Nina mashaka na wanaoitwa wanyonge

Nina mashaka na wanaoitwa wanyonge

huko Chato amepeleka miradi ya kufa mtu mpaka airport na uwanja wa mpira wakati hata timu ya kijiji hawana. tunataka tuone Wanyonge wakitumia sasa hiyo airport
Ile airport inayojengwa hapo soon wataanza kufugia nguruwe.
 
Watu wenye kipato cha chini ndo tunaweza kuwaita wanyonge, sasa huwezi kudai unawasaidia wanyonge kwa kuwabana wale wenye kipato cha kati, mfano watumishi wa umma, wafanyabiashara na wajasiriamali. Kwa sababu watu wa daraja la kati wakifanikiwa na kufanya matumizi ndo hapo kula ya wanyonge itapatikana, vinginevyo utajikuta unatengeza kundi moja kubwa la watu wanyonge tupu...
 
Wanyonge ni wajinga na kwa bahati mbaya ndio kundi kubwa la Watanzania
Siwalaumu sana kwani hawakujitakia ila walitengenezewa huo unyonge. Mfumo wa elimu kusoma kwa lugha ya kiswahili ktk elimu ya msingi alafu ngoma kubadilika na kuwa kiingereza ktk hatia za mbele ni chanzo kimojawapo cha huu unyonge. Kutokujua kusoma kiingereza ni chanzo cha ujinga
 
Siku zote mwenye shida ndio huumia mtetezi wake anapoaga dunia.

Umeandika sana pumba hapa. Kumbuka tu Machinga, Mama ntilie na Bodaboda jinsi walivyokuwa wanajitanua kwenye hii nchi yao tangu JPM aingie madarakani.

Kumbuka watu walivyo kuwa wana furahia usalama wa nchi yao. Mabasi kutembea usiku na mchana.

Pengine wewe pia ni mnyonge ila hujijui, siku ukijijua utaona namna JPM alivyo kugusa pengine kwenye miradi mbalimbali.

Rest easy our Hero.
Wewee ndo pumba kabisaaa unainyenyekea hela yako hiyo ni lazima Rais ahakikishe usalama wa walipa kodi wake mana ndio wanaomuweka madarakani hayo maswala ni lazima ayatekeleze kwa lazima na sio ombi watanzania tumerogwa na nani?
 
Kila la kheri! Alitutesa sana watumishi wa umma, miaka mitano mshahara ule ule wa 2015! Kuna watu katili sana Duniani.
Sifa kubwa ya 'wanyonge' ni watu wasiojielewa.. wanajua shida ni kiungo mojawapo kwenye mwili. Hawajui nini kinatakiwa au kilitakiwa kufanyika, hawajui kazi ya watawala wao ni nini.

Ndio maana Marekani walitilia shaka uwezo wa 'wanyonge' kuchagua kiongozi wa nchi, wakaamua watu wachache wenye busara(electoral college) ndio wachague Rais!
Hee kumbeee good idea
 
Mimi kiukweli huwa sikubaliani kabisa na hii falsafa ya wanaoitwa Wanyonge.
Ni kundi linalotengenezwa na watawala kwa maslahi ya watawala wenyewe.
Mfano, nchi za Africa,Tanzania ikiwemo,tulijengewa na wakoloni fikra na tukaikubali kwamba ni maskini ambao tunatakiwa kusaidiwa.
Hii iliwarahisishia sana kututawala kwa kutupa vimsaada ambavyo,kwa mawazo yetu finyu,tuliona ni msaada mkubwa sana kwetu na tukawa tunawakweza.Mpaka leo fikra hizo mbaya hazijatoweka miongoni mwetu.
Vivyo hivyo, Wanaoitwa Wanyonge wametengenezwa ili wawe mtaji wa wanasiasa kupata mamlaka.
Wanaoitwa wanyonge wakipewa nafuu fulani,hata kama ni haki yao ya msingi,hufurahi na kuwaona watoaji kama Mungu wao.
Kwa hiyo,namaliza kwa kuwataka wote wanaojiona wako kwenye kundi la wanoitwa wanyonge wajitambue na kujiona kuwa sio wanyonge na kama wanapatiwa nafuu yoyote na watawala wafahamu kuwa hiyo ni haki yao sio hisani.
Au ninasena uongo ndugu zangu?
Ubarikiwe
 
Waendelee kujiita wanyonge wajanja wanakula mema ya nchi
 
Mimi kiukweli huwa sikubaliani kabisa na hii falsafa ya wanaoitwa Wanyonge.
Ni kundi linalotengenezwa na watawala kwa maslahi ya watawala wenyewe.
Mfano, nchi za Africa,Tanzania ikiwemo,tulijengewa na wakoloni fikra na tukaikubali kwamba ni maskini ambao tunatakiwa kusaidiwa.
Hii iliwarahisishia sana kututawala kwa kutupa vimsaada ambavyo,kwa mawazo yetu finyu,tuliona ni msaada mkubwa sana kwetu na tukawa tunawakweza.Mpaka leo fikra hizo mbaya hazijatoweka miongoni mwetu.
Vivyo hivyo, Wanaoitwa Wanyonge wametengenezwa ili wawe mtaji wa wanasiasa kupata mamlaka.
Wanaoitwa wanyonge wakipewa nafuu fulani,hata kama ni haki yao ya msingi,hufurahi na kuwaona watoaji kama Mungu wao.
Kwa hiyo,namaliza kwa kuwataka wote wanaojiona wako kwenye kundi la wanoitwa wanyonge wajitambue na kujiona kuwa sio wanyonge na kama wanapatiwa nafuu yoyote na watawala wafahamu kuwa hiyo ni haki yao sio hisani.
Au ninasena uongo ndugu zangu?
Hapana ndugu umeongea UKWELI MTUPU!
wanyonge ni watu wa ajabu sana, tunawaona, tunaishi nao kwenye jamii zetu.
Huu unyonge ndio uliwapa wazungu wepesi wa kututawala enzi za ukoloni, na kuendelea kutawaliwa na weusi wenzetu hadi leo.
Ili tupige hatua tunapaswa kupambana na huu unyonge, unyonge sio sifa, unyonge ni ujinga na upumbavu!
 
Kongole mkuu, kuna shida mahali, yaani mtu anafurahi kuwa masikini/mnyonge!!
Jiulize baada ya kuwa mnyonge then utafanyiwa nini au utafurahi kusikia tajiri mmoja kafilisiwa au kaporwa pesa zake
 
Sifa kubwa ya 'wanyonge' ni watu wasiojielewa.. wanajua shida ni kiungo mojawapo kwenye mwili. Hawajui nini kinatakiwa au kilitakiwa kufanyika, hawajui kazi ya watawala wao ni nini.

Ndio maana Marekani walitilia shaka uwezo wa 'wanyonge' kuchagua kiongozi wa nchi, wakaamua watu wachache wenye busara(electoral college) ndio wachague Rais!
U hit the bull! Ahsante sana
 
Back
Top Bottom