Nimeupenda ustaarabu wa John Pombe Magufuli

Nimeupenda ustaarabu wa John Pombe Magufuli

gwamaka aswile

Senior Member
Joined
Mar 26, 2015
Posts
186
Reaction score
106
Tuachane na itikadi za kivyama, tuachane na ushabiki wa kisiasa nikimuangalia john pombe magufuli anavyoongea kila mahali anapopitwa kutambulishwa naamini kabisa tanzania imempata mtu sahihi wa kuivusha katika kipindi hiki kigumu cha kiuchumi na kisiasa. Ukweli mimi huwa naamini zaidi katika personality kuliko uvyama katika wanasiasa wa upinzani kwa wote kwa ujumla nikiwaangalia namuona dkt. Slaa ni mtu mwenye dhamira ya kweli kabisa kabisa so is magufuli ujue hawa jamaa ni watu ambao wako sirius sana. Nimempenda zaidi magufuli pale anaposema nikiwa rais nitakuwa rais wa watanzania wote si upinzani si ccm na nitawatumikia kwa moyo wangu wote. Sijayapenda zaidi maneno, la hasha bali nimependa namna anavyoyaongea ukweli ni kuwa hata ukimuangalia unaona kabisa kuwa huyu mtu ni mstaarabu. Japo kuna watu wanamkosoa kwa vitu vidogo vidogo lakini naamini kabisa magufuli atashauriwa kwenye vitu vidogo na atakuwa bonge la rais. Bila kusahau amweke muhongo kwenye nishati na filikunjombe apewe tamisemi awakomeshe wakurugenzi wezi ili maendeleo yaonekane fasta
 
magufuli kashindwa kujibu kashfa ya CAG ya bilion 263 sijui ndio alikuwa anajipanga uraHisi
Magufuli ni booonge la kiongozi. Kama hiyo kashfa ipo ataijibu tu ila mimi naamini haipo. Magufuli akiongea unajua kabisa kwamba yale maneno yanatoka ndani ya uvungu wa moyo wake. Huwa anapenda kutumia neno sincerly na kweli huwa anamaanisha anachokisema.

Kwa Magufuli tumelamba dume.
 
..sema ccm imepata mtu , rais wa tz si magufuli...
 
Akuna jipya hapo kwanza nawashanga mnasema tumelamba Dume kivipi? Ni kipi atakachokifanya nje ya matakwa y ilani ya ccm?
 
Mkuu usiangalie usanii wa mtu. Zile filamu za kiNaijeria wale wasanii wanaweza kuigiza kama wafalme wakubwa, wanaweza kuomboleza na kulia zaidi ya waliofiwa, wanaweza kuigiza kama majambazi na kadhalika. Usimwangalie mtu anavyoongea wala anavyoonekana ukapitisha kuwa tayari huyo ni raisi. Kikwete wakati wote amevaa cheating smile. Ukimchagua kwa tabasamu lake itakula kwako. Angalia sifa zingine za ndani zaidi ya hizo!!!!
 
Akuna jipya hapo kwanza nawashanga mnasema tumelamba Dume kivipi? Ni kipi atakachokifanya nje ya matakwa y ilani ya ccm?
Khaa!! Wewe umechelewa sana. Hizi ilani ni stori tu za vijiweni wala sizikuchanganye. Cha muhimu ni usimamizi wa utekelezaji wa ilani hizo. Tumeona jembe hili lilivyokuwa halina mzaha katika utekelezaji katika wizara. Kama kusoma hujui hata picha?
 
Magufuli ni booonge la kiongozi. Kama hiyo kashfa ipo ataijibu tu ila mimi naamini haipo. Magufuli akiongea unajua kabisa kwamba yale maneno yanatoka ndani ya uvungu wa moyo wake. Huwa anapenda kutumia neno sincerly na kweli huwa anamaanisha anachokisema.

Kwa Magufuli tumelamba dume.

Kama alishindwa kujibu siku zote sembuse akishakua raisi? Magufuli katununulia kivuko kibovu nalo unataka akishakua rais ndio atujibu?
 
Jakaya alishasema atakuja Rais mwenye Umri sawa na yeye wakati anakuwa Rais (Miaka 55), pia alisema mbele ya Mabalozi kule China kuwa Rais ajae atakuwa bora kuliko yeye. Ni John Pombe Magufuli ila upande wa wabunge tumpunguzie wabunge ''ndio "kwa kuchagua wapinzani wengi. Jana Lowassa sijamuona siku ya Mashujaa viwanja vya mnazi mmoja sio kawaida yake labda hangover ya "kamati ya Maadili "haijaisha
 
Khaa!! Wewe umechelewa sana. Hizi ilani ni stori tu za vijiweni wala sizikuchanganye. Cha muhimu ni usimamizi wa utekelezaji wa ilani hizo. Tumeona jembe hili lilivyokuwa halina mzaha katika utekelezaji katika wizara. Kama kusoma hujui hata picha?
Rohombaya kumbe huna roho mbaya penye ukweli unasema tu.
 
Last edited by a moderator:
Tuachane na itikadi za kivyama, tuachane na ushabiki wa kisiasa nikimuangalia john pombe magufuli anavyoongea kila mahali anapopitwa kutambulishwa naamini kabisa tanzania imempata mtu sahihi wa kuivusha katika kipindi hiki kigumu cha kiuchumi na kisiasa. Ukweli mimi huwa naamini zaidi katika personality kuliko uvyama katika wanasiasa wa upinzani kwa wote kwa ujumla nikiwaangalia namuona dkt. Slaa ni mtu mwenye dhamira ya kweli kabisa kabisa so is magufuli ujue hawa jamaa ni watu ambao wako sirius sana. Nimempenda zaidi magufuli pale anaposema nikiwa rais nitakuwa rais wa watanzania wote si upinzani si ccm na nitawatumikia kwa moyo wangu wote. Sijayapenda zaidi maneno, la hasha bali nimependa namna anavyoyaongea ukweli ni kuwa hata ukimuangalia unaona kabisa kuwa huyu mtu ni mstaarabu. Japo kuna watu wanamkosoa kwa vitu vidogo vidogo lakini naamini kabisa magufuli atashauriwa kwenye vitu vidogo na atakuwa bonge la rais. Bila kusahau amweke muhongo kwenye nishati na filikunjombe apewe tamisemi awakomeshe wakurugenzi wezi ili maendeleo yaonekane fasta

Inaonekana wewe ni mwepesi kuwa impressed na vitu vya kufikirika.
Magufuli hawezi kuwa kiongozi bora.
Thats guaranteed.
 
Magufuli ni booonge la kiongozi. Kama hiyo kashfa ipo ataijibu tu ila mimi naamini haipo. Magufuli akiongea unajua kabisa kwamba yale maneno yanatoka ndani ya uvungu wa moyo wake. Huwa anapenda kutumia neno sincerly na kweli huwa anamaanisha anachokisema.

Kwa Magufuli tumelamba dume.

Mfumo wa CCM hauwezi kumfanya Magufuli as effective as you think.
 
John Pombe yuko vizuri. Anasimamia sheria hadi nukta ya mwisho.

Alipouza nyumba za serikali alikuwa anasimamia serikali gani?
Barabara mbovu zimejengwa chini yake, huo usimamizi ni wa aina gani?
 
Back
Top Bottom