na nia yako.
LENGO ni KUWATENGANISHA watu ,kuwafarakanisha ,kuwagombanisha
Lakini pia inaweza kukuletea tasfiri potofu iliyogeuzwa juu ya unavyotafsiri mambo machoni,masikioni ,moyoni,nafsini..ukatafsiri ubaya kwenye wema..
Kukuchanganya akili CONFUSION.

3)Kukutia roho ya WOGA* hofu ,kukufanya ujione dhaifu,kwa kukutisha mana anautisho ,na hakuna wa kuweza kupambana naye isipokuwa Mungu pekee.
ndiyo mana inatupasa tujinyenyekeze chini ya mkono hodar wa Mungu wenye nguvu,peke yetu hatuwezi bila Mungu,...hii vita sio yetu bali ni ya Mungu mwenyewe.

hili joka mithili ya mamba linafanya kazi kwa SIRI kwa kuvizia na kwa akili ,hata linapokuvamia unaweza usijue kama umevamiwa na ROHO ya LEWIYATHAN mamba ila utasababisha madhara na kukusababishia madhara kama mamba anavyowinda baharini kwa kinyemelea kwa usiri.

4)UTAOTA NDOTO ZA MAMBA* ..ukiona mamba ndotoni...wanakushambulia.
ni roho chafu yenye nguvu sana inayofanya kazi kwa siri,ni roho hatari sana na mbaya sana .

SALA YA KUOMBA
Mungu BABA
NATUBU LEO kwa dhambi yangu ya KIBURI,majivuno,kujihesabia haki,na kujitukuza mwenyewe nilikokufanya katika mawazo yangu,nafsini mwangu,kwa maneno na matendo yangu.

NATUBU kwa kushambuliwa na maroho ya KIBURI

Naomba unisaidie nitoke nosinaswe kwenye mtego wa KIBURI,majivuno,kuhukumu wengine,kunung'unika(manung'uniko) pale ambapo nilipopatwa na magumu,majaribu ,matatizo( N:B KOSA alilolifanya Ayubu)

FUKUZA sauti za KIBURI na MAJIVUNO katika mawazo yangu,..naomba nipe neema ya kuwa MNYENYEKEVU
 
Zaburi 74:13
Ni wewe uliyeigawanya bahari kwa uweza wako; ulivunja vichwa vya mnyama mkubwa wa baharini

Hili joka mamba la baharini lewiyathani(leviathan spirit ,lina vichwa vingi .

vichwa vyake ndio hivi
Methali 6:16-19
Kuna vitu sita anavyochukia Mwenyezi-Mungu; naam, vitu saba ambavyo ni chukizo kwake:

1) Macho ya kiburi,
2)ulimi mdanganyifu,
3)mikono inayoua wasio na hatia, 4)moyo unaopanga mipango miovu, 5)miguu iliyo mbioni kutenda maovu,
6)shahidi wa uongo abubujikaye uongo, na
7) mtu achocheaye fitina kati ya ndugu.
 
1Petro 5: 5
“..ninyi nyote jifungeni unyenyekevu, mpate kuhudumiana; kwa SABABU MUNGU HUWAPINGA WENYE KIBURI, lakini huwapa wanyenyekevu neema”.

Mithali 29:23
“Kiburi cha mtu kitamshusha; Bali mwenye roho ya unyenyekevu ataheshimiwa”.

Yohana 2:16
“Maana kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na KIBURI CHA UZIMA, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia.”


Isaya 2:12 “Kwa maana kutakuwa siku ya Bwana wa majeshi juu ya watu wote WENYE KIBURI NA MAJIVUNO, na juu ya yote yaliyoinuka; nayo yatashushwa chini.”

maana kutakuwa siku ya Bwana wa majeshi juu ya watu wote WENYE KIBURI NA MAJIVUNO, na juu ya yote yaliyoinuka; nayo yatashushwa chini.”

Mithali 16:5 “Kila mwenye moyo wa kiburi ni chukizo kwa Bwana; Hakika, hatakosa adhabu”.

Mithali 8:13 “Kumcha Bwana ni kuchukia uovu; Kiburi na majivuno, na njia mbovu, Na kinywa cha ukaidi pia nakichukia.”’

Ayubu 40:12 “Mtazame kila mtu mwenye kiburi ukamshushe, Ukawakanyage waovu hapo wasimamapo”.

Zaburi 119:21 “Umewakemea wenye kiburi, Wamelaaniwa waendao mbali na maagizo yako”.
 
