Ninawaza kugombea jimbo HAI 2015

Very simple ila masharti yafuatayo uyatimize
1) uwe unatokea kaskazini mwa tz
2) uwe na undugu wa karibu na mtei
3) uwe na mtaji na magari kama mafuso au maloli yenye uwezo wa kukodishia cdm kipindi cha uchaguzi
4) uwe m..st.. safi
5) uwe mvumilivu hadi pale mbunge wa sasa atakapochoka au ku...ki (inshort ile safari ya kila mtu)

Nakutakia kila la kheri

ndugu yangu ubunge ni kazi ya mtu masikini ambaye anajua shida za wananchi wa kawaida kama tukiendelea kuamini mpaka uwe na pesa ndiyo utapata ubunge basi hawa wafanyabihashara wataendela kurisishana nafasi za uongozi kama ilivyo sasa.mimi sina vyote hivyo ila kichwani mwangu yapo makubwa kuliko hayo kwa faida ya walalahoi wenzangu si mabepari
 
Wadau sijasubiri niseme wazee wameniomba,ila ni nafsi yangu sasa imejiridhisha kuwa wakati umefika nami sasa nirudishe nguvu walizotumia watu wa nshara,uduru,lyamungo,masama,narumu,mronga,lambo,kisereni,mkweseko,uswoa,mkwarungo nk. kwa kunielimisha vya kutosha.ni zamu yangu sasa kuwaongoza kuijenga nchi yetu na kudai haki zetu kwa pamoja.

si kwamba Mhe Freeman ameshindwa kazi la hasha.ni kumpa nafasi aweze kufanya kazi zake ndani ya chama katika ngazi ya taifa.

wakati ukifika nitawakumbusha hapa jamvini,kwa kuja na utambulisho rasmi na sababu za mimi kuamua hilo.

najua mtapenda kujua ni chama gani? ni nani? ila muda ukifika yote mtajua.

Mie nadhani unge gombea uraisi, maana ndiyo hasa penye tatizo la msingi.....au wewe huyu unamwona bonge la Obama?
 
kwani kuwasaidia wananchi wa hai mpaka uwe mbunge? braza kumsupport Mbowe katika harakati zake Hai ni kuwaletea wananchi wa hai maendeleo!
mbowe afanya shughuli za kitaifa brother. hivi mbowe anajua daraja la lwamungu pale weruweru linafananaje?, na kwingine kwingi ambapo kwa hadhi yake na mfumo wa maisha aliyoyakuta kwa mzee Aikaeli na Mama Aishi hawezi kuyafahamu,wala kuhisi maisha magumu waliyonayo watu pale narumu.ebu jiuliza sasa anahabari kuwa kuna janga la kumbunga kilichosababisha ndizi nyingi ajabu zikagondoka hali inayoleta njaa kubwa hai?,simlaumu hata kidogo ila anakazi nyingi za kitaifa atakumbuka lini haya?
 
Wewe mwenyewe hujiamini nani atakupa huo uongozi maana kama unajiamini ungeingia na ID Name sahihi lako la kiserikali wewe unaingia na ID za KiJF, embu tuondokee hapa usituletee ukomedi wako hapa

Mkuu habari'umempa ya kweli huyu kimboka anaonekana ni porojo'kama wamekusomesha mbona tupo kibao tuliosomeshwa'kama unamaanisha ingia kwa id ya kweli na jitambulishe'mimi natoka lyamungo wewe unatoka wapi?sasa hivi unaishi wapi au unataka urudi kwa sababu ya ubunge umekuwa joshua nasari?kuhusu chama utapitia kipi??mkuu hujanishawishi bado!
 
Mkuu habari'umempa ya kweli huyu kimboka anaonekana ni porojo'kama wamekusomesha mbona tupo kibao tuliosomeshwa'kama unamaanisha ingia kwa id ya kweli na jitambulishe'mimi natoka lyamungo wewe unatoka wapi?sasa hivi unaishi wapi au unataka urudi kwa sababu ya ubunge umekuwa joshua nasari?kuhusu chama utapitia kipi??mkuu hujanishawishi bado!

mi nitajitambulisha usiwe na haraka,tena wewe lyamungo ndiyo unajua shida ya kupanda ile milima pale ukitokea makoa,mimi nashukuru Mungu nimeishi mikoa yote ndani ya Tanzania lakini kila mwaka lazima niende hai na kila kijiji ninakifahamu vizuri na mahitaji yao sasa ni mwaka wa tano tangu nimeanza utafiti wangu ambao nitawapa wana hai soon
 
kwani kuwasaidia wananchi wa hai mpaka uwe mbunge? braza kumsupport Mbowe katika harakati zake Hai ni kuwaletea wananchi wa hai maendeleo!

unaitaji tendi uneni (legal power and authority) ingekuwa hivyo wengi wangesaidia sana nchi hii
 
ndugu yangu ubunge ni kazi ya mtu masikini ambaye anajua shida za wananchi wa kawaida kama tukiendelea kuamini mpaka uwe na pesa ndiyo utapata ubunge basi hawa wafanyabihashara wataendela kurisishana nafasi za uongozi kama ilivyo sasa.mimi sina vyote hivyo ila kichwani mwangu yapo makubwa kuliko hayo kwa faida ya walalahoi wenzangu si mabepari
uongozi ni ni wito na kipaji toka kwa Mungu si umasikini wala utajiri, kama maisha yamekuwia magumu unataka kuneemekea kwenye ubunge umechemka,
 
hizo ni siasa za majitaka.sifanyi kazi ya kuhubiri mambo ya watu
mara mbowe tajiri kwanza anafanya kazi za kitaifa, mara oo sifanyi kazi za kuhubiri watu! Vipi broo mbona unajichanganya uko kama gia 1 haikai, 2 haikai 3 inafyetuka.
 
Una lipi jipya?
Au unataka kula posho tu huku ukijidai unataka kutusaidia?
 
nilimaanisha mkoa wa kilimanjaro,ambapo ndani yake kuna wilaya ya HAI

Mkuu mimi nakuunga mkono fanya haraka achana na wanaokukatisha tamaa

Inaonyesha una ufahamu mkubwa wa matatizo ya wananchi..keep it up

Nenda kagombee
 
Back
Top Bottom