Ninapenda Magufuli ashinde lakini nataka CCM ishindwe!

Ninapenda Magufuli ashinde lakini nataka CCM ishindwe!

Unaonekana Ni Kada Mzuri Lakini Magufuli Hashindi

Wala sina hadhi ya Kada....lakini nimeshikilia kura yangu kama wewe. Tuitumie vizuri kuweka viongozi wazuri. Rais Magufuli, waziri wa uchukuzi Mbatia unaona inavyopendeza?!!!!!
 
Kapokee buku 7 zako Lumumba.... Ni wehu tu ndio wataichagua CCM

Nimeandika kwa kutumia laptop niliyonunua kwa pesa yangu kariakoo. Natumia internet ya kuunganisha Zantel elfu kumi ya kujiunga. Lakini Lumumba sijawahi kuingia na wala sitakubali kupokea buku 7 kamawanatoa ili niwatangaze kijinga. Lakini Ocampo four nimesema kura yangu ninayo na nitampa Magufuli lakini mbunge mzuri kama Mnyika bado nitampa ya ubunge
 
Magufuli atashindwa na CCM itashindwa

Kwa kura yangu na statistics zinavyoonyesha bado Magufuli anaweza kushinda.......CCM ikishindwa kwa maana ya kupoteza viti vingi vya ubunge na udiwani wala sitashangaa
 
Kumbuka katiba yako ya sasa ni ya mwaka 1977...kipi kitazuia kuweka kiraka hicho?
Utaweka kiraka saa ngapi maana hao wanaotakiwa kukiweka ndiyo tunaowachagua sasa, na kura yako ndiyo itakayoamua wawe wangapi wa upande upi? Na kutegemea ni wapi watakuwa wengi ndiyo hasa wataamua ikiwa wanapenda kuweka hicho kiraka.
 
Kheri kuchagua mwizi aliyezungukwa na kundi la waadilifu kuliko kuchagua muadilifu aliyezungukwa na kundi la wezi peopleeeeees power.
 
Katiba yetu ingekuwa bora upendo wako ungeifurahisha nafsi yako....
Bahati mbaya Katiba si rafiki.
 
Hapana Abel.....bado nitampigia Magufuli. Lakini nataka kumpigia kura Kubenea jimbo la Ubungo. Nataka ikiwezekana wabunge wa CCM hapa DSM wawe walau watatu (3) tu. Wabunge wchache kama Filikunjombe nitafurahi wakirudi.
Kwa nini usimpigie hata mbunge wa ACT-Wazalendo kama hakuna mgombea wa CUF?

Kubenea ni kati ya watu wanafiki sana katika nchi yetu.

Kubenea ni kati ya wabunge watakaokuwa wananunuliwa ili kutimiza matakwa ya watu wabinafsi.
 
Ndoto yako siyo halisi maana Katiba yetu haituhusu hayo. Kumbuka kwa Katiba na mfumo wa sasa kura unayompigia rais pia inamwongezea mbunge wa viti maalum! Mabadiliko pekee yatakuja kwa kuanzia kubadilisha Katiba - na siyo hii iliyopendekezwa maana bado haina hayo mabadiliko unayoyaota

Kura za Urais haziongezi wabunge wa viti maalum.

Kura za wabunge ndiyo zinaongeza idadi ya wabunge wa viti maalum.

Sheria kuhusu viti maalum inasema hivi,

Viti Maalum vya Wabunge na Madiwani Wanawake.

Uteuzi wa Wabunge Wanawake wa Viti Maalum, umeelekezwa katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, Ibara ya 78, kifungu cha 86A cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343 na Kanuni za Uchaguzi wa Rais na Wabunge za mwaka 2010 chini ya Kanuni ya 67.

Kwa mujibu wa taratibu hizo, kila Chama cha Siasa kilichoshiriki katika Uchaguzi Mkuu ambacho kimepata angalau asilimia 5 ya Kura zote halali za Ubunge zilizopigwa, kitapendekeza kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi majina ya Wanawake kwa kuzingatia uwiano wa Kura ambazo kila Chama kimepata katika Uchaguzi wa Wabunge.

Vile vile kwa mujibu wa Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343 endapo itajitokeza kuwa katika Jimbo la Uchaguzi, Mgombea wa Chama amepita bila kupingwa, idadi ya Kura halali za Urais wa Chama cha Mgombea huyo kama Chama husika kimeweka Mgombea, ndizo zitatumika katika zoezi hilo la kupata uwiano. Endapo itatokea kuwa Chama husika hakikusimamisha Mgombea Urais, asilimia hamsini na moja (51%) ya Kura za watu wote waliojiandikisha Kupiga Kura katika Jimbo hilo zitatumika kwa madhumuni hayo ya kutafuta uwiano.
 
ni sawa na kusema unataka kwenda mbinguni lakin unampenda shetani
 
Haiwezekani UKAWA wakatoa wabunge wengi bungeni na wasitoe rais.

Watanzani hatujafikia hiyo level.
 
Option nzuri ya kulisaida Taifa ni kupigia kura UKAWA. Kwa kuwa tumefika hapa tulipo kwa sababu wabunge wa ccm ambao ndio wengi wanatetea serikali ambayo imeshindwa kuwatumikia wanabchi badala ya kuibana. Huyu JK anayezurura duniani na ambaye ndiye mwenyekiti wa chama ana nguvu ya kumshughulikia mbunge yeyote asiyelinda chama ndio maana mawaziri wanalala hawana wasi.

