JERUSALEMU
JF-Expert Member
- Sep 19, 2012
- 3,106
- 3,523
Habari wanajamvi !
Awali ya yote poleni kwa msiba! Niende moja kwa moja kwenye mada. Wanyonge wana shida tena kubwa sana. Twendeni pamoja taratibu mtajua shida ilipo. Siku moja nikiwa mahali fulani nikasikia mnyonge mmoja anasema ' afadhali sasa tumeanza kuheshimiana.' Kwake yeye kitendo cha watumishi wa umma kutokuongezewa mishahara kwa kipindi cha miaka mitano, yeye alifarijika sana.
Wanyonge wapo wengi sana! Karibu wote hufurahia madhira wayapatao watumishi wa umma au wafanyabiashara waliofanikiwa. Nikamsikia mnyonge mmoja anafurahia kuona wahitimu wa vyuo vikuu wakiishia kuchoma mahindi au kuosha magari baada ya kukosa ajira serikalini au taasisi binafsi.Kwao wao wote tukiwa masikini ndio faraja yao.
Nilikuwepo siku wakazi Wa Ubungo mpaka Mbezi huko wakibomolewa nyumba zao bila fidia yoyote , nikamsikia mnyonge mmoja anasema ' huyo ndio Magu bwana , hana huruma na mafisadi bwana' . Kwake yeye kila mwenye nyumba nzuri ni fisadi.
Wanyonge mahali fulani ni wajinga! Ndio maana wanatumiwa na wanasiasa kama stepping stone. Wanatumika na manabii wa uongo kujitajirisha. Wana fikiria wanaweza kuwa matajiri kwa kuombewa...! Bila kufanya kazi.
Juzi nimeona wanao lia na kuzimia wengi ni hao masikini wavaa kandambili. Sijaona hata waziri mmoja akizimia.
SASA JIULIZE KATI YA WAZIRI NA HAWA WANYONGE NANI ALIMFAHAMU KWA KARIBU RAIS MAGUFULI? wanyonge badilikeni!!
Awali ya yote poleni kwa msiba! Niende moja kwa moja kwenye mada. Wanyonge wana shida tena kubwa sana. Twendeni pamoja taratibu mtajua shida ilipo. Siku moja nikiwa mahali fulani nikasikia mnyonge mmoja anasema ' afadhali sasa tumeanza kuheshimiana.' Kwake yeye kitendo cha watumishi wa umma kutokuongezewa mishahara kwa kipindi cha miaka mitano, yeye alifarijika sana.
Wanyonge wapo wengi sana! Karibu wote hufurahia madhira wayapatao watumishi wa umma au wafanyabiashara waliofanikiwa. Nikamsikia mnyonge mmoja anafurahia kuona wahitimu wa vyuo vikuu wakiishia kuchoma mahindi au kuosha magari baada ya kukosa ajira serikalini au taasisi binafsi.Kwao wao wote tukiwa masikini ndio faraja yao.
Nilikuwepo siku wakazi Wa Ubungo mpaka Mbezi huko wakibomolewa nyumba zao bila fidia yoyote , nikamsikia mnyonge mmoja anasema ' huyo ndio Magu bwana , hana huruma na mafisadi bwana' . Kwake yeye kila mwenye nyumba nzuri ni fisadi.
Wanyonge mahali fulani ni wajinga! Ndio maana wanatumiwa na wanasiasa kama stepping stone. Wanatumika na manabii wa uongo kujitajirisha. Wana fikiria wanaweza kuwa matajiri kwa kuombewa...! Bila kufanya kazi.
Juzi nimeona wanao lia na kuzimia wengi ni hao masikini wavaa kandambili. Sijaona hata waziri mmoja akizimia.
SASA JIULIZE KATI YA WAZIRI NA HAWA WANYONGE NANI ALIMFAHAMU KWA KARIBU RAIS MAGUFULI? wanyonge badilikeni!!