Ninakwenda mafunzo ya JKT...

Status
Not open for further replies.
Nipo njiani naja,tutakuwa pamoja huko kupiga kwata
napinga mtanzania yeyote kwenda jkt na much more kwa mbunge! kwa mazingira ya tanzania na ya dunia ya sasa kupeleka watu jkt ni kuchanganyikiwa,ufisadi na zaidi ni kale ka mchezo ka mbuni kuficha kichwa mchangani ukijidai umejificha.tatizo tunalijua wote na sio watu kutokwenda jkt! lakini kwa sababu tumeamua tena kujidanganya kama kawaida yetu basi yatakayotupata na yatupate maana tumejipangia wenyewe kwa ujinga na uoga wetu wa kupinga mambo ya kijingajinga.
 

Yaani wewe navokujua mpaka mafunzo yaishe basi ushashindilia mimba maafande 8 na makuruta wenzio 23
 
Nawatakia ujenzi mwema wa taifa kwa kutumia ubao huu/tuition hii ya bure itoayo elimu ya maisha ie JF.
Likes Received 47
Likes Given 0

Naona pamoja na unafiki wa kuisifia JF, hujawahi kutoa 'Like' hata moja, kama vile michango ya wengine wee hujaona la maana.
Bila shaka JKT watakufundisha kukubali mawazo ya wengine.
 

Nakuombea urudi angalau ukiwa na chembechembe walau ndogo sana za uzalendo kwa nchi yako.
 
Akili za huyu jamaa bwana anadhani uzalendo unajifunzwa .No unazaliwa nao naye tayari si mzalendo hata akitoka huko hatakuwa na lolote maana akili zako ziko kwenye Chama kushika utamu .Poa sana Mkuu nenda huenda ukarudi na heshima na matusi yawe yameisha .
 
Wiki tatu, hayo ni mafunzo au warsha.......!mnalipwa au bure>?]

sikuwa namjua mchemba, lakin kumtukana sio poa, bali kama nyuz nilizosoma nikapata meseji ya tabia yake mh. mchemba. Atakuwa anaenda ajifunze kushka silaha na kulenga shabaha. Inaonesha mchemb ana element za Rage
 
mbona kwenye kutoa matusi hutuagi? We nenda tu sina desturi ya kumtakia kheri msaliti kama wewe
 
hv wewe unavyoaga kuwa waenda huko ili iwe nini?mbona una akili za kitoto sana,unapewaje cheo kikubwa hcho halafu unakuwa na vi2 vya visivyo na msingi?nenda huko pengne akili itapanuka uache matusi jukwaani,ila kabidhi jimbo kwanza,
 

hongera, ni imani yangu kubwa utabadilika na kuwa na mtazamo wa kizalendo badala ya ushabiki wa iyena iyena na kuwatukana wazalendo wa ukweli.
 
Wadau, nina swali kidogo.
Hivi wabunge walioishia FORM SIX nao wanaenda JKT au batch hii ni ya wale wenye degree tu?

Juliana Mwampamba na Mtela shonza waulize watakujibu vizuri sana weee kada mkuu....
 
Minafkiri waheshimiwa mnakwenda kama seminatu nakuongeza CV flani hivi yakupandia majukwaani. Naamini hamtofanya mafunzo halisi, mambo mengi sana hayato fanywa mkiwepo kwa nafasi zenu kisiasa, kimsingi uheshimiwa wenu utawakosesha mambomengi yamsingi sana yanayo mtofautisha, mtu aliyepita mafunzo ya kijeshi na ambaye hakupita kwamfano, kutolewa uraia ndani ya wiki 6 zakukesha bila kulala mkimwagiwa maji nawakati mwingine kuchapwa viboko na mikanda ya jeshi mkiimba usiku kucha huku mkifanya kazi za ovyo ovyo na bila kuoga kufua wala kuvua combat wala buti wala soksi, namengine mengi ambayo siwezi andika yote hapa. Amini nawaambia hakuna muheshimiwa anaeweza vumilia walao kwasiku tatu kwamafunzo halisi ya JKT.
 
Hii JKT ni mpango tu wa kufanya vijana wawe na uoga wa kuunga mkono upinzani kwa mwavuli wa
kinachoitwa Uzalendo,hakuna nia nyi
ngine zaidi ya hiyo.
Wenyewe mmekaa mmpanga mmeona mtumie njia hiyo kudhoofi
sha mapenzi ya vijana kwa upinzani!

Serikali hii ya CCM haiwezi kuingia gharama kubwa kama hiyo kwa nia
eti ya kufanya watu wawe Wazalendo na Wakakamavu,sio kweli,Ukweli ni kwamba hii yote ni Siasa tu ni janja ya nyani.
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…