Nina milioni mbili nataka nimfungulie biashara mke wangu,je itatosha?

MENISON

JF-Expert Member
Apr 26, 2013
726
622
Nipo Dar nafanya kazi nimeajiriwa ,kwa sasa nina mil 2 nahitaji msaada wa biashara ya kufanya na mke wangu kwa kuanzia.Naishi maeneo ya kimara baruti na mke wangu anakaa tu home ,yeye anataka nimfungulie biashara lakini mtaji ninao mdogo,Naombeni ushauri
 
Nipo Dar nafanya kazi nimeajiriwa ,kwa sasa nina mil 2 nahitaji msaada wa biashara ya kufanya na mke wangu kwa kuanzia.Naishi maeneo ya kimara baruti na mke wangu anakaa tu home ,yeye anataka nimfungulie biashara lakini mtaji ninao mdogo,Naombeni ushauri

Aanze kupika maandazi au chapati halafu awe anazitembeza maofisini.
Kama ana haiba yenye mvuto biashara yenu itastawi vizuri tu na soon ataanza kupiga trip za Guangzhou!!
 
Mmeshafikiria ni biashara gani mnataka kufanya kama mke na mume? Mtaji huo ni kianzio kizuri kabisa.
Nilifikiria nichukue fremu ndogo ya 70 hapa mtaani kwetu naona kwa miezi sita si ndio hela yenyewe inaisha.
Unaweza kutushauri mkuu tupo uswahilini
 
  • Thanks
Reactions: BAK
genge lina lipa sana...
tigo pesa, m pesa pesa....
biasha ya khanga na vitenge...
duka...
viatu vya wadada...
saluni ya kike....
zote ni biasha nzuri inategemea na maamuzi yenu!!
 
Inatosha sana kwa mwanamke. Wadau wa kukuza mitaji ya wake za watu tupo wengi sana hapa Dar.
 
Uliza Mkuu gharama ya hiyo frame kwa nusu mwaka ni kiasi gani kwa wale wafanyabiashara walizonazo kasha uangalie na mtaji uliokuwa nao na biashara mtakayoamua kuifanya. Kuna biashara nyingine zinalipa sana katika baadhi ya maeneo.

Nilifikiria nichukue fremu ndogo ya 70 hapa mtaani kwetu naona kwa miezi sita si ndio hela yenyewe inaisha.
Unaweza kutushauri mkuu tupo uswahilini
 
Nipo Dar nafanya kazi nimeajiriwa ,kwa sasa nina mil 2 nahitaji msaada wa biashara ya kufanya na mke wangu kwa kuanzia.Naishi maeneo ya kimara baruti na mke wangu anakaa tu home ,yeye anataka nimfungulie biashara lakini mtaji ninao mdogo,Naombeni ushauri

Sijui bwana nisamehe siingilii ya kwako, lkn mi wangu nilimfungulia kwa mtaji almost na huo yaani 2.5m vitenge vya Kg wax lkn alianza nyodo kujiona anazo sana jeuri kwangu baadaye mtaji ukakata jeuri ikaisha sasa tunapendana kweli, hivyo tu nakupa tahadhari usije ukawa unafungulia frustration jiandae kwa lo lote!
 
Mh kama unaweza mwache hivyo hivyo!! Hawa watu wengi wao ni wa ajabu sana. Ila kama umepata bahati ya kupata mwenza wa kweli ndio mtaweza kusaidiana kwenye maendeleo. Ila mkuu, kuwa mwangalifu sana. Biashara ya kufanyia nyumbani nafikiri ndio nzuri zaidi kuliko ya kuzunguka nje.

Ngoja nifikirie nikipata idea nzuri nitaileta hapa.
 
Aanze kupika maandazi au chapati halafu awe anazitembeza maofisini.
Kama ana haiba yenye mvuto biashara yenu itastawi vizuri tu na soon ataanza kupiga trip za Guangzhou!!

