Nini hatma ya Lowassa akikosa urais 2015?

Nini hatma ya Lowassa akikosa urais 2015?

Nimeziona juhudi za Lowasa ktk kuutafuta Urais wa jamhuri ya Tanzania kwa hali na mali kabla hata hajapata kashfa ya Richmond iliyomwondoa ofisini.

Aliposhinda Kikwete mwaka 2005 kila mtu alijua Lowasa atakuwa PM. na hakuna aliyeshangaa Lowasa kuwa PM wa nchi hii maana walijua anaandaliwa kuwa Rais mwaka 2015.

Lakini hata alipotupwa nje ya serikali kwa kashfa ya ufisadi bado hajapoteza matumaini ya kuongoza nchi hii. anafanya harakati za kujisafisha na kufanya publicity kila kukicha. anatoa misaada ya fedha, anakubali kila mwaliko, anafanya shughuli za kijamii ili tu kujipatia credit ya urais 2015.

Amefika mbali zaidi kwa kutumia media kujisafisha na kujipigia debe kwa gharama kubwa. (pitia gazeti la Rai leo).

SWALI:JE LOWASA ATAFANYAJE AKIUKOSA URAIS ANAOUOTA KILA SIKU? EITHER KWA KUKATALIWA NDANI YA CHAMA CHAKE ASIPITISHWE AU KWA KUKATALIWA NA WATANZANIA. JE ATAJIUA? ATATUBU NA KUMRUDIA MUNGU? ATAKIMBIA NCHI? ATASTAAFU SIASA? AU ATAFANYAJE?!!!!!!!!!!!!

Atakuwa muuza madawa na mfugaji
 
Kama kigezo ni U Dr. basi bora hata Dr. Ulimboka!
Mkuu siasa za tz ndo zilivyo itakavyokuwa ni kama ilivyofanyika kumuweka spika Makinda. Dr. ASHA ROSE MIGIRO ndo habari ya mjini kwa chini chini.
 
Mkuu siasa za tz ndo zilivyo itakavyokuwa ni kama ilivyofanyika kumuweka spika Makinda. Dr. ASHA ROSE MIGIRO ndo habari ya mjini kwa chini chini.

Nahisi kwenu kiongozi wa familia ni mama sio baba mbona umaongea mapera sana bora hata ungeongea machumgwa hizo habari ya mujini uliziweka wewe kuwa dr.asha anagombea ama usikurupuke
 
Nahisi kwenu kiongozi wa familia ni mama sio baba mbona umaongea mapera sana bora hata ungeongea machumgwa hizo habari ya mujini uliziweka wewe kuwa dr.asha anagombea ama usikurupuke

mkuu unayo ambiwa yako waz kabs,usitake utafuniwe kila kitu,hatakma hujui kusoma hata picha inakushinda!!hutaki unaacha
 
Nahisi kwenu kiongozi wa familia ni mama sio baba mbona umaongea mapera sana bora hata ungeongea machumgwa hizo habari ya mujini uliziweka wewe kuwa dr.asha anagombea ama usikurupuke

Mkuu wala usipiniki twende taratibu kama hujazipata tulia ndo unaambiwa hivo hata mi nimeshangaa ndo maana nimesema ni tetesi na hii nimliquote mdau hapa kwenye thread hii hii fuatilia utaona alikuwa analalamika kuwa anasikia kuna tetesi CCM wanataka kumuweka mgombea mwanamke. Mimi nimefanya kulitaja tu hilo jina la huyo mwanamke ambaye ni dr. ASHA ROSE MIGIRO, tatizo liko wapi hapo hadi unapaniki mkuu? Tafakari.
 
Jibu la hoja yako ni jepesi sana. Uwezekano wa vikao vya juu vya ccm (hasa kamati kuu) kupitisha jina la EL, SS au mtu mwingine anayoonekana kutoka kwenye kambi moja hasimu na kambi nyingine ni mdogo au niseme haupo. Kitakachofanyika baada ya EL kuondolewa kwenye mchujo wa awali, atagombea kama mgombea binafsi kama katiba mpya itaruhusu hivyo. Hata hivyo, kutokana na taswira yake kwa watanzania walio wengi na hasa wapiga kura vijana kuwa si nzuri kutoka na kashfa ya ufisadi ambayo haijafutika na haiwezi kufutika kabla ya 2015, hawezi kushinda uchaguzi. Atakachofanya ni 'kusaidia' kupunguza kura za ccm na kumpa nguvu mgombea wa upinzani. Mzee SS kwa upande wake, anaweza kukubali yaishe na kusubiri zawadi ya uwaziri, ubalozi au cheo kingine.
Mh. Tashwira ipi mbaya kwa vijana kumhusu Lowassa? Hao vijana unaosema ni wale wa Bagamoyo au Mchambawima Zanzibar? NB: awamu hii hatutaki rais Juakali, mwendo uleule wa Kenya pia neno Fisadi ni mtu anayemnyemelea mke wako kaka!
 