MOYO WA DAUDI
Zab 131:1 SUV
BWANA, moyo wangu hauna kiburi, Wala macho yangu hayainuki. Wala sijishughulishi na mambo makuu, Wala na mambo yashindayo nguvu zangu.

Mdo 13:22
Na alipokwisha kumwondoa huyo, akamwinua Daudi awe mfalme wao ambaye alimshuhudia, akisema, Nimemwona Daudi, mwana wa Yese, mtu anayeupendeza moyo wangu, atakayefanya mapenzi yangu yote.
 
Wafilipi 2:3
Msitende neno lolote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake.
 

Attachments

  • images - 2026-05-15T181805.395.jpeg
    images - 2026-05-15T181805.395.jpeg
    35.5 KB · Views: 9
  • ego-enemy-quote-self-improvement-600w-1937816428.jpg
    ego-enemy-quote-self-improvement-600w-1937816428.jpg
    103.3 KB · Views: 9
Jinsi ufalme wa Mungu unavyofanya kazi ni mfano wa ufalme au serikali inayofuata SHERIA zilizo katika katiba katika kutoa hukumu A HAKI kifupi ni kama mfumo wa MAHAKAMA ya haki.

Mungu akiwa kama HAKIMU
(2 Wathesalonike 1:5
kwamba hukumu ya Mungu ni ya haki



YESU malaika wa Mungu kama mtetezi wetu,wakili wetu(
Ayu 19:25
Lakini mimi najua ya kuwa Mteteaji wangu yu hai



SHETANI na mapepo wabaya ufalme wa giza pamoja na jeshi la wakuu wa anga giza wa,majini,wachawi hawa ni WASHITAKI wetu.
1 Pet 5:8-10
mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze.

SHEATANI ufalme wa giza mapepo wanaongea na Mungu pia katika kusikiliza hizi kesi juu ya wanadamu(USIFIKIRI shetani na Mungu hawaongei..Ayu 1:7
BWANA akamwuliza Shetani, Umetoka wapi wewe? Ndipo Shetani akamjibu BWANA, na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani, na katika kutembea huku na huku humo.

kila siku shetani anapeleka mashitaka kuwashitaki watakatifu wa Mungu kila wanapokosea.

SHERIA ama KATIBA ZINAZOTUMIKA INAYOTUMIKA ni sheria za Mungu NENO LA MUNGU ama kitabu cha biblia BIBLIA hii ndio kama katiba ya milele inayouhukumu ulimwengu wote sasa na hata siku ya hukumu ya mwisho mbeleni future.Dunia na ulimwengu utapita lakini neno la Mungu litasimama halitapita..hakuna katiba mpya wala sheria mpya ni neno lile lile la Mungu litasimama BIBLIA TAKATIFU milele.

kutokujua sheria haikuondelei kosa hivyo ni vizuri tukajua sana sheria ya Mungu neno la Mungu ili tusije tukaangukia katika dhambi(NENO la Mungu tuliweke moyoni mwetu kwa wingi ili tisitende dhambi,kuijua sheria ya na katiba ya kitabu cha hukumu.

upande wa MASHITAKA(ufalme wa giza ,shetani ,mapepo ,wachawi)

Unafungua kesi za mashitaka kila dakika dhidi yetu pale tunapovunja sheria ya Mungu (KIUKA NENO LA BIBLIA NENO LA MUNGU) kwa kutumia ishahidi wa kisheria wa kimaandiko..

kitu cha kujua..KILA DHAMBI unayoifanya hata kwa SIRI DHAMBI ZA SIRI (za moyoni mwako) ufalme wa giza unazijua ,kitu cha kufahamu ukitenda dhambi tu ile dhambi inapiga kengele inapiga kelele au inaonekana kwenye kioo au television (HAKUNA DHAMBI YA SIRI ) utakayoifanya Shetani na mapepo wachawi wasijue au wasio one yani wewe ni kama KIOO kinachoangaza kuonyesha maisha yako ya dhambi na utakatifu wako kwa shetani na mapepo na wachawi na hata mbele za Mungu kila kitu unachofanya na hali yako ya kiroho ,kama ukiwa mtakatifu otaonekana wazi na kama umefanya dhambi sekunde hiyo hiyo itaonekana(wewe ni kama BARUA inayosomeka katika ulimwengu wa roho hakuna kilichojificha huwezi kumdanganya Mungu wala huwezi kumficha shetani,hata dhambi za moyoni mwako zinaonekana ,asiloweza kulijua sheteni kuhusu wewe ni mawazo yako unawaza nini ila pindi ikitenda dhambi tu INAREKODIWA video inaonekana kwwnye screen haijifichi.
INAKUWA USHAHIDI hata kama ni dhambi ya SIRI ya ndani ya moyo.

