Nimeumia sana

Nimeumia sana

roho imeniuma sana
nimezaa na aliyekua mchumba wangu, kutokana na matatizo ya hapa na pale hatukubahatika kufunga ndoa japo tuliachana vibaya lakini nilijipa moyo tu.
nilipojifungua nilimtaarifu alinipa hongera japo hakuhudumia wala matimizi hakutoa ila alitoa jina na hatukuwasiliana tena na ni miezi 2 sasa.
kabla alikua anamtoto wa miaka 7 alizaa na mwanamke mwingine na walisha achana pia.
leo nimetumia acount ya mtu mwingine fb nimechart nae mpaka kafikia kunitaka uchumba katika kukibali nikamwelezea story feki ya maisha na yeye akaniambia.
kilichoniuma hamtambui mtoto wangu kasema anamtoto mmoja tu!!!
nimeumia sana mungu shahidi sijawahi kumsaliti na yeye analijua hilo sikuwahi kabisa kumchanganya na mwanaume mwingine mungu wangu wa mbinguni ni shahidi.
hata kama mimi hanitaki kwa nn asimtambue mtoto wake? asimtunze sawa lakini ajue ni mtoto wake. nimeumia sana jmn!!!

Umezaa nae ama amakuzalisha?
 
Usijipe presha hio ndio tabia za baadhi ya wanaume ambao hawapo responsible, angesema ukweli huoni kwamba angekataliwa? Inabidi adanganye tu huyo wako angemjua akishatimiza matakwa yake.
 
Pole sana mtoto wako anakuhitaji sn usimtupe maana situation kama ndo utasikia mtoto huko chooni, maana wadada wa dot com acha tu, songa songa songa mbele hata watu wakuseeeeme
 
Tatizo ni pale ulipoamua kuzaa kabla ya ndoa. Pole lakini sasa achana nae huyo mwehu we endelea na maisha yako, ipo siku Mungu atakupa mwanaume mwingine anayejitambua.OVER
 
Dada una uakika ujafanya jambo lolote la kumkwaza shemeji labda shemeji ni mvumilivu anaweza akakuta msg kwenye cm yko akapata picha ya mtoto co wake lkn akashindwa kukwambia pole sana lkn kma ilikuwa mnapendana iweje akatae dam yke
 
Inawezekana kajaribu kashndwa hasa ukizingatia ndo kwanza miezi miwili toka ajifungue,by the way time,pain and tears will heal her ajipe muda tu, nothing hurt forever

Na hakuna permanent situation duniani..........afute vumbi asonge mbele.........
 
Kama umeweza kulea na kujifungua bila msaada wake na unaendelea kusurvive unamtafuta wa nn?????? be strong......... bus likiharibika shuka beba mizigo yako panda lingine endelea na safari.
 
Ndiye yeye...

So far sijaona kitu chochote contradictory isipokuwa huyu binti/mwanamke ni kama ana mental breakdown hivi...

Ni wale wanawake wanaoweka mioyo na akili zao zote kwa wanaume, sasa kasheshe huwa ni pale wanapoachwa na si kuachwa tu bali wanatiwa na kibendi kabisa...

25 August 2014
Natafuta baba mlezi

Mama pita,samahani kama ntakuwa nimekuchanganya,sio wewe uliyewekaga thread Kuwa unatafuta baba mlezi atakayekuwa tayari umpe mtoto akishazaliwa,na wakati huo ulikuwa na ujauzito wa miezi 8?na tukakushauri cha kufanya,sio we we kweli? Mi sio mfukunyuaji mzuri wa thread zilizopita ila kumbukumbu zangu zinaniambia kama ni we we!kama nimejichanganya utanisamehe!
 
Back
Top Bottom