Nimeupenda ustaarabu wa John Pombe Magufuli

Nimeupenda ustaarabu wa John Pombe Magufuli

magufuli ni zero kabisa. sijaona cha maana alichoongea.


SITAWAANGUSHA
 
watu wanajitoa fahamu eti kupotea bilioni 263 wizara ya magufuli ripoti ya cag sio kashfa! mahaba yakizd sana chongo huitwa kengeza.
 
Hicho tu ndio umekiona this year lowasa team lazima mufweee. This guy is our presidaaa. Penda ucpende
 
Hujaona aliyoyafanya ndani ya nchi hii acha ishabiki ukweli utabaki ukweli tuu. Keep it up magufuri the pride of Tanzania
 
Mtalia sana this year in fact mm sinaga chama but for this guy I have to vote for him. Welcome King magufuri to the white house.
 
Anasema atakuwa Rais wa watanzania wote hata wapinzani mbona kauli yake kwenye ufunguzi wa madaraja na barabara huwa anasema Ccm inajenga barabara lakini Chadema, Nccr, Cuf na wengine watapita kwenye barabara hizi hizi.

Rais gani hajui kuwa kodi haibagui vyama, mimi si mdau wa ccm, lakini nakatwa income tax karibu laki moja kila mwezi, nalipa motor vehicle TRA nk, na pesa hiyo hiyo ndiyo inayojenga madaraja na barabara. Magufuli bado sana.
 
mtoa maada umenichesha sana yaan hujapenda maneno yake ila umependa anavyozungumza!!! Sikiliza Watanzania hatutaki sauti nzuri, sauti nzuri peleka kanisani, tunataka nameno mazuri yenye utekelezaji ndani yake sio yale ya BUKOBA NITAWALETEA MELI ALAFU KUWA AHADI YA MANENO.
 
Hivi siku zote tunajaribu kuwaelimisha watu hawaelewi acheni kuwa wapumbavu msiofundishika,tatizo la mfumo uliopo ccm ndio unaoharibu itikadi za watu binafsi mfano mzuri ni wakati watangaza nia wa ccm walipokuwa majukwaani. Wengi wa watangazania walijinadi vizuri sana mpaka mtu unajiuliza hawa kweli wako katika serikali hii? Mawazo yao ukiyapeleka katika utekelezaji basi nchi hii ingegeuka kuwa ya maziwa na asali ndani ya muda mfupi lakini wapi ccm ndio donda ndugu joka la makengeza.
 
Penye ukweli tuseme,Tanzania inapitika sasa kwa kiwango cha lami tena barabara kubwa mikoa mingi,ukicompare barabara ya mombasa Nairobi na Dar Mwanza au Arusha utajua uzuri barabara zetu,pia sirari hadi nai bado hulinganishi kabisa na barabara zetu.anapostahili pongezi tumpe sio kila kitu kuponda.na siku zote maendeleo ya kweli huletwa na sisi wenyewe.
watu akili ndogo! Hivi miradi mikubwa kama barabara inaletwa na waziri? huyu si supervisor tu? Anayeweza kupewa credit kwenye miradi ya barabara ni yule aliyekuja na maamuzi ya kuanaza kujenga barabara kwa kutumia pesa za ndani pasipo kutumia mikopo na huyu ni MKAPA. Magufuli alikuwa supervisor tu kitu ambacho waziri yoyote ni wajibu wake na mbele ya mkapa hakuna waziri angefanya ujinga!

Tunataka Kiongozi siyo mnyampara. Rais ni kiongozi hivyo anahitajika mtu mwenye kuona mbali na mwenye kufanya maamuzi sahihi wakati wote yaani mwenyr hekima! Magufuli hana sifa hizo hata moja ni!mkurupukaji tu na ndiyo maana maamuzi yake yote yamejaa uonevu kwa ajili ya kutaka sifa huku akiumiza watu. Kama ukinipa magufuli na Dr.Slaa mimi nitampa Dr.Slaa kwa sababu anazo sifa za kiongozi kwa asilimia kubwa ukimlinganisha na magufuli. magufuli pia yupo ndani ya mfuamo ambao hana uwezo wa kufanya kinyume na waliomweka pale!
 
Kiukweli kwa siasa uchwara za vyama vya upinzani tz ulivyo jamaa anasubiri kuapishwa tu

Kwa wewe uliyoko ccm ndo utaona ni uchwara kwa sababu unataka wakurupuke ili mpate mwanya wakutokea.Mwaka huu mtabanwa mpaka mwisho hamtachomoka.Tembezeni mgombea wenu mpaka achuje kwanza!
 
Kuna watu wengi sana wanaishi kama kasuku wenyewe kazi yao kubwa ni kucopy maneno hata bila kufikiria na niwataalamu sana wa kucopy halafu yeye kama yeye unakuta hamna kitu kichwani
Alikuja lowassa walimpa sifa kibao hata ambazo hazipo
Nae makufuli hivyo hivyo ukimuuliza ivi kwanini unashoboka hivi anakuambia mimi mwenyewe sijui
 
Niliwahi kusoma mahali kuwa Tanzania inashika nafasi ya juu sana kwenye ushirikina. Pia nikasikia Watz wanaamini sana kwenye miujiza. Miujiza na ushirikina vinalanadana. Hata wale wanaolala makanisaani wakisubiri miujiza hawanatofautiani sana na hawa wengine.

Sababu kuu ya imani hizi ni akili finyu na kutopenda kufikiri pamoja na uvivu. Matokeo yake ni kama haya ya mauaji ya albino na mambo kama hayo.

Mleta mada anaangukia kwenye fungu hili. Huwezi kumwaangalia mtu au ukamsikia mtu akiongea sentensi chache tu halafu tayari ukamwamini eti atakuwa kiongozi bora bila kufikiri uongozi hasa Ikulu ni nini.

Ikulu ni taasisi na sio mtu. Matakwa ya mtu ambaye ndie rais yanaweza yasitekelezwe na hiyo taasis kwa hiyo maamuzi yake yakawa sifuri. Namshauri ajifunze system inavyofanya kazi na sio kuamini kwenye sura na maneno ya kisiasa ya Magufuli. Ajue Magufuli sasa hivi anaongea kama yeye, lakini akiwa rais hata hicho cha kuongea anaandikiwa na mtu mwingine.
Ajue CCM ina ajenda, sera na ilani zake ambazo akietenda tofauti hao hao wana CCM watampiga chini. Kuamini kuwa ataenda tofauti itakuwa ni MIUJIZA, kama wale wanaosubiri miujiza ifanyike kwenye maisha yao wapate hela za bure, na kupona magonjwa bila dawa.

Kinachotakiwa hapa ni rna real thing na sio miujiza. The real thing ni kuingoa CCm na agenda zake. Baasi.

Yatupasa kufikiri na kuachana na kuamini kwenye miujza na uchawi.
 
mliana hivyo hivyo kusifia mwaka 2005...eti tache siasa oooh sijui nini...hawa walewale...
 
watu akili ndogo! Hivi miradi mikubwa kama barabara inaletwa na waziri? huyu si supervisor tu? Anayeweza kupewa credit kwenye miradi ya barabara ni yule aliyekuja na maamuzi ya kuanaza kujenga barabara kwa kutumia pesa za ndani pasipo kutumia mikopo na huyu ni MKAPA. Magufuli alikuwa supervisor tu kitu ambacho waziri yoyote ni wajibu wake na mbele ya mkapa hakuna waziri angefanya ujinga!

Tunataka Kiongozi siyo mnyampara. Rais ni kiongozi hivyo anahitajika mtu mwenye kuona mbali na mwenye kufanya maamuzi sahihi wakati wote yaani mwenyr hekima! Magufuli hana sifa hizo hata moja ni!mkurupukaji tu na ndiyo maana maamuzi yake yote yamejaa uonevu kwa ajili ya kutaka sifa huku akiumiza watu. Kama ukinipa magufuli na Dr.Slaa mimi nitampa Dr.Slaa kwa sababu anazo sifa za kiongozi kwa asilimia kubwa ukimlinganisha na magufuli. magufuli pia yupo ndani ya mfuamo ambao hana uwezo wa kufanya kinyume na waliomweka pale!

viongozi wangapi wametafuna pesa za miradi,hili jembe kila wizara anayopewa anatusua,kazi zake zinaonekana,wewe kama unampenda slaa ni juu yako na akili yako kubwa,yangu unayoiona ndogo ishaona mbali kitambo Sana,mbwembwe za majukwaani hazitutishi,kura yangu ni kwa Magufuli na usijaribu kufikiri utaniteka akili.
 
Back
Top Bottom