MASHITAKA anayotushtaki nayo shetani ni DHAMBI zetu kwa kuwa anazijua dhambi zetu na yeye shetani ndiyo baba wa uovu ndio kiongozi wa uovu na dhambi toka mwazo ndiye anayepeleka mashitaka mashitaka YANAPELEKWA KILA DAKIKA (umetenda dhambi shetani anafungua kesi kupeleka kwa Mungu kukushitaki KUKATA rufaa kupinga KUZUIA MAPINGAMIZI mahakama ya Mungu ILI kuzuia maombi yako ,yani ili Mungu asikubariki,asijibunmaombi yako ,na UPATE HUKUMU ya kuadhibiwa au mapepo wachawi shetani apate uhalali wa kukushambulia.

MAMBO YA KUFANYA KWAKO
1) Maisha ya TOBA tubu mara kwa mara,omba ROho mtakatifu akuonyeshe dhambi zote ulizofanya ndani ya siku nzima tokanimeanza na tubu haraka mapema kabla ya siku kuisha kabla hujalala usilale ukiwa hujatubu dhambi zako ulizofanya ambazo zimemuhuzinisha roho mtakatifu hata kama ni zile unazo ona ni dhambi ndogo ndogo na hata ulizozisahau au ambazo hukujua .(TOBA na kuomba kutakaswa)

2.SAMEHE WATU usiweke kinyongo kubeba watu moyoni kitokusamehe vinyongo,chuki na hasira hata kama aliyekukosea hajakuomba msamaha ama unahisi hastahili kusamehemwa msamehe kwa ajili ya faida yako mwwnyewe.

mfano..MKE alimfumania MUMEWE sasa akaweka kinyongo na kuyokusamehe ..kupitia hiyo dhambi ya kutokumsamehe mume wake aliyefanya dhambi ya uzinzi/uasherati ..inapelekea shetani kupata uhalali wa kisheria kukushambulia kwa sababu
atendaye dhambi ni wa Ibilisi; kwa kuwa Ibilisi hutenda dhambi tangu mwanzo.na tena mshahara wa dhambi ni mauti na zaidi dhambi zetu zinatutenga na Mungu

KWA KIFUPI DHAMBI INAFUNGUA MLANGO wa kuruhusu shetani akushambulie zaidi.

tena atashambulia zaidi hiyo hiyo NDOA yako kwa kitendo cha wewe mwanamke kutokumsamehe tu mumeo kwa vile amefanya uzinifu/uasherati..Shetani atakusukumia maroho ya MAGOMVI,CHUKI HASIRA,na HATA KUVUNJA KUTENGANA kuvunja ndoa ,kabisa,na hata kudhuru familia na maisha ya kiroho na inada zako...

itambue mitego ya SHETAni ukitambua Silaha wanazotumia ulimwengu wa giza ukiwapeleleza siyo vibaya kujua ulimwengu wa giza unavyofanya kazi kuharibi kushambulia watu wa Mungu,hata JOSHUA alituma wapelelezi kuipeleleza maadui waliokuwa wanakalia nchi ya KAANANI..ukimjua adui yako utajua pia namna ya kupambana naye na silalaha anazotumia.

Mwanamke ukimsamehe mume wako ukaondoa kinyongo utaiponya ndoa yako na maisha yako ya kiroho wewe mwenyewe .

VINYONGO KUTOKUSAMEHE (unforgiveness,bitternes,na uzinzi/uasherati )ni moja ya mashitaka yanayopelekwa kutishitaki na kufungulia mlango wa kuingiza MAUTI katika maisha yetu...USIMPE SHETANI NAFASI ..usimruhusu usimfungulie mlango..huo ni mfano mmojawapo ipo mifano mingi ya vinyongo na kutokusamehe.

3)...TUMIA DAMU YA YESU katika hukumu DAMU ya YESU inatupa NEEMA yani kama ni kesi inalipa FAINI au DENI zetu au inafuta mashitaka kwa kulipa gharama ya tuliyostahili adhabu DAMU YA YESU inalipa in FULL..

sasa hata kama kesi ni kubwa kiasi gani,lakini hii neema ya damu ya Yesu siyo ya kuichezea yani kurudia rudia kufanya dhambi kwa makusudi kwa kuwakuwa kuna neema ya damu ya Yesu..BIG NO.!!!

