Naibu Spika wa bunge Job Ndugai amesema ana furaha kubwa kusikia Rais ameshasaini mswada wa sheria uliokuwa unabishaniwa.
Akizungumza jana Ndugai amesema kwanza haelewi kinachobishaniwa kuhusu Mswada huo na bunge liliupitisha baada ya sheria na taratibu zote za kibunge kufuatwa.
Kuhusu kurejeshwa bungeni baada ya majadiliano ya wapinzani na Rais Kikwete Ndugai amesema kwanza wanaopigia debe suala hilo ni lazima wajiulize Je, kanuni zinaruhusu?
Kwanza sina uhakika kama mswada huu huu utarejeshwa ila ninachofurahi umeshasainiwa na Rais...'alisema Ndugai kwa Furaha.'
Source:Tanzania Daima.