Mtetezi.com
JF-Expert Member
- Oct 6, 2016
- 3,134
- 3,601
Mkemee shetani wewe acha kujidanganya mana siku ukiora unaliwa voda sijui utatuambia?
njo nkwambie kitu dadaAiseee,..nimewaza tuu siku ukifa kwenye hiyo ndoto sijui utaoneshwa life after death,.![]()
Yote hayo huwa naota. Naoga, naongea, nacheza, naogelea, nafanya mikutano, naenda supermarket kununua vitu, yote hayo ndotoni. Na nikiamka nakuta kila kitu nilipolala kipo shwari na mke wangu yuko kando yangu kama kawaida.Chunga usije ukaota unakunya, alafu ukiamka ukute kimba kwa bed....
Miushauri wangu ni huo tu.
![]()
![]()
![]()
![]()
Hata ninavyoandika hapa sijui sasa ndio niko kwenye ndoto au maisha halisi.
Hongera sana mkuu, basi weendelea tu kula bata ndotoni kwasababu hakuna madharaYote hayo huwa naota. Naoga, naongea, nacheza, naogelea, nafanya mikutano, naenda supermarket kununua vitu, yote hayo ndotoni. Na nikiamka nakuta kila kitu nilipolala kipo shwari na mke wangu yuko kando yangu kama kawaida.
Asante kwa sahihisho. Sasa sijui tuiiteje, ni double life ya ndotoni. Au ni nini? Lakini ninavyoona watu hawa wawili ni tofauti. Kule ndotoni ni kijana wa 30's wakati hapa nilishakula chumvi miongo mitano!Hata mimi nilielewa hivyo kumbe ni tofauti kabisa na kichwa cha habari 🙂
Sina hiyo kitu. Hata kama sijijui, ningeshasikia hata angalao fununu kwa watu kuwa nina abnormal behaviour fulani. Wagonjwa wa akili wanafahamika hata kwa tabia zao tu, licha ya wale wanaotibiwa hospitalini.Hapa nanusa dalili za mental illness mkuu
Nina wake wawili na two homes. Moja ya real life hii hapa na nyingine ya ndotoni. Na zote naziishi kwa kulala. Nikilala huku naamkia kule, na nikilala kule naamkia huku. Lakini si kwamba huwa silali, no, ninapoamka najisikia fresh kabisa kwamba nimepumzika vya kutosha usingizini na yaliyotokea ni ndoto tu.Haahaaa mi mwenyewe nilidhani ana mke na mchepuko hawajuani kumbe ndotoni
Dah
Elewa tu kuwa ninapokuwa huku ni ndoto ya kule, na nikiwa kule ni ndoto ya huku. Kwahiyo maisha yote ni ndoto.Story ulikuwa umejitahidi kuiandika vizuri, ila hapa ndo umeiharibu.
Mara nyingine uwe unajaribu kuirudia story kwa kuvaa viatu vya hadhira kabla hujaipost.
Sivuti bangi wala sigara. Hata pombe sinywi.Bangi mbaya sana!!
Ngoja niingie google nifananishe. Asante kwa hint.Labda unaishi kwenye "simulation". Wataalam wa artificial intelligence wanatabiri siku zijazo watu wataishi katika virtual reality iliyokuwa simulated kwa kompyuta. Pengine umetangulia...
Popote ninapolala lazima iendelee. Tangu 2010 hadi leo. Nilishalala mahotelini mara nyingi hadi nje ya nchi. Hata nikilala kwa ndugu zangu mikoani ninapowatembelea.
Ni hali ya kweli imenipata tangu mwaka 2010. Leo ni mara ya kwanza naisema. Siamini mambo ya misukule, lakini hii hali kweli siielewi, lakini ni kama naifurahia hivi.
Ilitokea hivi. Mwaka 2010 sikumbuki tarehe, siku moja nililala nikaota ndoto kuwa eti niko kwenye mji fulani tofauti na ninakoishi, nikiwa nasoma chuo masomo ya biashara, business administration. Sijawahi kusoma masomo hayo katika maisha nje ya ndoto. Kesho yake nikaamka, nikaendelea na siku yangu hadi ikaisha. Nilipolala tena ile ndoto ya jana yake ikaendelea, nikapata marafiki darasani, nikawa najishughulisha na michezo nikajifunza kuogelea (sijui kuogelea nje ya ndoto!) na mambo mengi mazuri. Huko katika ndoto, usiku ukaingia nikaenda kulala hostel, nikiwa usingizini nikaota ndoto kuwa nimeamka ambako niliamkia nyumbani kwangu kwenye maisha yangu ya siku zote.
Kufupisha story, nimekuwa kwenye mzunguko wa ndoto za kama za series, yaani nalala nyumbani naota mwendelezo wa ile ndoto na huko ndotoni nikilala naota nimeamkia nyumbani, kwa hiyo mzunguko unaendelea. Hata ninavyoandika hapa sijui sasa ndio niko kwenye ndoto au maisha halisi. Kule kwenye ndoto nyingine maisha yameendelea vizuri, nimemaliza chuo, nafanya kazi kwenye kampuni ya kuuza pikipiki, na nimejenga nyumba eneo fulani la mlimani, na nina mke na mtoto wa miaka 4. Kwenye maisha haya niliyoamkia leo asubuhi ni mtu mzima kuliko yule wa ndotoni, nina mke na watoto wanne wakubwa, wa mwisho yuko form four.
Sina tatizo lolote la kiakili, na wala ninapoamka sijisikii kuchoka popote, nakumbukia tu maisha yangu ya ndotoni na kuyashangaa, basi.
Je, hili ni tatizo? Kuna wengine wenye ndoto za aina hii?