Unapoanza siku funika siku yako kwa damu ya Yesu,akili zako nafsi yako,watito wako,nyumba yako ,jifunike kwa damu ya YESU na familia yako na kila jambo lako ,kazi yako,ndoa yako ,milango ,madirisha FUNIKA KWA DAMU YA YESU na usiku kabla ya kulala funika kwa damu ya Yesu.
Tunahesabiwa haki kwa kupitia Yesu mwenye haki,na kwa kupigwa kwake Yesu sisi tumepona,Yesu amechukua dhambi zetu na adhabu yetu.

Ufunuo 12:11
Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-kondoo,



4)KUMSIFU MUNGU katikati ya mateso katikati ya shida na dhiki.
Mungu wetu anakaa katika sifa ,yani ni sawa na kukata rufaa kwenda kumfukia Mungu kwa njia ya sifa,na ile kumsifu Mungu ukiwa katikati ya mateso magumu unayopitia ni lugha unayo ongea kumwambia Mungu pamoja na haya magumu yote adui amenitendea amenifanyia ila bado wewe kwangu ni BWANA hii hi kumfikia Mungu anayekaa katika sifa.

Zaburi 22:3
Hata hivyo, wewe ni mtakatifu; wewe watawala na kusifiwa

yani ni sawa na kumwambia Mungu hata yanipate mabaya kiasi gani hata adui anitende mabaya kiasi gani hata nichinjwe shingo katika hali yeyote ile wewe Mungu kwangu ni yote katika vyote hata nikose vyote wewe Mungu kwangu unatosha ,ni sawa na kusema ,Mungu kwangu wewe ndio kila kitu,hakuna cha kunitenga na upendo na wema wa Mungu.

mfano mzuri ,PAULO NA SILO walipofungwa gerezani wakiwa wamegungwa minyororo katikati ya gereza waliomba,milango ya gereza na minyororo iliyowafunga ikafunguka..



Kamwe usije ukamlalamikia Mungu usimnungunikie Mungu hata kama unapitia shida usilalamike hata kama unapitia mateso makubwa kiasi gani ,wewe msifu Mungu ,wengi wamepokea uponyaji na wameona wanapoea majibu kupitia kumsifu Mungu katikati ya MATESO na majaribu makubwa waliyokuwa wanapiatia.

Mdo 16:25
Lakini panapo usiku wa manane Paulo na Sila walikuwa wakimwomba Mungu na kumwimbia nyimbo za kumsifu, na wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza(Mara, milango yote ikafunguka na minyororo iliyowafunga hao wafungwa ikaachana.

minyororor maana yake ni vifungo vyote vya shetani vinavyokutesa na mashitaka yote ,usiangalie minyororo ya mwilini na milango ya jengo la gereza.

gereza ni mambo yako yaliyofungwa maeneo mbalimbali.


5)KUWAJALI WAHITAJI"

hii ni kusaidia wale wasiojiweza wanyonge ambao hutarajii wakulipe fadhila yoyote na wala sio kwa lengo la kupata sifa au kujioyesha,ni tofauti kusaidia watu waojiweza marafiki zako ukiwa na lengo kuna siku na wao watakulipa fadhila kama unawakopesha utakuja kulipwa.

Mit 19:17
Amhurumiaye maskini humkopesha BWANA; Naye atamlipa kwa tendo lake jema.

sasa hapa ukimsaidia masikini ni sawa na kumkopesha MUNGU mwenyewe na lazima atakulipa mema,hapa hata shetani aje na kesi yake kukushitaki unampiga knock out.

lakini mkono unaotoa ndio unaobariwa kuliko unaopokea,lakini ukiwapa watu vitu utapokea kwa kipimo cha Mungu kilichosukwa sukwa na kusindikiwa hata kumwagika.

lakini dini iliyo safi isiyo na taka ni kuwasaidia wahitaji,Yakobo 1:27
Dini iliyo safi na isiyo na hitilafu mbele ya Mungu Baba ni hii: Kuwasaidia yatima na wajane katika shida zao,

zaidi ya yote ni hii

ZABURI YA 41
Heri amkumbukaye mnyonge;
BWANA atamwokoa siku ya taabu
.
2BWANA atamlinda na kumhifadhi hai,

Naye atafanikiwa katika nchi;

Wala usimtie katika hali wamtakiayo adui zake
.
3BWANA atamtegemeza alipo mgonjwa kitandani.
Katika ugonjwa wake unamponya maradhi yake.

