Ninaomba ushauri kutoka Idara ya Wanyamapori

Ninaomba ushauri kutoka Idara ya Wanyamapori

Koryo2

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2016
Posts
2,056
Reaction score
2,523
Nianze kwa kutamka kuwa mimi ni mfugaji. Ninataka nipate ndama dume ya nyati ambaye ana umri wa wiki moja ili nimlete kwenye kundi langu la ng'ombe ili aweze kukua na kunyonya maziwa ya ng'ombe wangu mpaka awe na mri mkubwa wa kuweza kujilisha kwa majani.

Nia yangu kubwa ni kuja kupata dume la mbegu ili nije nipate ng'ombe wakubwa (chotara) wenye uzito mkubwa unaoanzia kilo 1500 na kuendelea. Itabidi nimtoe mapembe ili asilete madhara. Kumleta ndama dume kwenye kundi la ng'ombe wangu atazoea na ile fikra ya porini itakuwa imepotea. Sasa swali langu kwa Idara ya Wanyama Pori,

Je, utaratibu huu unawezekana?.
 
Kuna hizi taasisi za mifugo zinaitwa LITI kama sikosei Ndio hufanya uboreshaji wa mbegu. Tuliwahi kufuga mnyama wa namna hiyo lakini nadhani kuna utaratibu wa kitaalamu zaidi. Ila mbegu chotara nyati/ng'ombe ipo, na wanamatokeo mazuri kwenye ng'ombe wa nyama.
LITI MPWAPWA ndio waliosimamia hiyo project

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna hizi taasisi za mifugo zinaitwa LITI kama sikosei Ndio hufanya uboreshaji wa mbegu. Tuliwahi kufuga mnyama wa namna hiyo lakini nadhani kuna utaratibu wa kitaalamu zaidi. Ila mbegu chotara nyati/ng'ombe ipo, na wanamatokeo mazuri kwenye ng'ombe wa nyama.
LITI MPWAPWA ndio waliosimamia hiyo project

Sent using Jamii Forums mobile app
Kiboko/Kitimoto je?
 
Kuna hizi taasisi za mifugo zinaitwa LITI kama sikosei Ndio hufanya uboreshaji wa mbegu. Tuliwahi kufuga mnyama wa namna hiyo lakini nadhani kuna utaratibu wa kitaalamu zaidi. Ila mbegu chotara nyati/ng'ombe ipo, na wanamatokeo mazuri kwenye ng'ombe wa nyama.
LITI MPWAPWA ndio waliosimamia hiyo project

Sent using Jamii Forums mobile app
Kweli hao jamaa wa LITI wanajishugulisha na uboreshaji wa mbegu bora za wanyama.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna hizi taasisi za mifugo zinaitwa LITI kama sikosei Ndio hufanya uboreshaji wa mbegu. Tuliwahi kufuga mnyama wa namna hiyo lakini nadhani kuna utaratibu wa kitaalamu zaidi. Ila mbegu chotara nyati/ng'ombe ipo, na wanamatokeo mazuri kwenye ng'ombe wa nyama.
LITI MPWAPWA ndio waliosimamia hiyo project

Sent using Jamii Forums mobile app


Loo, hivi inawezekana Nyati, Cape Buffalo akazaa na ng'ombe ???
 
Ukisema species hizi ziko karibu mno maana yake hawawezi kuzaa, ni lazima wawe exactly the same specie ndipo watazaa. Mfano Liger ni cross breed ya Lion na Tigress, they are the same specie.
Kuna namna mbili.
1. Two closely related species can INTERBREED and produce an infertile offspring. Mfano American bison and domesticated cattle.
Hii wanaishafanya sana America kuzalisha hayo Madude makubwa kwa ajili ya nyama kibiashara.

2. Two closely related species can INTERBREED and produce a fertile offspring. Mfano African cape buffalo + domesticated cattle.
Hii study familia yangu ilishiriki, yaani ng'ombe wetu alipandikizwa mbegu za mbogo na alizaliwa mbogo Dume mkubwa sana chotara safi. Alikua mkorofi kidogo lakini watoto wake huyu ( chotara × ng'ombe wa kawaida ) walikua wapole zaidi.
Na hawa chotara wapo mpaka Leo mbegu ilisambaaa sana maeneo yetu pale.

