mzeempili
JF-Expert Member
- Aug 16, 2021
- 327
- 531
Kuelekea mwishoni mwa mwaka 2019 nilikuwa na kazi ya miezi mitano mkoani Kigoma. Nikiwa huko nilikutana na classmate na roommate wa chuo niliyesoma naye miaka ya nyuma DIT.
Tulipiga stori za hapa na pale, tukazoeana kiasi. Akajitambulisha kuwa anafanya kazi kwenye shirika la misaada, na pia anajishughulisha na kuagiza magari. Tulivyoendelea kukutana na kuzoeana tulizidi kufahamiana. Bahati mbaya nilijikuta nimefunguka kuwa nilikuwa ninapanga kununua gari.
Tulivyokuwa tunaendelea kuonana, jamaa alianza kunionyesha mawasiliano na kampuni za kuagiza magari, na kuniaminisha kuwa tunaweza ku-save hela kama ataagiza gari yeye, kisha gari likifika atanikabidhi.
Alinishawishi kuwa nimpatie kile kiasi cha kulipia nje huko, millioni 13. Kwa kumwamini, nilimwekea kwenye akaunti yake ya benki. Nikabaki na bank slip.
Ulipofika wakati wa gari kufika, jamaa alianza hadithi. Mwanzo alidai nimpe muda atoe gari, kisha atanipatia tumalizane. Zikapita zaidi ya wiki. Baadae akasema kuna mtu amelipenda, ananunua kwa bei nzuri, tuagize lingine. Akadai amesafiri, anarudi tutaonana.
Nilipoona anazunguka kinyume na makubaliano nikampeleka polisi. Afande niliyemkuta akampigia simu, jamaa akafika, akakubali kuwa ameuza gari ananirudishia pesa yangu na nyongeza. Tukaandikishana nikatulia.
Baada ya hapo, mpaka leo imekuwa ni mwendo wa kuzungushana kila mahali, na pesa sijapata. Kila akipigiwa simu anadai amepata majanga, mara vifo, nk.
Hajalipa pesa zangu.
Naombeni ushauri namna bora ya ku-deal na mtu wa aina hii.
Natanguliza shukrani za dhati.
Tulipiga stori za hapa na pale, tukazoeana kiasi. Akajitambulisha kuwa anafanya kazi kwenye shirika la misaada, na pia anajishughulisha na kuagiza magari. Tulivyoendelea kukutana na kuzoeana tulizidi kufahamiana. Bahati mbaya nilijikuta nimefunguka kuwa nilikuwa ninapanga kununua gari.
Tulivyokuwa tunaendelea kuonana, jamaa alianza kunionyesha mawasiliano na kampuni za kuagiza magari, na kuniaminisha kuwa tunaweza ku-save hela kama ataagiza gari yeye, kisha gari likifika atanikabidhi.
Alinishawishi kuwa nimpatie kile kiasi cha kulipia nje huko, millioni 13. Kwa kumwamini, nilimwekea kwenye akaunti yake ya benki. Nikabaki na bank slip.
Ulipofika wakati wa gari kufika, jamaa alianza hadithi. Mwanzo alidai nimpe muda atoe gari, kisha atanipatia tumalizane. Zikapita zaidi ya wiki. Baadae akasema kuna mtu amelipenda, ananunua kwa bei nzuri, tuagize lingine. Akadai amesafiri, anarudi tutaonana.
Nilipoona anazunguka kinyume na makubaliano nikampeleka polisi. Afande niliyemkuta akampigia simu, jamaa akafika, akakubali kuwa ameuza gari ananirudishia pesa yangu na nyongeza. Tukaandikishana nikatulia.
Baada ya hapo, mpaka leo imekuwa ni mwendo wa kuzungushana kila mahali, na pesa sijapata. Kila akipigiwa simu anadai amepata majanga, mara vifo, nk.
Hajalipa pesa zangu.
Naombeni ushauri namna bora ya ku-deal na mtu wa aina hii.
Natanguliza shukrani za dhati.