(wanaojua siri hii utawakuta wanatoa sana misaada kwa masikini na wahitaji,ni vizuri tuwe na maarifa mbona wana wa giza wana maarifa sana katika kututenda maovu,na sisi tuwe na maarifa ya KIROHO)

6)KUTII SHERIA/NENO YA MUNGU
Submissive kutii hata kile ambacho unaona kinakunyima starehe ama raha ya mwili au hata kama kinaonekana kinafurahisha mwili.

mfano..mfanyakazi mkoja wa taasisi moja alipata JARIBU mtihani ,boss wake alimlazimisha afanye kughushi udanganyifu ofisini kwake ili waweze kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu ..lakini yeye alisimama akisema hiki kiti ni siwezi kufanya kwa sababu ni dhambi kwa Mungu ni bora kama ni kazi nipoteza kazi lakini sipo tayari kufanya dhambi ya udanganyifu na wizi ,..mwisho wa siku yule bosi alietaka kumfukuza kazi kwa kukataa kutii agizo la kufanya udanganyifu wa wizi wa kalamu,kukipatia pesa alifukuzwa kazi yeye na yule aliyelinda uaminifu mbele za Mungu alipandishwa cheo.

Meshacj ,shedrak Abednego walikataa kuabudu sabamu ya nebukadreza wakatupwa kwenye tanuru la moto ila Mungu akawaoko kwa kuwatumia malaika hata kwwnye tundu la simba.

Zab 1:2-3
Bali sheria ya BWANA ndiyo impendezayo, Na sheria yake huitafakari mchana na usiku. Naye atakuwa kama mti uliopandwa Kandokando ya vijito vya maji, Uzaao matunda yake kwa majira yake, Wala jani lake halinyauki; Na kila alitendalo litafanikiwa.

Zab 119:
Moyoni mwangu nimeliweka neno lako, Nisije nikakutenda dhambi.

huyu DAUDI aliyeandika zaburi hata moyoni mwake anasema hana kiburi,na hata kutubu dhambi alikuwa mwepesi kutubu dhambi kwa haraka mara kwa mara.

ndiyo maana alimpendeza Mungu.

so utii ni bora kuliko dhabifu yani kumtii Mungu ni bora zaidi kuliko.

kwa maana ya kusikia na kuyafanya mapenzo ya Mungu.

YESU ANAKUPENDA Isa 53:5

Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake,

Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.
 
Jinsi ufalme wa Mungu unavyofanya kazi ni mfano wa ufalme au serikali inayofuata SHERIA zilizo katika katiba katika kutoa hukumu A HAKI kifupi ni kama mfumo wa MAHAKAMA ya haki.

Mungu akiwa kama HAKIMU
(2 Wathesalonike 1:5
kwamba hukumu ya Mungu ni ya haki



YESU malaika wa Mungu kama mtetezi wetu,wakili wetu(
Ayu 19:25
Lakini mimi najua ya kuwa Mteteaji wangu yu hai



SHETANI na mapepo wabaya ufalme wa giza pamoja na jeshi la wakuu wa anga giza wa,majini,wachawi hawa ni WASHITAKI wetu.
1 Pet 5:8-10
mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze.

SHEATANI ufalme wa giza mapepo wanaongea na Mungu pia katika kusikiliza hizi kesi juu ya wanadamu(USIFIKIRI shetani na Mungu hawaongei..Ayu 1:7
BWANA akamwuliza Shetani, Umetoka wapi wewe? Ndipo Shetani akamjibu BWANA, na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani, na katika kutembea huku na huku humo.

kila siku shetani anapeleka mashitaka kuwashitaki watakatifu wa Mungu kila wanapokosea.

SHERIA ama KATIBA ZINAZOTUMIKA INAYOTUMIKA ni sheria za Mungu NENO LA MUNGU ama kitabu cha biblia BIBLIA hii ndio kama katiba ya milele inayouhukumu ulimwengu wote sasa na hata siku ya hukumu ya mwisho mbeleni future.Dunia na ulimwengu utapita lakini neno la Mungu litasimama halitapita..hakuna katiba mpya wala sheria mpya ni neno lile lile la Mungu litasimama BIBLIA TAKATIFU milele.

kutokujua sheria haikuondelei kosa hivyo ni vizuri tukajua sana sheria ya Mungu neno la Mungu ili tusije tukaangukia katika dhambi(NENO la Mungu tuliweke moyoni mwetu kwa wingi ili tisitende dhambi,kuijua sheria ya na katiba ya kitabu cha hukumu.

upande wa MASHITAKA(ufalme wa giza ,shetani ,mapepo ,wachawi)

Unafungua kesi za mashitaka kila dakika dhidi yetu pale tunapovunja sheria ya Mungu (KIUKA NENO LA BIBLIA NENO LA MUNGU) kwa kutumia ishahidi wa kisheria wa kimaandiko..

