Hamna kitu hapo unapoteza muda tu. Vijana mwanamke ukiwa nae kama hauna maisha halafu unategemea yeye aje ndipo mtafute pamoja hayo maisha then u are wasting your best years of life and huo uhusiano utakuwa ni sarakasi tu sababu wanawake wa kaliba hiyo sidhani kama wapo miaka hii.
Hizi efforts za kugombana na kubishana na mwanamke ungetia katika kugombana na changamoto za maisha iikiwamo kujifunza mbinu bora za kisasa za kupata pesa na kujenga himaya yako then ungeanza kupiga hatua kwa haraka sana. Sababu hicho unachokitaka kwasasa huko mbeleni utakipata hadi utakinai.
Kwa sasa wewe priority iwe kwanza ni wewe na MUNGU wako katika kujijenga kama mtoto wa kiume. Jenga mahusiano bora na MUNGU akupe nguvu, maono, ujasiri, uwezo, na mbinu za kuweza kubaini na kutumia vipaji alivyokupa katika kujijenga kimaisha na ujitahidi hadi uyaone mafanikio yanaanza kunukia na kukujia.
Na mafanikio yakija then jiwekeze zaidi katika kujiimarisha na kuboresha maisha yako. Uwe na assets zako ambazo zitakupa cash flow nzuri ya uhakika, fanya mazoezi, kula chakula kizuri na kwa wakati,kuwa mtu wa ibada, jenga network nzuri ya ndugu jamaa na marafiki ambao watakuwa msaada maeneo mbali mbali ya maisha yako na familia yako utayotengeneza,kaa mbali na maisha ya kihuni. Tupia ila kwa akili achana na mambo ya kuendekeza hisia za kuganda kama kumbi kumbi sababu huko ndio unapoteza uanaume wako.
Ukishakamilisha haya na yakaonekana then utakuwa tayari kutafuta mwanamke wa kujenga nae familia.
Shida inakuja mara nyingi huwa watoto wa kiume huwa mnahangaikia sana kupata mwanamke as if ni Golden Goose (Bata wa dhahabu) ambae ndio ana siri ya mafanikio yako something which is not true.
Kwa hali ya maisha ya kisasa na mitazamo iliyopo ni ngumu sana kwa mwanamke kuishi na mwanaume katika mazingira ya mwanzo wa maisha bila chochote bila kupitia mifarakano, mizinguo, michubuano, vituko na visa, kupotezeana muda, kufujana nguvu kazi, na kadhalika. Na pengine mnaweza msifike mbali au mkafika mkiwa na uchovu wa kihisia sana na kushindwa kuweza kuwa na upendo unaotakiwa. Ikitokea ukapata ambae hana njaa na tamaa ya maisha ya urahisi then mshike vema na mjijenge pamoja ila kwa dunia ya sasa ni ngumu sana kupata pisi kali halafu iwe na utu ndani yake wa kuvumiliana na kuwa na focus ya maisha. Nasisitiza tena wapo ila ni very rare.
Ila lait kama mtoto wa kiume ukianza kujijenga mapema unakuwa na advantage ya kuanzisha familia kwa utulivu. Na hapa sizungumzii uwe bilionea au milionea bali kuwa na maisha before haujaanza kuhangaika na mahusiano serious kwasababu mabinti wa sasa hawajapitia hizo training za kuunda mifumo ya kujenga maisha. Wasasa wao akili zinaanza kufunction na kutambua kuwa wao ni mke wa mtu pale akikuona upo katika sehemu una maisha yako na hautetereki na mambo ya kidunia.