Ningekuwa mwana CHADEMA ningeshauri tukio kubwa tarehe 05 Novemba, 2016

MWONA MBALI

JF-Expert Member
Oct 7, 2016
460
610
Nilisha andika mahala kuwa CHADEMA ni chama kikubwa ila idara yake ya uenezi na propaganda ni dhaifu sana.

Ningekuwa mwana CHADEMA labda ningeshauri wasingeiacha tarehe 5 November ipite kama inavyopita.

CHADEMA ni chama cha mawazo ya pili , yaani mawazo shindani leo hii raisi ameitisha kikao na waandishi wa habari kuzungumzia mazuri na changamoto za utawala wake, upande wa pili pia ulikuwa na haja ya kusikika ili kuipa changamoto serikali.

Ni masikitiko yangu kuwa CHADEMA haina watu wa mikakati ya kisiasa, watabaki kudandia matukio wasio weza kuyamaliza kama operation ukuta na sasa wamedandia hoja ya muswada wa habari (ukisoma mazungumzo ya rais na wana habari ) utagundua hoja hii imeshapita tayari na CHADEMA wanapambana kushindwa tu.

Ningetamani kuona CHADEMA inatumia fursa za kisiasa zilizopo kwa mfano ingekuwaje kama CHADEMA wangeandaa dua maalum ya kuliombea taifa na hutuba fupi za ndani wakaalika waandishi na kuipa siku hii ujumbe maalum kama ''Tanzania yetu na uhuru wa kidemocrasia' au 'wakati ukuta' au wakaipa siku jina maalum kama 'maumivu day' ili mradi hii siku isipite bila kuwa na maoni ya upande wa pili.

Nasikitika sana kuona fursa hii hawakuiona kama zilivyopita zingine, kwa kutokufanya hivyo wanaruhusu mashambulizi ya kisiasa yaje upande wao na mwisho wa yote ni CHADEMA kutoaminika kwa jamii.

Badala ku kuandika meseji za kutukana wakuu wa mikoa kama alivyofanya Lema ni vizuri wangetumia akili zao kuimarisha idara yao ya uenezi na propaganda.

Nawasilisha
 
Jina Magufuli ndio shida kwa sasa CDM
Wana nchi hawana muda tena wakurubuniwa na hawa wasaka tonge

Leo Rais kamaliza
Anakuambia unakuta mtu anamdomo mrefu kuongea na kwa kuwa yupo upinzani unaona kama mzalendo
Kumbe nihatari.
Mfano kasema wapo wana siasa tena upinzani ambao wamekopa pesa nyingi mno
Kuruudisha imeshindikana
Na ukiangalia uwezekano wa kurudisha haupo,
taasisi iliyo kopya ikifilisika wa kwanza kunyoosha mdomo wao!!!

Tumuunge Mkono Rais wetu huyu,
Watanzania tumempata mtetezi wataifa,
Hawa wanaojiita wapinzani hakuna lolote zaidi ya maslahi binafsi.

Unaishi kwenye nyumba ya serikali hulipi kodi
Wewe ulitakiwa kuwa kioo cha jamii kumbe nawe Fisadi tu!!!
 
Jina Magufuli ndio shida kwa sasa CDM
Wana nchi hawana muda tena wakurubuniwa na hawa wasaka tonge

Leo Rais kamaliza
Anakuambia unakuta mtu anamdomo mrefu kuongea na kwa kuwa yupo upinzani unaona kama mzalendo
Kumbe nihatari.
Mfano kasema wapo wana siasa tena upinzani ambao wamekopa pesa nyingi mno
Kuruudisha imeshindikana
Na ukiangalia uwezekano wa kurudisha haupo,
taasisi iliyo kopya ikifilisika wa kwanza kunyoosha mdomo wao!!!

Tumuunge Mkono Rais wetu huyu,
Watanzania tumempata mtetezi wataifa,
Hawa wanaojiita wapinzani hakuna lolote zaidi ya maslahi binafsi.

Unaishi kwenye nyumba ya serikali hulipi kodi
Wewe ulitakiwa kuwa kioo cha jamii kumbe nawe Fisadi tu!!!
Rais Aliposema Kuna Wana Ccm Wa Hovyo Kabisa Nadhani Nawe Ni Mmoja Wao!
 
Mkuu acha kuwadhalilisha Chadema kwamba hawana watu wa mikakati wakati Lowasa, Sumaye na yule CCM mwingine aliyeko Chadema juzi walikuwa bungeni kuwafundhisha wabunge wa Chadema(Mbowe akiwemo) namna ya kujenga hoja bungeni.
 
Back
Top Bottom