Ng'ombe na mbogo ni familia moja, yaani mbogo ndo ancestor wa ng'ombe. Ni vile ng'ombe walikua domesticated zamani sana.
Tuendelee kujifunza na eneo is hili bado lina nafasi nyingi kufanya tafiti hata iwekezaji kibiashara.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
2. Two closely related species can INTERBREED and produce a fertile offspring. Mfano African cape buffalo + domesticated cattle.
Hii study familia yangu ilishiriki, yaani ng'ombe wetu alipandikizwa mbegu za mbogo na alizaliwa mbogo Dume mkubwa sana chotara safi. Alikua mkorofi kidogo lakini watoto wake huyu ( chotara × ng'ombe wa kawaida ) walikua wapole zaidi.
Na hawa chotara wapo mpaka Leo mbegu ilisambaaa sana maeneo yetu pale.



Yaani wewe umenifanya hadi nimemuuliza profesa wa SUA kuhusu Domestic cattle kuzaa na cape buffalo; ambapo amesema HAIWEZEKANI KABISA, amesema chromosomes pair hazifanani na hata Genus ni tofauti, amesema Genus ya ng'ombe ni Bos na ile ya nyati (cape buffalo) ni syncerus.

Huyo niliyemuuliza ni profesa wa animal science kutoka SUA, nimeongea naye kwa simu 10 minutes ago.
 
Yaani wewe umenifanya hadi nimemuuliza profesa wa SUA kuhusu Domestic cattle kuzaa na cape buffalo; ambapo amesema HAIWEZEKANI KABISA, amesema chromosomes pair hazifanani na hata Genus ni tofauti, amesema Genus ya ng'ombe ni Bos na ile ya nyati (cape buffalo) ni syncerus.

Huyo niliyemuuliza ni profesa wa animal science kutoka SUA, nimeongea naye kwa simu 10 minutes ago.
Nilisema inabidi tufuatilie kuna gaps nyingi. Ila hao ng'ombe chotara wa mbogo wapo, sijahadisiwa nimeshiriki kuwatunza na nyama Yao nilikula.
Nahisi matokeo ya tafiti hizi hayawekwi public au donors wanaondoka nayo sijajua.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilisema inabidi tufuatilie kuna gaps nyingi. Ila hao ng'ombe chotara wa mbogo wapo, sijahadisiwa nimeshiriki kuwatunza na nyama Yao nilikula.
Nahisi matokeo ya tafiti hizi hayawekwi public au donors wanaondoka nayo sijajua.

Sent using Jamii Forums mobile app


Nasema, na narudia kusema kwamba nyati (cape buffalo) na hata nyati- maji (water buffalo) kamwe hawawezi kuzaa (impossble cross breeding) na domestic cattle., kama ingalikuwa inawezekana basi tayari jambo hilo lingekuwa publiced zamani sana kama ilivyokuwa publicised kuzaa kati ya Simba na Tiger, kati ya punda na Farasi na kati ya Chui na Jaguar.

Huko Kenya kuna mtu kafuga nyati pamoja na ng'ombe, alimchukua bado akiwa mdogo, wanaishi zizi moja na ng'ombe, huyo bwana anasema kazi kubwa ya huyo nyati ni kama mlinzi wa wa hao ng'ombe inapofika usiku, yaani yeye huwa very vigilant kwenye hatari ukilinganisha na ng'ombe, ni mwepesi kugundua hatari, ya watu au wanyama wakali wanapokaribia zizi usiku, anasema hana kazi nyingine yoyote ya muhimu kwa huyo bwana isipokuwa ni hiyo tu.

Huyo prof, aliniambia ng'ombe kutozaa na nyati ni sawa na Sokwe kutozaa na Binadamu au nyani kutozaa na tumbili.
 
Back
Top Bottom