Wanajamii... Wazima?
Ni mwaka sasa tokea nimeachana na aliyekuwa kipenzi changu. Alinipenda sana. Alinipenda nilipokosa kazi na hata nilipopata.
Kuna kipindi nilihisi kumchoka tu. From no where nilimpigia simu nikamwambia asinijue wala nisimjue.
Nakumbuka binti wa watu alilia sana. Kweli alikuwa na mapenzi ya dhati. Aliomboleza kwa zaidi ya miezi mitatu. Mara nyingine alikuwa akija nyumbani kunipigia magoti akiwa amelewa wakati hakuwa mnywaji. Sikuhisi huruma hata chembe.
Nilichotaka ni kutoona sura yake wala kumsikia ingawa mama mzazi alimpenda sana binti.
Sasa nataka kurudi lakini sielewi ndugu zangu, kumuacha kwa maneno yote mabaya vile, leo narudi vipi? Sijaona simu yake muda sasa.
Msaada tutani.