Ninatamani kurudi kwake...

Ninatamani kurudi kwake...

Acha kulialia hapa mtoto wa kiume!


mijitu mingine inaudhi ujue mkuu, sasa kilichomfanya amuache hata hakieleweki anataka Sisi tumshauri nini wakati hajapambanua kwa nini alimwacha binti wa watu,hawa ndio wanaotufanya mabinti warembo wote watuchukie wanaume wote kwa tabia hizi za kishenzi
 
mijitu mingine inaudhi ujue mkuu, sasa kilichomfanya amuache hata hakieleweki anataka Sisi tumshauri nini wakati hajapambanua kwa nini alimwacha binti wa watu,hawa ndio wanaotufanya mabinti warembo wote watuchukie wanaume wote kwa tabia hizi za kishenzi
Halafu mademu kibao tu! Hili lazima kutoka ile mikoa ya Kule tu. Hapa Dar mambo ya kulialia tushasahau
 
Dah too sad! Nikushauri kitu, muombe msamaha kwanza uhakikishe amekusamehe bila hata ya kumwambia unataka kurudiana nae muombe sana! Mpaka aridhie yaan make sure amekusamehe! Usipofanya hivo KARMA itakutesa sana! Baada ya kusamehewa chukua kama wiki mbili au tatu! Then muombe mrudiane! Angalizo!! Akikataa usimlazimishe na jiandae kisaikolojia kukubaliwa au kukataliwa mkuu! Madhara ya kurudiana na mtu ambae ulimtesa imani na ww kujengeka itakuwa ngumu! Utatumia nguvu sana kuirudisha imani lakini kwake itakuwa ngumu kukuamini! Lakini pia akikataa usimtenge onesha kumjali kama ilivokuwa mwanzoni bila kinyongo sababu umemkosea sana! By the way najua umemkumbuka sana ila kama ana amani muache aendelee na maisha yake!
 
Eeeh Mungu msaidie huyo dada popote alipo asirudi katika mikono ya huyu mwanaume The Donchop maana wewe mwanaume ni mshen... umenikera sana utafikiri mimi ndo huyo dada na ninaomba upate mdada wa mjini akunyooshe mpaka ushike adabu
 
Mh kumuumiza mwanamke unayeamini anakupenda sana sio jambo zuri kwa kweli, heri kama unashindwa utafute wa kuzugia lakini anaekupenda asijue na usimuache
 
Sasa mkuu demu mwenyewe ulisema asikujue usimjue, na umemchoka na kumdhalilisha vya kutosha..leo hii unataka umrudie..nini kimekupata?? Nakushauri achana nae tu, usizidi kuumiza hisia zake, ulishaharibu hisia zake vya kutosha jambo ambalo sio zuri na hata ukilazimisha useme urudi kwake hakutakuwa na mapenzi ya kweli kubali kataa!!
 
Wanajamii... Wazima?
Ni mwaka sasa tokea nimeachana na aliyekuwa kipenzi changu. Alinipenda sana. Alinipenda nilipokosa kazi na hata nilipopata.
Kuna kipindi nilihisi kumchoka tu. From no where nilimpigia simu nikamwambia asinijue wala nisimjue.
Nakumbuka binti wa watu alilia sana. Kweli alikuwa na mapenzi ya dhati. Aliomboleza kwa zaidi ya miezi mitatu. Mara nyingine alikuwa akija nyumbani kunipigia magoti akiwa amelewa wakati hakuwa mnywaji. Sikuhisi huruma hata chembe.
Nilichotaka ni kutoona sura yake wala kumsikia ingawa mama mzazi alimpenda sana binti.
Sasa nataka kurudi lakini sielewi ndugu zangu, kumuacha kwa maneno yote mabaya vile, leo narudi vipi? Sijaona simu yake muda sasa.
Msaada tutani.

ACHA UJINGA!

PAMBANA NA HALI YAKO!!!


Sent from Mbagala Maji Matitu
 
Namba yake nikusaidie kumuanza wifi yangu lazima atarejea,...wahenga walisema "penzi upofu" atakuwa ajafumbua macho bado
 
Wanajamii... Wazima?
Ni mwaka sasa tokea nimeachana na aliyekuwa kipenzi changu. Alinipenda sana. Alinipenda nilipokosa kazi na hata nilipopata.
Kuna kipindi nilihisi kumchoka tu. From no where nilimpigia simu nikamwambia asinijue wala nisimjue.
Nakumbuka binti wa watu alilia sana. Kweli alikuwa na mapenzi ya dhati. Aliomboleza kwa zaidi ya miezi mitatu. Mara nyingine alikuwa akija nyumbani kunipigia magoti akiwa amelewa wakati hakuwa mnywaji. Sikuhisi huruma hata chembe.
Nilichotaka ni kutoona sura yake wala kumsikia ingawa mama mzazi alimpenda sana binti.
Sasa nataka kurudi lakini sielewi ndugu zangu, kumuacha kwa maneno yote mabaya vile, leo narudi vipi? Sijaona simu yake muda sasa.
Msaada tutani.
Damu ya usaliti ni lazima ikurudie. Ni lazima utateseka kimapenzi.
 
Ivi uliangalia mbele kweli au ndio mwanamke wako wa kwanza? au wewe ndio wale wanaopendwa wakajiona wao ndio mafundi wanajua kusimamia kucha kumbe hata miguu yake kusimamia mtihani? usimpoteze mda mwache apate anae mstahili wewe nadhani type yakoo ni wale rough riders, jiulize nafsi yako kwanini unamtaka tena? analipi jipya lakukupa? au kwanini akukubalie wakati umesha tapika mpaka ukapitiliza kwenu,hakuna kitu kibaya sana kama maneno mabaya,daima kama humtaki mtu bora mwambie mpaka hapa mimi naona basi ila usitoe maneno mabaya kumuudhi binadamu mwenzio hujui una muathiri kiyasi gani kisaikolojia...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom