Nina mashaka na wanaoitwa wanyonge

Nina mashaka na wanaoitwa wanyonge

Habari wanajamvi !

Awali ya yote poleni kwa msiba! Niende moja kwa moja kwenye mada. Wanyonge wana shida tena kubwa sana. Twendeni pamoja taratibu mtajua shida ilipo. Siku moja nikiwa mahali fulani nikasikia mnyonge mmoja anasema ' afadhali sasa tumeanza kuheshimiana.' Kwake yeye kitendo cha watumishi wa umma kutokuongezewa mishahara kwa kipindi cha miaka mitano, yeye alifarijika sana.

Wanyonge wapo wengi sana! Karibu wote hufurahia madhira wayapatao watumishi wa umma au wafanyabiashara waliofanikiwa. Nikamsikia mnyonge mmoja anafurahia kuona wahitimu wa vyuo vikuu wakiishia kuchoma mahindi au kuosha magari baada ya kukosa ajira serikalini au taasisi binafsi.Kwao wao wote tukiwa masikini ndio faraja yao.

Nilikuwepo siku wakazi Wa Ubungo mpaka Mbezi huko wakibomolewa nyumba zao bila fidia yoyote , nikamsikia mnyonge mmoja anasema ' huyo ndio Magu bwana , hana huruma na mafisadi bwana' . Kwake yeye kila mwenye nyumba nzuri ni fisadi.

Wanyonge mahali fulani ni wajinga! Ndio maana wanatumiwa na wanasiasa kama stepping stone. Wanatumika na manabii wa uongo kujitajirisha. Wana fikiria wanaweza kuwa matajiri kwa kuombewa...! Bila kufanya kazi.

Juzi nimeona wanao lia na kuzimia wengi ni hao masikini wavaa kandambili. Sijaona hata waziri mmoja akizimia.

SASA JIULIZE KATI YA WAZIRI NA HAWA WANYONGE NANI ALIMFAHAMU KWA KARIBU RAIS MAGUFULI? wanyonge badilikeni!!
Huyu wanaemlilia alitoka katika familia za aina yao. Akapanda hadi kuwa kiongozi wa nchi kwa bahati mbaya. Matokeo yake tumeyaona!
 
Usifurahie kuitwa Mnyonge aiseeee,Kutokomeza Ujambazi yes,well done,ila kuwaruhusu Machinga wajiachie bila mipaka kuna sehemu tumefeli.Wanaharibu sana mandhari na miundombinu jumlisha uchafu.
Mwisho Wanyonge waaache roho mbaya.Wanyonge wana wivu sana
Wana wivu hatari! Mtu hajasoma anamuonea wivu aliye soma ! Kuna siku alifukuzwa kazi mkuu Wa TAKUKURU Mtwara pale Masasi , walishangilia utadhani timu ya Taifa imeshinda Gold medal! Kumbe yule kiongozi hakuwepo kwasababu alikuwa na msiba alifiwa na mtoto wake kabisa! Memo alipo ambiwa akaishia kumrudisha kazini lakini alimhamisha kituo.
 
Tokea 2015 graduates tunabangaiza mtaani. Tunaambiwa tujiajiri, lakini wao wameajiriwa na hawataki hata kustaafu. Na waliopo kwenye ajira hawapandishwi ili wapya waingie kwenye system na waliofanikiwa kujiajiri biashara zimekua ngumu sababu mtaani hakuna pesa. RIP
Na akifika mbinguni afe tena.
 
Siku zote mwenye shida ndio huumia mtetezi wake anapoaga dunia.

Umeandika sana pumba hapa. Kumbuka tu Machinga, Mama ntilie na Bodaboda jinsi walivyokuwa wanajitanua kwenye hii nchi yao tangu JPM aingie madarakani.

Kumbuka watu walivyo kuwa wana furahia usalama wa nchi yao. Mabasi kutembea usiku na mchana.

Pengine wewe pia ni mnyonge ila hujijui, siku ukijijua utaona namna JPM alivyo kugusa pengine kwenye miradi mbalimbali.

Rest easy our Hero.

Mabasi kutembeaw usiku?
 
Ngoja msiba uishe.Mkituletea ujinga wa awamu ya nne kwa mgongo wa nyuma wanyonge tulishazoea haki tutamuenzi Baba kwa kuvunja ukuta wa ikulu.
 
Hapa nakupa tano mkuu.Jiwe anajifanya raisi wa wanyonge wakati yeye hana unyonge wowote.Ni kipindi cha kuanza kuibua waziwazi upigaji wa Jiwe .Mimi naanza na zile Trilioni 1.5 zilizoibuliwa na Profesa Assad ambazo hazina maelezo mpaka leo!
Uzuri JF hamkopeshi.Makaburi yanafukuliwa:
 
Hujui? Kamuulize DPP ! Ile mijihela aliyo kuwa anapokea bila risiti ilikuwa inaenda wapi?
Hizi ni porojo/hisia.

Kuna tofauti kati ya kumiliki mali(tajiri) na kufuja/kutapanya mali.
Kwa kigezo chako, Magu alifuja mali za uma.
 
Haonwa
Siku zote mwenye shida ndio huumia mtetezi wake anapoaga dunia.

Umeandika sana pumba hapa. Kumbuka tu Machinga, Mama ntilie na Bodaboda jinsi walivyokuwa wanajitanua kwenye hii nchi yao tangu JPM aingie madarakani.

Kumbuka watu walivyo kuwa wana furahia usalama wa nchi yao. Mabasi kutembea usiku na mchana.

Pengine wewe pia ni mnyonge ila hujijui, siku ukijijua utaona namna JPM alivyo kugusa pengine kwenye miradi mbalimbali.

Rest easy our Hero.
hao hao wamachinga walijikweza na kuanza kupanga bidhaa mbele ya biqshara za watu ambao walikuwa wanalipa kodi kubwa TRA,haimek sense mm nalipia mapato afu mtu analipa elfu 20 aje kupanga bidhaa zake mbele ya biashara yangu
 
Aisee hawa jamaa ni wabishi kupita maelezo, ni wajuaji na kumbe hawajui kitu.
Kuwasaidia sio jambo dogo kama unavyosema
Umeongea reality mkuu...hakuna njia unaweza tumia kuwaelekeza hawa watu,kwanza propaganda zimewaingia kisawasawa....kila mtu apambane na hali yake.
 
Tafsiri neno 'Mnyonge' ni pana sana la hakika watu wengi hatujuwi maana halisi. Kibaya zaidi tunafurahia kuitwa wanyonge. Mkuu aliweza sana kubadilisha mindset zetu na wote kuendelea kupenda umakini na unyonge.

Mganga wa JPM alikuwa mkali sana aliweza kuogopwa na kila mtu hata mtoto aliyopo tumboni. Ningepata bahati ya kukutana na JPM ningemuomba anipe connection ya Mganga wake maana ni hatari sana.
 
Tafsiri neno 'Mnyonge' ni pana sana la hakika watu wengi hatujuwi maana halisi. Kibaya zaidi tunafurahia kuitwa wanyonge. Mkuu aliweza sana kubadilisha mindset zetu na wote kuendelea kupenda umakini na unyonge.

Mganga wa JPM alikuwa mkali sana aliweza kuogopwa na kila mtu hata mtoto aliyopo tumboni. Ningepata bahati ya kukutana na JPM ningemuomba anipe connection ya Mganga wake maana ni hatari sana.
Unafikiri alikuwa na mganga ? Watanzania sisi naturally ni waoga sana. Unafikiri tungeamua kuandamana maelfu kwa maelfu ange tuweza? Polisi wangetushindwa na hatimae tungemkamata kama panya. Mungu ametuonea huruma amefanya yake.
 
Tate Mkuu
ilifikia kipindi baadhi ya hao wanyonge wanauliza kuwa je mshahara wa mwezi huu watumishi watapata!?
ikabidi nikauliza,kwanini unauliza hvyo?
akanijibu,kwani huoni kama magufuli amekufa!
nikauliza kwani kifo cha magufuli na mshahara vinahusiana nini?
akakosa jibu!
ikabidi nimjibu kuwa kifo cha magufuli akiathiri mshahara!
tena hata yeye mwenyewe marehemu wa mwezi huu atauvuta swafi!
tena zile hela siyo zake,ni zetu wote!
akabaki kubung'aa tu!
Wanyonge ni watu wapumbavu sana, mimi ni masikini ndiyo na najitahidi niukimbie umasikini ila ukiniita mnyonge nitakutusi.
 
Wanyonge ni watu Masikini.
Na umasikini wao wengi wa kupenda au wrong choices.
Wanyonge hao hao wanatumiwa na elites kunyonya na kufurahia madhila ya watu wengine kwa manufaa ya wachache..

Wanyonge ni tool ya kuendelea kutawala.. ukiwasikiliza ukawafanyia yanayokonga nyoyo zao.. watakupa kura.

Wanyonge ni wezi, wazurumaji, matapeli.. na wamejaa kila mahala.. imagine unauza Mikanda kwenye duka unalolipa kodi, na unaleseni ya biashara.. anakuja mtu na mbao za kuokota anagonga gonga mbele ya duka lako anaanza kuuza Mikanda bila kodi ya pango wala EFD mashine.. yeye ana kitambulisho cha mmachinga.. mnyonge huyo.

Biashara zinakufa, wenye majengo ya kukodisha wanakosa wateja, wenye maduka wanalalamika.. ila mnyonge yeye kwake.burdani kabisa...

Unatoa fedha unalipa fidia unanunua shamba.. unapima unamilikishwa... Wanakuja wanyonge wanataka uwapishe kisa wewe wanaona huna kazi nalo.. ndio maana liko wazi... Na serikali sikivu inakunyang'anya inawapa.. walijawa kiburi mno sikuwahi kuona kabla..

Wana sense of intittlement ... Hawajali na ni waharibifu sana. Hawajui haya yote wanayoyakimbilia na kuona wamepata ni very short lived.. na hatima yake inadumaza the entire economy.. wanyonge.
 
Habari wanajamvi !

Awali ya yote poleni kwa msiba! Niende moja kwa moja kwenye mada. Wanyonge wana shida tena kubwa sana. Twendeni pamoja taratibu mtajua shida ilipo. Siku moja nikiwa mahali fulani nikasikia mnyonge mmoja anasema ' afadhali sasa tumeanza kuheshimiana.' Kwake yeye kitendo cha watumishi wa umma kutokuongezewa mishahara kwa kipindi cha miaka mitano, yeye alifarijika sana.

Wanyonge wapo wengi sana! Karibu wote hufurahia madhira wayapatao watumishi wa umma au wafanyabiashara waliofanikiwa. Nikamsikia mnyonge mmoja anafurahia kuona wahitimu wa vyuo vikuu wakiishia kuchoma mahindi au kuosha magari baada ya kukosa ajira serikalini au taasisi binafsi.Kwao wao wote tukiwa masikini ndio faraja yao.

Nilikuwepo siku wakazi Wa Ubungo mpaka Mbezi huko wakibomolewa nyumba zao bila fidia yoyote , nikamsikia mnyonge mmoja anasema ' huyo ndio Magu bwana , hana huruma na mafisadi bwana' . Kwake yeye kila mwenye nyumba nzuri ni fisadi.

Wanyonge mahali fulani ni wajinga! Ndio maana wanatumiwa na wanasiasa kama stepping stone. Wanatumika na manabii wa uongo kujitajirisha. Wana fikiria wanaweza kuwa matajiri kwa kuombewa...! Bila kufanya kazi.

Juzi nimeona wanao lia na kuzimia wengi ni hao masikini wavaa kandambili. Sijaona hata waziri mmoja akizimia.

SASA JIULIZE KATI YA WAZIRI NA HAWA WANYONGE NANI ALIMFAHAMU KWA KARIBU RAIS MAGUFULI? wanyonge badilikeni!!
Nikimsikia kiongozi anasema anaongoza wanyonge namuona ni kichwa tupu debe kutika

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Humu inaonekana kuna watu wanaishi Tanzania nyingine ndio maana awazielewi shida za wanyonge.

Hadithi ya ukweli.

Kuna mama mmoja alikuwa akiishi nje ya nchi, akarudi Tanzania 2008. Kakuta viwanja vyake vimeuzwa na wajanja.

Kaenda ardhi kufuatilia anazungushwa kuanzia 2008-2015, vilikuwa viwanja vinne chake na vya watoto wake watatu.

Katika muda huo wakati kesi inaendelea watemi wawili wakajenga utawafanya nini wakati wanawajua watu wizara ya ardhi na mahakama ya ardhi kesi yake inapigwa kalenda.

Magufuli kaingia late 2015 mpaka katikati ya 2016 mama karudishiwa viwanja vyake vyote. Wale waliojenga mahakama inakupa na tingatinga la kwenda kubomoa nyumba. Bahati nzuri mama alikuwa mstaarabu waliojenga walimpa viwanja maeneo mengine na hela kadhaa wakamalizana ivyo.

Hao ndio wanyonge wanaoongelewa na hata wao watakwambia upatikanaji wa hela sio rahisi chini ya Magufuli lakini uwaelezi kitu kwake. Mifano ni mingi sana na ndio watu wanaojiuliza nani atawatetea tena.
 
Back
Top Bottom