Nimetoa rushwa leo kwa traffic

Nimetoa rushwa leo kwa traffic

Hii kitu hakiezi kuisha.kwanza nimekutwa na kosa la overspeeding in residential area.pili insurance imeisha muda tatu sijafunga mkanda. Ingenitoka kama 90,000 hivi. Yeye mwenyewe akaanza kuniuliza unashilingi ngapi..ah nikatoa 10,000 mfukoni nikaendelea na safari,mambo mswano kabisa

Wewe una matatizo makubwa kuliko huyo huyo uliyemhonga 10,000/= sijui usaidiweje sasa, labda uende kituo cha polisi kilicho karibu nawe utoe hiyo taarifa ili ufunguliwe kesi mahakamani na ufungwe walau miezi mitatu tu ujue kweli kwamba ulifanya makosa, maana sasa yamefika manne
 
Hii kitu hakiezi kuisha.kwanza nimekutwa na kosa la overspeeding in residential area.pili insurance imeisha muda tatu sijafunga mkanda. Ingenitoka kama 90,000 hivi. Yeye mwenyewe akaanza kuniuliza unashilingi ngapi..ah nikatoa 10,000 mfukoni nikaendelea na safari,mambo mswano kabisa

Stupidity!
 
Mleta uzi inaonekana ana undugu na "NAPe". Maana hata utindio wake wa ubongo unadhìhirisha ni SHAKE WELL BEFORE USE.
Ni sawa na mtoto anye kitandani alafu atambe mbele ya watoto wenzake mimi leo nimekunya kitandani. Unahisi mwisho wa siku LOFA ataonekana nani..!?
 
Hii kitu hakiezi kuisha.kwanza nimekutwa na kosa la overspeeding in residential area.pili insurance imeisha muda tatu sijafunga mkanda. Ingenitoka kama 90,000 hivi. Yeye mwenyewe akaanza kuniuliza unashilingi ngapi..ah nikatoa 10,000 mfukoni nikaendelea na safari,mambo mswano kabisa
Mbona ni kawaida tuu mkuu?
Tena ningekukamata mie ningekuacha tuu uchape mwendo,upendo kwanza kazi baadae!
 
Tatizo ni kusema ukweli? mbona ni maisha ya mujini hayo woooooote twayajua!
 
sikuamini kabisa maneno ya mtoa mada na namna alivyojiona mshindi. ama kweli kazi tunayo. hawa ndio wanajamii tulionao na huku wengine tunataka mabadiliko.

haya nayo yamoooooooooooooo
 
Hii kitu hakiezi kuisha.kwanza nimekutwa na kosa la overspeeding in residential area.pili insurance imeisha muda tatu sijafunga mkanda. Ingenitoka kama 90,000 hivi. Yeye mwenyewe akaanza kuniuliza unashilingi ngapi..ah nikatoa 10,000 mfukoni nikaendelea na safari,mambo mswano kabisa
Yaani wewe ungejulikana ingebidi ufungwe kabisa kwani umekiri mwenyewe kosa la jinai la kutoa rushwa
 
Ha haa haaa kwi kwi kwi. yaani kuishi kwingi kuona mengi na duniani kuna kila aina ya watu.


This shows how ignorant you are!!
  • Over speeding kwenye makazi ya watu, je unaona ni fahari sana ungejisikiaje kama ungegonga mtu katika eneo hilo?
  • Umetoa rushwa ya shs 10,000.00, badala ya kujisikitikia umefanya kosa, wewe wajitutumua ati umetoa rushwa,
  • Gari halikuwa na insurance: Gari umeazima!! au ni la kwako!? kwa mtazamo wa harakaharaka yaonekana una ulimbukeni na gari, na inavyonekana utaendelea tu kutoa rushwa ambayo eventually itakuwa sawa na kulipia insurance
  • Looks like umeanza kuendesha gari hivi karibuni, kama sivyo, basi una ugeni na mambo ya magari
  • Halafu umeleta thread hapa ili iweje? tukupe pole kwa kutoa rushwa?????
 
Kwanza wewe si Dereva ndiyo mnaodharirisha kazi za watu. Una overspeed kwenye makazi hlf umetoa rushwa unajisifu?

Hii nchi inatakiwa iwe na sheria za kuuwa wala rushwa. Tunatoka povu kukemea wewe unakuja kwa kinywa kipana kbs eti leo umetoa

Ulijua kbs unafanya makosa yaani ilibidi uwe Ukonga muda huu.

Nakumbuka siku moja kwenye UBU Kamanda Mpinga alisema faini wanaweza sasa iwe ni Mahabusu halafu Kifungo.

Kwahiyo hapo ana makosa manne na hilo la kutoa rushwa, ila kiukweli kuna vitu vingine tunawalaumu police wanapenda rushwa kumbe hata sie tunawajengea mazingira ya kula rushwa, ukiangalia makosa hayo yote yanazuilika na yamesababishwa na dereva. Wote na police wake wanatakiwa adhabu kali hapo
 
Hii kitu hakiezi kuisha.kwanza nimekutwa na kosa la overspeeding in residential area.pili insurance imeisha muda tatu sijafunga mkanda. Ingenitoka kama 90,000 hivi. Yeye mwenyewe akaanza kuniuliza unashilingi ngapi..ah nikatoa 10,000 mfukoni nikaendelea na safari,mambo mswano kabisa

Rafiki Pole sana,

Umetenda makosa matano,

1) Overspeeding in residential area
2) Insurance imeisha
3) Haujafunga mkanda
4) Umetoa rushwa
5) Unatangaza na kujisifu kufanya madhambi haya.

Je haujui kwamba Overspeeding in residential area can kill someone ?

Je haujui kwamba kufunga mkanda ni kwa ajili ya usalama wako Mwenyewe ?

Je haujui kwamba kutoa na kupokea rushwa ni haramu na inadhuru uchumi wa inchi yako ?

Muombe Mungu akusamehe.
 
Nimeanza kuelewa kwamba kuna watoto hapa wanaoiba magari ya shemeji zao, au baba zao halafu wanakuja hapa kuongea mambo ya kitoto kabisa! Hebu angalia huyu kutoa elf 10 anakuja kututangazia hapa wakati anajua kwamba ni kosa! Sijui anataka tuseme asante au tumuone mpumbavu au nani? Pumbaf
 
Hii kitu hakiezi kuisha.kwanza nimekutwa na kosa la overspeeding in residential area.pili insurance imeisha muda tatu sijafunga mkanda. Ingenitoka kama 90,000 hivi. Yeye mwenyewe akaanza kuniuliza unashilingi ngapi..ah nikatoa 10,000 mfukoni nikaendelea na safari,mambo mswano kabisa
Naona wachangiaji wengi wamekulaumu na wengine kukutukana na hii ndio hulka ya Mswahili.
Umeeleza ukweli wa mambo uliyofanya leo mojawapo likiwa ni kumpa rushwa askari polisi wa barabarani.Hukuishia hapo na ukatoa tofauti ya faini na rushwa uliyotoa.
Mimi naomba tuliangalie jambo hili from another angle,faini zinapunguza ajali wakati system ni corrupt?Kwa mtizamo wangu ni afadhali faini ziwe kidogo ili ziwazuie watu kutoa rushwa lakini unapokuwa na faini kubwa halafu kuanzia RPC mpaka constable wote wananuka rushwa husaidii kuongeza kipato,kupunguza ajali wala kuwasaidia wananchi ila unaharakisha kufa kwa askari wetu kwani wanakuwa na pesa nyingi wasizozitokea jasho na kama tujuavyo "pesa huongeza urijali"
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom