Ni bora nife maskini kuliko kutegemea chuma ulete kama wewe. Hivi bila aibu umeweka bando kutetea ushirikina? Pumbafuu kabisa.Mimi sio maskini mwenzio.
Unaweza kuendelea kuishi na itikadi zako za kimasikini.
Ila wanakuwaga hawana maendeleo yoyote.Vibubu vinasaidia sana ila kuna code mkuu? Wakati unanunua unasubiria palepele yaani kinatengenezwa upo hapohapo unaondoka nacho, vingi huwa vinawekwa tamaduni..
Ipo hivi, chuma ulete inakuwaje?
Chuma ulete inategemeana na mazingira husika.
Mfano hapa nilipo mimi chuma ulete yao inakuwa hivii
Anakupa 5000 anataka kitu cha 1000, wewe unamrudishia elfu 4000 anachukua ile elfu 4000 anasepa nayo kisha ile elfu 5000 ambayo amekupa ukiichanganya na pesa zingine ile ile 5000 ndio inasepa katika mazingira ya kihabeshi..hapo wewe unakuwa umebukuliwa jumla ya shilingi 4000 na bidhaa umempatia. Yaani anakuchukulia ile 4000 yako na kitu anakuwa kapata bure, huku yeye mwana tamaduni mfukoni mwake akiwa na 9000.
4000 uliyomrudishia chenji ( faida kutoka kwa fala wewe, bidhaa husika ) kisha 5000 yake itarudi kwake katika muda usiojulikana...wanapenda kutumia noti mpya mpya katika hizo jarakati zao za kibazazi.
Watu wenye chuma ulete mara nyingi ni vijana wenzetu, wazee na wanawake.
Kweli kabisa mkuuWatu wengi wanapenda kutoa visingizio kwenye kushindwa kwao.
Chuma ulete ni excuse inayopendwa na watu wazembe walioshindwa kudhibiti mahesabu/matumizi ya pesa... au wafanyakazi wezi wanaoibia mabosi wao kwenye sehemu za biashara walizoaminiwa kuzisimamia!
BigBro tatizo makato na tozoKibubu unatengeneza mwenyewe sio kununua au njia rahisi hifadhi kwenye simu halafu hamishia account yako ya bank every single day, then utajikuta umeweka akiba nyingi sana...
Nitakupiga chuma ulete hadi uje utengue hii kauli wee ngoja tu 🥸🥸Kweli kabisa mkuu
Yamekukuta mkuu?Nitakupiga chuma ulete hadi uje utengue hii kauli wee ngoja tu 🥸🥸
Mie hapana sijawai pigwa chuma ulete ila wapo waliopigwa hii afahamu hata uadilifu wao na wakalizwaYamekukuta mkuu?
Mkuu unaakili sana. Kachukue kitimoto chapHapa nimekaa kwenye sakafu nafikiria na usiku huu plus baridi hili natamani niende nikachukue kitimoto lost ya hii hela yote iliyobaki niondoe mikosi!
Duuh mi siaminMie hapana sijawai pigwa chuma ulete ila wapo waliopigwa hii afahamu hata uadilifu wao na wakalizwa
Hahaha
WAKATI WA KURUDI UKASAHAU NI MLIMA! POLENilitaka kutengeneza mwenyewe, tatizo muda kaka!
Ubize mwingi, na nilipoona hivyo vidude vinauza buku tu nikaona kitonga hii hapa naserereka na buku langu, kumbe ni matatizo!
Ila sio wote huwa wahanga wa chuma ulete, unataka soda gani mkuu uletewe hadi mlangoniDuuh mi siamin
Mbona umekivunja mapema sana? Ungekiacha walau mwaka mmoja ukaona faida yake. Halafu jaribu kuweka elfu tano tano siyo kujaza noti za elfu moja au sarafu, utaona faida yake.Dah, yaani hapa wakuu natamani kucheka wakati ni jambo la hovyo limetokea
Siku ya tarehe 3 mwezi huu, ni juzi tu hapo niliamua kununua kibubu na nikaanza kuweka visenti vyangu ninavyopata kazini, kazini nalipwa kwa kila siku, nikaona hela nayolipwa kwa siku ni nyingi na nikajiapiza kuwa nitakuwa nakula walau robo ya kipato na nyingine nitadumbukiza kwenye kibubu.
Kwakuwa ilikuwa tayari ni usiku na nimeshatumia hela niliyolipwa siku hiyo, nikaamua kukizindua kibubu changu kwa kuweka vijisenti vilivyobaki kwenye matumizi, nikaweka 3,400/=
Tarehe 4. 7,000/=
Tarehe 5. 12,000/=
Tarehe 6. 10,000/=
Tarehe 7 nikaweka chenchi chenchi kama za elfu 3.
Tarehe 8 nikaweka 20,000/=
Sasa kwakuwa huwa nasikia stori nyingi kuhusu vibubu, ikabidi nifanye ziara ya kushtukiza kwenye kibubu changu, nikivunje kibubu nione hesabu zangu kama ziko sawa au vipi.
Haha! Kama mchezo wa kuigiza tu wakuu, yaani Hapa nimekuta 23,000 mpaka siamini nachokiona.
Chenchi zote zipo, kasoro zile noti tu.
Mlaaniwe wauza vibubu