kitu cha kujua..KILA DHAMBI unayoifanya hata kwa SIRI DHAMBI ZA SIRI (za moyoni mwako) ufalme wa giza unazijua ,kitu cha kufahamu ukitenda dhambi tu ile dhambi inapiga kengele inapiga kelele au inaonekana kwenye kioo au television (HAKUNA DHAMBI YA SIRI ) utakayoifanya Shetani na mapepo wachawi wasijue au wasio one yani wewe ni kama KIOO kinachoangaza kuonyesha maisha yako ya dhambi na utakatifu wako kwa shetani na mapepo na wachawi na hata mbele za Mungu kila kitu unachofanya na hali yako ya kiroho ,kama ukiwa mtakatifu otaonekana wazi na kama umefanya dhambi sekunde hiyo hiyo itaonekana(wewe ni kama BARUA inayosomeka katika ulimwengu wa roho hakuna kilichojificha huwezi kumdanganya Mungu wala huwezi kumficha shetani,hata dhambi za moyoni mwako zinaonekana ,asiloweza kulijua sheteni kuhusu wewe ni mawazo yako unawaza nini ila pindi ikitenda dhambi tu INAREKODIWA video inaonekana kwwnye screen haijifichi.
INAKUWA USHAHIDI hata kama ni dhambi ya SIRI ya ndani ya moyo.

MASHITAKA anayotushtaki nayo shetani ni DHAMBI zetu kwa kuwa anazijua dhambi zetu na yeye shetani ndiyo baba wa uovu ndio kiongozi wa uovu na dhambi toka mwazo ndiye anayepeleka mashitaka mashitaka YANAPELEKWA KILA DAKIKA (umetenda dhambi shetani anafungua kesi kupeleka kwa Mungu kukushitaki KUKATA rufaa kupinga KUZUIA MAPINGAMIZI mahakama ya Mungu ILI kuzuia maombi yako ,yani ili Mungu asikubariki,asijibunmaombi yako ,na UPATE HUKUMU ya kuadhibiwa au mapepo wachawi shetani apate uhalali wa kukushambulia.

MAMBO YA KUFANYA KWAKO
1) Maisha ya TOBA tubu mara kwa mara,omba ROho mtakatifu akuonyeshe dhambi zote ulizofanya ndani ya siku nzima tokanimeanza na tubu haraka mapema kabla ya siku kuisha kabla hujalala usilale ukiwa hujatubu dhambi zako ulizofanya ambazo zimemuhuzinisha roho mtakatifu hata kama ni zile unazo ona ni dhambi ndogo ndogo na hata ulizozisahau au ambazo hukujua .(TOBA na kuomba kutakaswa)

2.SAMEHE WATU usiweke kinyongo kubeba watu moyoni kitokusamehe vinyongo,chuki na hasira hata kama aliyekukosea hajakuomba msamaha ama unahisi hastahili kusamehemwa msamehe kwa ajili ya faida yako mwwnyewe.

mfano..MKE alimfumania MUMEWE sasa akaweka kinyongo na kuyokusamehe ..kupitia hiyo dhambi ya kutokumsamehe mume wake aliyefanya dhambi ya uzinzi/uasherati ..inapelekea shetani kupata uhalali wa kisheria kukushambulia kwa sababu
atendaye dhambi ni wa Ibilisi; kwa kuwa Ibilisi hutenda dhambi tangu mwanzo.na tena mshahara wa dhambi ni mauti na zaidi dhambi zetu zinatutenga na Mungu

KWA KIFUPI DHAMBI INAFUNGUA MLANGO wa kuruhusu shetani akushambulie zaidi.

tena atashambulia zaidi hiyo hiyo NDOA yako kwa kitendo cha wewe mwanamke kutokumsamehe tu mumeo kwa vile amefanya uzinifu/uasherati..Shetani atakusukumia maroho ya MAGOMVI,CHUKI HASIRA,na HATA KUVUNJA KUTENGANA kuvunja ndoa ,kabisa,na hata kudhuru familia na maisha ya kiroho na inada zako...

itambue mitego ya SHETAni ukitambua Silaha wanazotumia ulimwengu wa giza ukiwapeleleza siyo vibaya kujua ulimwengu wa giza unavyofanya kazi kuharibi kushambulia watu wa Mungu,hata JOSHUA alituma wapelelezi kuipeleleza maadui waliokuwa wanakalia nchi ya KAANANI..ukimjua adui yako utajua pia namna ya kupambana naye na silalaha anazotumia.

