Habari za wakati huu.
Ninaandika hapa nikiwa na msongamano wa mawazo mengi, huyu mwanamke ambaye ni mpenzi amekuwa akinipasua kichwa sana, ni mwepesi wa kubadili maamuzi bila kufikiria kuwa ni kiasi gani inaweza kutugharimu.
Ana ujauzito wangu ila kila tutakapokwaruzana anakimbilia kusema atalea mwenyewe hahitaji msaada wangu wala hanitegemei sana, nikitaka nijitoe tu, sasa nabaki na maswali, mwanangu nahitaji tumlee pamoja wazazi wake wawili, ikiwa nina mpango wa kumuoa nije kuishi naye, ila najiuliza sana kama tutafika mwisho wa safari, ili yeye aendelee kuwa na mimi inanilazimu nimnyenyekee sana, hebu nishaurini wakuu nifanyaje maana nahisi kuchanganyikiwa.
UPDATE; Comment number 5 nimeweka screenshot ya maongezi.
Sent using
Jamii Forums mobile app