mkuu unayo ambiwa yako waz kabs,usitake utafuniwe kila kitu,hatakma hujui kusoma hata picha inakushinda!!hutaki unaacha
Mkuu afadhali umeliona hilo lakini jamaa amepaniki utafikiri kuna ugomvi hapa kumbe tunapeana habari tuzazozisikia na zingine tunazoziona kwa hiyo siyo lazima wewe tu ndo uwe umeziskia ama unataka habari ile tu itakayokufurahisha.
 
Atakufa tuu au aisehie ktk comma....km hii miaka ya JK 8 tuu tayari keshachoka vumilia.
 
Mkuu siasa za tz ndo zilivyo itakavyokuwa ni kama ilivyofanyika kumuweka spika Makinda. Dr. ASHA ROSE MIGIRO ndo habari ya mjini kwa chini chini.
Sina chuki na akina mama kwani bila mama nisingechangia lolote hapa JF. Hii inchi si ya kuongoza umebeba lipshine kwenye mkoba inatakiwa komandoo la kimasai lenye viatu maarufu kama "katambuga,fullstop!
 
Be informed, huna hoja madhubuti hapa..vinginevo sema kama wewe umekuja kupima upepo, poor mind!, unajua serikali ndio inahusika na umaskini wa kila mahali tanzania bila kujali hili au lile ni jimbo la mbuge gani?...Nani alikwambia majimbo ya wapinzani wabunge ndio wanaleta maendeleo? wapinzani wanaserikali?...hufaham kwamba chama kilichoko madarakani ndicho chenye serikari na serikali hiyo ndio yenye jukumu la kuleta maendeleo kupitia ilani ya chama chake? akili finyu ni hasara kwa mtumiaji na anao kaa nao, you are useless[/]#SAFI SANA b'cause most are ignorant! they dont think deep!
 
E. L. asipopitishwa kugombea au say akagombea akashindwa, hautakuwa mwisho wa chama chochote hapa nchini. Kwani alianza lini kuusaka u-jk, na akashindwa..?? Kwa sasa watz ambao tunauwezo wa kuiongoza nchi tupo wengi sana..!! Ukiona biashara ya jumla inakula kwako unajaribu biashaara ya rejareja babaangu.
 
Lowassa,Wassira,Membe na Sitta kuna mchuano mkali sana.
 
jamani mnataka EL aseme nini tena?,kwamba atagombea anagombea mara ngapi?,anatoa misaada kwa watanzania kwa huruma gani?,anatembea na mabilionea kila anakokwenda kwa kigezo cha marafiki zake,mbona hawataji kwa majina?

Alipokuwa moshi alisema kuna rafiki yake atagharamia uwekani miundombinu kwenye ujenzi wa mwalimu SACCOS kwa gharama ya sh,Milioni 400 wakati mahitaji ni mil.100,huyo rafiki yake mbona hajamtaja?.

Hofu yangu ni afya yake naiona kwa mbali kama inamgogoro kidogo,anatembea kama mtu anayehitaji uangalizi wa karibu,kama mnabisha jaribuni kumuona live wakati akitembea mtaona.tumtakie kila la heri maana urais ni gharama.

ujumbe wa leo-IKULU NI PAHALA PATAKATIFU,TUMUULIZE EL ANAUTAFUTA URAIS KWA GHARAMA KUBWA KIASI HICHO NANI ATAMREJESHEA HIZO GHARAMA?,NA HAO MARAFIKI ZAKE NANI ATAWAREJESHEA HAYO MAMILIONI YA FEDHA KAMA SI KUPEWA UONGOZI NA EL?
 
Atakaa kama raia wengine na kumheshimu aliyechaguliwa.

Ataomba ahamie chadema halafu chadema watakataa hapo ndipo ile stroke yake itakapoamka atapelekwa ujerumani hapo ndiyo mwisho
 
Back
Top Bottom