Mwanamke ukimsamehe mume wako ukaondoa kinyongo utaiponya ndoa yako na maisha yako ya kiroho wewe mwenyewe .

VINYONGO KUTOKUSAMEHE (unforgiveness,bitternes,na uzinzi/uasherati )ni moja ya mashitaka yanayopelekwa kutishitaki na kufungulia mlango wa kuingiza MAUTI katika maisha yetu...USIMPE SHETANI NAFASI ..usimruhusu usimfungulie mlango..huo ni mfano mmojawapo ipo mifano mingi ya vinyongo na kutokusamehe.

3)...TUMIA DAMU YA YESU katika hukumu DAMU ya YESU inatupa NEEMA yani kama ni kesi inalipa FAINI au DENI zetu au inafuta mashitaka kwa kulipa gharama ya tuliyostahili adhabu DAMU YA YESU inalipa in FULL..

sasa hata kama kesi ni kubwa kiasi gani,lakini hii neema ya damu ya Yesu siyo ya kuichezea yani kurudia rudia kufanya dhambi kwa makusudi kwa kuwakuwa kuna neema ya damu ya Yesu..BIG NO.!!!

Unapoanza siku funika siku yako kwa damu ya Yesu,akili zako nafsi yako,watito wako,nyumba yako ,jifunike kwa damu ya YESU na familia yako na kila jambo lako ,kazi yako,ndoa yako ,milango ,madirisha FUNIKA KWA DAMU YA YESU na usiku kabla ya kulala funika kwa damu ya Yesu.
Tunahesabiwa haki kwa kupitia Yesu mwenye haki,na kwa kupigwa kwake Yesu sisi tumepona,Yesu amechukua dhambi zetu na adhabu yetu.

Ufunuo 12:11
Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-kondoo,



4)KUMSIFU MUNGU katikati ya mateso katikati ya shida na dhiki.
Mungu wetu anakaa katika sifa ,yani ni sawa na kukata rufaa kwenda kumfukia Mungu kwa njia ya sifa,na ile kumsifu Mungu ukiwa katikati ya mateso magumu unayopitia ni lugha unayo ongea kumwambia Mungu pamoja na haya magumu yote adui amenitendea amenifanyia ila bado wewe kwangu ni BWANA hii hi kumfikia Mungu anayekaa katika sifa.

Zaburi 22:3
Hata hivyo, wewe ni mtakatifu; wewe watawala na kusifiwa

yani ni sawa na kumwambia Mungu hata yanipate mabaya kiasi gani hata adui anitende mabaya kiasi gani hata nichinjwe shingo katika hali yeyote ile wewe Mungu kwangu ni yote katika vyote hata nikose vyote wewe Mungu kwangu unatosha ,ni sawa na kusema ,Mungu kwangu wewe ndio kila kitu,hakuna cha kunitenga na upendo na wema wa Mungu.

mfano mzuri ,PAULO NA SILO walipofungwa gerezani wakiwa wamegungwa minyororo katikati ya gereza waliomba,milango ya gereza na minyororo iliyowafunga ikafunguka..



Kamwe usije ukamlalamikia Mungu usimnungunikie Mungu hata kama unapitia shida usilalamike hata kama unapitia mateso makubwa kiasi gani ,wewe msifu Mungu ,wengi wamepokea uponyaji na wameona wanapoea majibu kupitia kumsifu Mungu katikati ya MATESO na majaribu makubwa waliyokuwa wanapiatia.

Mdo 16:25
Lakini panapo usiku wa manane Paulo na Sila walikuwa wakimwomba Mungu na kumwimbia nyimbo za kumsifu, na wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza(Mara, milango yote ikafunguka na minyororo iliyowafunga hao wafungwa ikaachana.

minyororor maana yake ni vifungo vyote vya shetani vinavyokutesa na mashitaka yote ,usiangalie minyororo ya mwilini na milango ya jengo la gereza.

gereza ni mambo yako yaliyofungwa maeneo mbalimbali.


5)KUWAJALI WAHITAJI"

hii ni kusaidia wale wasiojiweza wanyonge ambao hutarajii wakulipe fadhila yoyote na wala sio kwa lengo la kupata sifa au kujioyesha,ni tofauti kusaidia watu waojiweza marafiki zako ukiwa na lengo kuna siku na wao watakulipa fadhila kama unawakopesha utakuja kulipwa.