Loh pole
Mambo hongkong
 
Nipo Dar nafanya kazi nimeajiriwa ,kwa sasa nina mil 2 nahitaji msaada wa biashara ya kufanya na mke wangu kwa kuanzia.Naishi maeneo ya kimara baruti na mke wangu anakaa tu home ,yeye anataka nimfungulie biashara lakini mtaji ninao mdogo,Naombeni ushauri
Wengi wamekushauri vizuri,issue za wanawake na biashara za kuzunguruka ni tatizo sana.
Kwanza ili utake kufanikiwa kwa hilo jaribu kumsikiliza na kumpa nafasi yeye ndie awe mwenye wazo kuu,ila kama wewe ndio utajifanya unawazo kuu basi itakufa muda sio mrefu.Chukua kama mawazi matatu ya kwake kisha lete humu uchambuliwe.
Unaweza kuwa na wazo la Duka la mtaani,yeye akawa na wazo jingine.
Ila kwa mtaji huo ni mkubwa sana.
Kuwa makini na wala usimtishe nakumkaripia,hapo atakuwa anafanya biashara kwa hofu na wala hamtofanikiwa.
Muwe tayari kwa changamoto za aina yoyote hapo ndio ukomavu wa akili unakuja.Unaweza kukuta mtajo wote unakufa,sasa ukifa unaweza kukuta ndoa inatetereka kama hampo makini,kwa mwenye Hekma na ndoto huo ni muda wa kukaa na kutathmini kwanini mtaji umekata namna hii,huo ndio utakuwa mwanzo wa kuzi face changamoto.Na akili usi iset ikaamini kwamba hiyo pesa au huo mtaji ndio maisha yako,Keep it kwenye biashara kisha relax usubiri changamoto.
 
Wengi wamekushauri vizuri,issue za wanawake na biashara za kuzunguruka ni tatizo sana.
Kwanza ili utake kufanikiwa kwa hilo jaribu kumsikiliza na kumpa nafasi yeye ndie awe mwenye wazo kuu,ila kama wewe ndio utajifanya unawazo kuu basi itakufa muda sio mrefu.Chukua kama mawazi matatu ya kwake kisha lete humu uchambuliwe.
Unaweza kuwa na wazo la Duka la mtaani,yeye akawa na wazo jingine.
Ila kwa mtaji huo ni mkubwa sana.
Kuwa makini na wala usimtishe nakumkaripia,hapo atakuwa anafanya biashara kwa hofu na wala hamtofanikiwa.
Muwe tayari kwa changamoto za aina yoyote hapo ndio ukomavu wa akili unakuja.Unaweza kukuta mtajo wote unakufa,sasa ukifa unaweza kukuta ndoa inatetereka kama hampo makini,kwa mwenye Hekma na ndoto huo ni muda wa kukaa na kutathmini kwanini mtaji umekata namna hii,huo ndio utakuwa mwanzo wa kuzi face changamoto.Na akili usi iset ikaamini kwamba hiyo pesa au huo mtaji ndio maisha yako,Keep it kwenye biashara kisha relax usubiri changamoto.
Asante mkuu kwa ushauri wako
 
genge lina lipa sana...
tigo pesa, m pesa pesa....
biasha ya khanga na vitenge...
duka...
viatu vya wadada...
saluni ya kike....
zote ni biasha nzuri inategemea na maamuzi yenu!!

Labda hayo mengine lkn hizo mambo za Tigo n mPESA ss hv pasua kichwa2
 
Sijui bwana nisamehe siingilii ya kwako, lkn mi wangu nilimfungulia kwa mtaji almost na huo yaani 2.5m vitenge vya Kg wax lkn alianza nyodo kujiona anazo sana jeuri kwangu baadaye mtaji ukakata jeuri ikaisha sasa tunapendana kweli, hivyo tu nakupa tahadhari usije ukawa unafungulia frustration jiandae kwa lo lote!

Ndg nimecheka sana Kwahiyo mtaji wa WAX uliiweka NDOA rehani...!!!
 
Mh kama unaweza mwache hivyo hivyo!! Hawa watu wengi wao ni wa ajabu sana. Ila kama umepata bahati ya kupata mwenza wa kweli ndio mtaweza kusaidiana kwenye maendeleo. Ila mkuu, kuwa mwangalifu sana. Biashara ya kufanyia nyumbani nafikiri ndio nzuri zaidi kuliko ya kuzunguka nje.

Ngoja nifikirie nikipata idea nzuri nitaileta hapa.

Inasemekana ili umjue mtu hadi apate Pesa manake mpaka hapa Jamaa bado hajajua Rangi halisi ya YF wake.....!
 
Mimi nadhani ni muhimu km mtaulizana km alivyosema jamaa hapo juu Unaweza kuamua ww kumne mwenzio ana Wazo jingine la manufaa zaidi..! Kwa mtaji wa 2m Angalia km kuna DUKA lolote kubwa la mahitaji muhimu ya nyumbani km hakuna weka hiyo Ila jaribu kulifanya liwe tifauti na mengine yaliyo karibu nawe..! Au nguo za watoto na Wanawake ila km ni Biashara ya Nguo inatakiwa awe SHARP ila ni muhimu umckilize nayy akupe Wazo lake...!
 
Back
Top Bottom