Chamoto
JF-Expert Member
- Dec 7, 2007
- 8,319
- 17,473
Nimeshangazwa na kusikitiswa kuona kuwa tovuti ya bunge la Tanzania ambayo inatumia ip adress 66.187.104.94linatunza mafaili yake Marekani. Kwakweli nimeshtuka kwasababu bunge ni nguzo muhimu katika nchi yetu, huwezi kutunza mafaili yake nje ya nchi.
Inakuwaje taarifa muhimu na hata zile za siri kuhifadhiwa ughaibuni? Hivi nchi husika (US) ikiamua kufunga hiyo akaunti kama walivyofanya Megaupoad, Bunge la Tanzania litafanya nini?
Mwisho natoa pongezi kwa Tovuti ya Taifa kutunza mafaili yake nchini.
Inakuwaje taarifa muhimu na hata zile za siri kuhifadhiwa ughaibuni? Hivi nchi husika (US) ikiamua kufunga hiyo akaunti kama walivyofanya Megaupoad, Bunge la Tanzania litafanya nini?
Mwisho natoa pongezi kwa Tovuti ya Taifa kutunza mafaili yake nchini.