Bado nipo nipo
Member
- Nov 19, 2011
- 69
- 11
- Thread starter
- #21
Kilimanjaro wapi, tema data tukushauri tunaojua hayo mazingira vizuri...
maeneo ya Marangu.
Kilimanjaro wapi, tema data tukushauri tunaojua hayo mazingira vizuri...
Yani hapa ndipo unapoupata na kuuhisi utamu wa JF, watu hawana roho za kupe, wanatoa ushauri/mawazo hadi inaleta amani katika moyo, japo hawakosekani wanaokatisha wenzao tamaa. WanaJF wengi mngekuwa viongozi wa hii nchi, leo tusingekuwa na hali hii mbaya katika nchi yetu. Mbarikiwe wote mliotoa mawazo chanya kwa mwenzetu.
Vipi wadau wa hapa ndani, leo nimekuja kwenu kuomba msaada juu ya hili. Nina baba yangu ambaye mambo yake yamemwendea kombo sana mwaka huu, haswa kwa swala la kifedha. Na ameniambia anataka kuuza nyumba pamoja na kiwanja alicho nacho ambamo ndiko anakoishi na familia yake ili warudi kijiji walipotoka na kufanya biashara na fedha atakayopata. Je hii itasaidia ama ndio muendelezo wa matatizo endapo biashara itazorota?