Kwa hiyo kuchagua Rais na Wabunge wa UKAWA litakuwa ni somo kuwa wananchi hawataki mchezo. Na ni muhimu ccm ipoteze kimojawapo ama vyote yaani Urais na/au idadi ya wabunge wengi. Kwa kuwa hatuna uhakika kipi kitatokea ni vyema kuchagua UKAWA kwenye Urais na Ubunge ili kimojawapo kitokee au vyote. Na ni wazi kuwa na wabunge wengi wa ccm upinzani hiyo serikali haitalala kwani watataka kurudi madarakani na nchi itafaidi.

Tatizo la wanajamvi mnakuwa kama mmechanganyikwa, Dar sio kwamba ndio tz, unaposema watz wameamua unafanya makosa makubwa sana, mnavomwamini Lowasa nyie msidhani pia wote wanaamini hivo, mfano kwa uelewa wangu wa kawaida sana, Lowasa hana ushawishi wowote wa kufanya nimpatie kura yangu, make hana uwezo wa kufafanua sera zake ili nimkubali, amebakia kusema anachukia umasikini, kwa hali hiyo inanifanya niamini kwamba uwezo wake umepungua aidha kutokana na umri au inawezekana afya sio njema sana. Urais ndo hatima yangu pia urais haujaribiwi hata kidogo, vijana waliowengi wanataka kujaribu urais, miaka mitano ni mingi sana sana.
 
Hapana Abel.....bado nitampigia Magufuli. Lakini nataka kumpigia kura Kubenea jimbo la Ubungo. Nataka ikiwezekana wabunge wa CCM hapa DSM wawe walau watatu (3) tu. Wabunge wchache kama Filikunjombe nitafurahi wakirudi.

mkuu umeongea kitu ambacho nilikuwa nikikifikiria kila uchwao maana najilazimisha kumkubali Lowasa lakini dhamira Yang inanisuta maana nilijenga chuki dhidi Yake name ccm!Hat a Mimi naona bora nimpe kura Yang magufuli then ubunge name udiwan ni kwa upinzani.
 
Kwa nini usimpigie hata mbunge wa ACT-Wazalendo kama hakuna mgombea wa CUF?

Kubenea ni kati ya watu wanafiki sana katika nchi yetu.

Kubenea ni kati ya wabunge watakaokuwa wananunuliwa ili kutimiza matakwa ya watu wabinafsi.

umenena mkuu Ryan kama ningelikuwa mpiga kura wa jumbo LA ubungo kura Yang isingeenda kwA Kubenea wala kwa masaburi.
 
Umesema kweli, uchaguzi huu ni mgumu ila kitakachotuokoa sisi wanchi ni coalition government kwa either yeyote atakayeshinda urais
 
Acha uhuni wewe, Naona Lumumba mnaleta staili mpya ya kupata kura za Magufuli. Naona ile ya Chagua Magufuli na si CCM imebuma, Haaa haaaa haaaa.

endelea kuamini kuwa mimi Lumumba.....ukitaka fuatilia comments zangu kabla ujio wa lowassa
 
Mleta mada ulichoongea kinamashiko kabisa, kiukweli Dr Magufuli anaweza akaifanyia makubwa nchi ya Tanzania kuliko Lowasa. Ni kweli watu tumeichoka CCM lakini vilevile CHADEMA sio suluhisho. Watu wengi tunalalamikia tatizo ni mfumo lakini tumesahau kuwa mfumo hutengenezwa na watu. Mtu mmoja kwenye mfumo especially anayeuongoza mfumo anaweza akaubadilisha mfumo ukawa na tija. Mi napingana na wengi....it is not about mfumo but it about a personal who lead that mfumo.

Mfano mkubwa ukimwangalia Rais Buhari wa Nigeria alikuwa chama cha upinzani cha APC, lakini Buhari anajulikana yeye si mtu wa rushwa wakati huo huo amezungukwa na wala rushwa wengi kwenye chama cha APC kama vile Senator Tinubu, Sariki na wengine wengi. Kimfumo ndani ya APC huwezi ukasema ni msafi lakini kiongozi ana maono ya usafi.

Mpaka sasa Raisi Buhari kama yeye na si kama mfumo ameonyesha kumudu kwa kukamata wala rushwa, kuziba mianya ya rushwa katika nyanja nyingi za serikali. Yote haya ameyafanya bila kusaidiwa na mfumo maana mpaka hii leo bado hajaanza kufanya kazi na baraza la mawaziri.

Mi nina hakika watanzania tusipomchagua Dr Magufuli kwa kisingizio cha mfumo na hakika tunaenda KUPISHANA NA MABADILIKO
 
Kura za Urais haziongezi wabunge wa viti maalum.

Kura za wabunge ndiyo zinaongeza idadi ya wabunge wa viti maalum.

Sheria kuhusu viti maalum inasema hivi,
Sheria ya Uchaguzi haina maelezo hayo! Unaweza kuniwekea umeyapata wapi. hata hivvyo bado kwa vyama vingi kura za Rais ndiyo determinant za idadi ya viti maalumu
 
Sheria ya Uchaguzi haina maelezo hayo! Unaweza kuniwekea umeyapata wapi. hata hivvyo bado kwa vyama vingi kura za Rais ndiyo determinant za idadi ya viti maalumu
Kama unasema sheria ya uchaguzi haina maelezo hayo, ingekuwa ni vizuri ukayakataa maelezo kwa kuleta maelezo yanayokinzana.

Hiyo ndiyo sheria ya kupata wabunge wa Viti Maalum.
 
Back
Top Bottom