Edward Ngoyai Lowasa aka laighwanan, kama watanzania wote tujuavyo, ameonyesha uchu mkubwa wa madaraka wa kuutaka urais ambao haujawahi kuonekana toka nchi ipate uhuru. lo-rushwa ametumia kila mbinu iwe safi au chafu kuhakikisha kwamba lazma 2015 ccm ndio inamteua kubeba bendera ya ccm.
Nionavyo mimi mambo ambayo yatatokea lo-rushwa "akila za uso" kama malecela, na kutemwa na ccm ni haya
1. lo-rushwa ataacha kugawa hela zake chafu misikitini, makanisani. nawashauri mapadri na mashehe watafute vyanzo vingine vya mapato
2. lo-rushwa ataacha kuvilipa vikaragosi vyake mitandaoni. navishauri vitafute kazi ingine.
3. lo-rushwa hatawaalika tena wenyeviti wa ccm wa mikoa mwisho wa mwaka mondul na kuwapa kila mmoja bahasha ya ts 500 000/=
4.lo-rushwa ataacha kuwaganjia wajumbe wa vikao vya maamuzi rushwa
5. lo-rushwa atacha kuvihonga baadhi ya vyombo vya habari
6. l-rushwa ataacha kuwachafua wenzake
wa-tz wenzangu mnaona nini kingine kitatokea?
Mkuu Galiya, asante kwa taarifa hii.
Ukweli ni huu!, rais wa Tanzania kwa mwaka 2015, sii mwingine yoyote bali yule tuu aliyeandikiwa na Mungu, kuwa atakuwa rais wa JMT mwaka 2015!.
Hakuna binadamu yeyote ajuaye ni nani aliyeandikiwa kuwa rais wetu, 2015, na wote wanaousaka urais ni watu tuu wenye wish, kama Mungu alivyotufundisha, "ombeni mtapewa!", "tafuteni mtapata!", na "bisheni hodi, mtafunguliwa!", hivyo hao watafuta urais, wote ni waombaji, watafutaji na wabisha hodi, only "the choosen" one ndiye atakayepata, na huyo "the choosen one" ni "one and only!".
Kwa vile hakuna ajuaye ni nani aliyeandikiwa, Mungu anayo namna yake ya kutenda, ikitokea aliyemuandikia ndiye huyo huyo unayemtaja, basi ni lazima atakuwa yeye!, inyeshe mvua, liwake jua, "liandikwalo ndilo liwalo!", alilolipanga Mungu, binadamu hawezi kulipangua!.
ila pia Mungu hupenda kujidhihirisha uwepo wake pale ambapo hakuna aliyetegemea!, kwa kuwafanya watu mioyo yao iwe migumu, ili kujidhihirisha utukufu wake, kwa kumnyanyua asietarajiwa kabisa!. Tumemshuhudia akimchukua mtu low life, "mvuvi tuu wa samaki", na kumuinua na kumgeuza kuwa "mvuvi wa watu!", akamwambia "Wewe Mwamba!, juu ya mwamba huu, nitalijenga kanisa langu!", akatuambia, atawaonyesha mataifa jinsi "Jiwe walilolikataa waashi, litafanywa kuwa ni jiwe kuu la pembeni!".
Na kama wewe uko kwenye lile kundi mnaoamini kuna jambo fulani haliwekekani, nakuhakikishia "there is nothing imposible under the sun!", lisilowezekana kwa binaadamu, kwa Mungu linawezekana!.
Rais wa Tanzania kwa mwaka 2015, tayari yupo, ameishaandikiwa, amaisha pangiwa, kinachosubiriwa sasa ni kusubiri tuu ile siku na saa ya kuapishwa!, na yeyote atakayeapishwa siku hiyo, huyo ndiye aliyeandikiwa hata ikitokea akawa ni Galiya!, huyo ndiye!.
Pasco.