Ninapenda Magufuli ashinde lakini nataka CCM ishindwe!

Ninapenda Magufuli ashinde lakini nataka CCM ishindwe!

Mkuu nakuunga mkono kabisa....nafsi yangu hainitumi kabisa nimpigie kura Lowassa ingawa nimeipenda chedema kwa mda mrefu sana....nashukuru leo nimepata jibu....kura yangu udiwami cdm, ubunge cdm uraisi nasikitika sana kwamba nitampigia magufuli....kwangu kibaya hiki ni afadhari kuliko lowassa

Kumbe tuko wengi wa mawazo haya. Mimi nimeshabikia na kusapoti NCCR na baadae chadema tangu 1992. Mwaka huu nilikuwa na matumaini makubwa sana na chadema, lakini siyo kupitia kwa Lowassa, huyu nimemkataa siku zote.
Kwa hiyo kura zangu 3 ni kama ifuatavyo:
Rais: John Magufuli (namkubali yeye binafsi, siyo CCM yake)
Mbunge: Julius Mtatiro (namkubali yeye binafsi, siyo CUF yake)
Diwani: Simjui jina (lakini naikubali Chadema, kwahiyo hii itaenda chadema).

Kumbe chadema ingeniwekea wagombea ninaowakubali kwa nafasi zote ningepiga kura kwa raha sana. Au Magufuli na Mtatiro wangekuwa chadema ingenoga sana (hata hivyo bado naona kwa misimamo yao wanafanana na kile ninachopendea chadema, kwahiyo watapata kura zangu kiroho safi kabisa).
 
Magufuli sio mgombea binafsi msitudanganye
Magufuli na Lowassa ni wagombea binafsi.
Magufuli hafanani na CCM kama vile Lowassa asivyofanana na chadema.
Magufuli ni kondoo kati ya mbwa mwitu
Lowassa ni mbwa mwitu aliyejivika ngozi ya kondoo.
Wote wana missions tofauti na vyama vinavyowabeba.
 
Mimi kura yangu kwa magufuri,ubunge ukawa na udiwani ukawa.nimekuwa mpenda mageuzi na hata 2010 nilimpigia dk.slaa.kiukweli Mimi sio mtoto mdogo wa kumwambia karatasi ni pesa
 
Akili ya kuambiwa changanya na yako.Jibu October inyeshe Mvua jua liwake Lowasa Rais

Umepotea brooooo. Wako sahihi. Magufuli kwa urais na wengine upinzani kutegemea na nani aliesimikwa hapo lakini. Namaanisha jimboni
 
Never magufuli and ccm be separated, ni sawa samaki na maji, so think critically b4 deciding
 
Mnatapatapa watu wameamuka ukawa iko juu lowasa tendo la kuhama kateka hisia za wengi hadi vijijini sola kila mtaa watu wanaangalia yanayoendelea hakuna kudanganyana. Lowasa ikulu yake utake usitake.
 
Miye ndo sijui nifanyeje, napenda Ukawa wachukue lakini simkubali Lowasa. Namkubali Magufuli lakini sikubali mfumo wa CCM kuendelea kutawala.
 
Tatizo la wanajamvi mnakuwa kama mmechanganyikwa, Dar sio kwamba ndio tz, unaposema watz wameamua unafanya makosa makubwa sana, mnavomwamini Lowasa nyie msidhani pia wote wanaamini hivo, mfano kwa uelewa wangu wa kawaida sana, Lowasa hana ushawishi wowote wa kufanya nimpatie kura yangu, make hana uwezo wa kufafanua sera zake ili nimkubali, amebakia kusema anachukia umasikini, kwa hali hiyo inanifanya niamini kwamba uwezo wake umepungua aidha kutokana na umri au inawezekana afya sio njema sana. Urais ndo hatima yangu pia urais haujaribiwi hata kidogo, vijana waliowengi wanataka kujaribu urais, miaka mitano ni mingi sana sana.

Labda una matatizo ya macho otherwise nioneshe wapi nimetaja Dar kwenye post yangu. Endelea kujidanganya ila nchi imefikishwa hapa ilipo na washenz.i wa ccm. Unless useme chama gani kingine kimewahi kuendesha serikali.
 
Back
Top Bottom