Mit 19:17
Amhurumiaye maskini humkopesha BWANA; Naye atamlipa kwa tendo lake jema.

sasa hapa ukimsaidia masikini ni sawa na kumkopesha MUNGU mwenyewe na lazima atakulipa mema,hapa hata shetani aje na kesi yake kukushitaki unampiga knock out.

lakini mkono unaotoa ndio unaobariwa kuliko unaopokea,lakini ukiwapa watu vitu utapokea kwa kipimo cha Mungu kilichosukwa sukwa na kusindikiwa hata kumwagika.

lakini dini iliyo safi isiyo na taka ni kuwasaidia wahitaji,Yakobo 1:27
Dini iliyo safi na isiyo na hitilafu mbele ya Mungu Baba ni hii: Kuwasaidia yatima na wajane katika shida zao,

zaidi ya yote ni hii

ZABURI YA 41
Heri amkumbukaye mnyonge;
BWANA atamwokoa siku ya taabu
.
2BWANA atamlinda na kumhifadhi hai,

Naye atafanikiwa katika nchi;

Wala usimtie katika hali wamtakiayo adui zake
.
3BWANA atamtegemeza alipo mgonjwa kitandani.
Katika ugonjwa wake unamponya maradhi yake.

(wanaojua siri hii utawakuta wanatoa sana misaada kwa masikini na wahitaji,ni vizuri tuwe na maarifa mbona wana wa giza wana maarifa sana katika kututenda maovu,na sisi tuwe na maarifa ya KIROHO)

6)KUTII SHERIA/NENO YA MUNGU
Submissive kutii hata kile ambacho unaona kinakunyima starehe ama raha ya mwili au hata kama kinaonekana kinafurahisha mwili.

mfano..mfanyakazi mkoja wa taasisi moja alipata JARIBU mtihani ,boss wake alimlazimisha afanye kughushi udanganyifu ofisini kwake ili waweze kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu ..lakini yeye alisimama akisema hiki kiti ni siwezi kufanya kwa sababu ni dhambi kwa Mungu ni bora kama ni kazi nipoteza kazi lakini sipo tayari kufanya dhambi ya udanganyifu na wizi ,..mwisho wa siku yule bosi alietaka kumfukuza kazi kwa kukataa kutii agizo la kufanya udanganyifu wa wizi wa kalamu,kukipatia pesa alifukuzwa kazi yeye na yule aliyelinda uaminifu mbele za Mungu alipandishwa cheo.

Meshacj ,shedrak Abednego walikataa kuabudu sabamu ya nebukadreza wakatupwa kwenye tanuru la moto ila Mungu akawaoko kwa kuwatumia malaika hata kwwnye tundu la simba.

Zab 1:2-3
Bali sheria ya BWANA ndiyo impendezayo, Na sheria yake huitafakari mchana na usiku. Naye atakuwa kama mti uliopandwa Kandokando ya vijito vya maji, Uzaao matunda yake kwa majira yake, Wala jani lake halinyauki; Na kila alitendalo litafanikiwa.

Zab 119:
Moyoni mwangu nimeliweka neno lako, Nisije nikakutenda dhambi.

huyu DAUDI aliyeandika zaburi hata moyoni mwake anasema hana kiburi,na hata kutubu dhambi alikuwa mwepesi kutubu dhambi kwa haraka mara kwa mara.

ndiyo maana alimpendeza Mungu.

so utii ni bora kuliko dhabifu yani kumtii Mungu ni bora zaidi kuliko.

kwa maana ya kusikia na kuyafanya mapenzo ya Mungu.

YESU ANAKUPENDA Isa 53:5

Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake,

Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.
*KUHUSU KUTOKUSAMEHE-- unforgiveness,bitterness ,kinyongo.

reply by

"zinginary" JF member

SWALI:=??


DUNIA YA SASA KUSAMEHE UNAONEKANA BOYAA NA DHARAU KIBAO ZINAONHEZEKA. BORA KISASI

JIBU

Kusamehe si kwa ajili ya aliyekukosea ila kwa faida yako mwenyewe na kwa sababu ya kutii neno la Mungu.

Mt 6:14-15

Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao, na Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi. Bali
msipowasamehe watu makosa yao, wala Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa yenu.

sasa kama sheria ya MUNGU ndiyo hiyo kuwa kama wewe husamehi watu makosa yao na wewe hustahili kusamehewa.


kama sisi nasi Mungu asipotusamehe makosa yetu mana yake tunastahili mshahara wa dhambi ambao ni mauti.

Rum 6:23 S
Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti;


KUSAMEHE NA KUACHILIA WATU MOYONI KUSAHAU KABISA NI BORA KULIKO KUBEBA KINYONGO MOYONI.
 
Back
Top Bottom