Nimesitisha kumuombea Rais

Nimesitisha kumuombea Rais

There is a prayer.. And they are prayers... Hopefully you belong to prayers..
 
Hivi kuna haja gani kuombewa na Shetani. Wengine dua zao zinakuwa kama za kuku kwa mwewe
 
Hivi kuna haja gani kuombewa na Shetani. Wengine dua zao zinakuwa kama za kuku kwa mwewe
Una maana rais aliomba kuombewa na shetani au unawafananisha Watanzania na shetani, waombe radhi.
 
Hivi kuna haja gani kuombewa na Shetani. Wengine dua zao zinakuwa kama za kuku kwa mwewe
Huyu tukimuombea ndio anazidi kuwa kama shetani mkuu Lucifer. roho mbaya,visasi,kejeli,kiburi na vitisho.miungu ya ghamboshi imetuzidi ujanja.
 
Wengi wetu huwa tunatarajia hali zetu za kimaisha kuwa nzuri kadri ya siku zinavyosonga mbele, mbaya hali inapokuwa kinyume na mbaya zaidi ukikuta ugumu wa maisha unasababishwa na mkono wa mwanadamu kwa makusudi. Hakuna maendeleo kwa taifa letu yatakuja bila kuanza kwa kuboresha hali za maisha kwa walio wengi ama utakuwa unalenga kundi la watu wachache. Hali ya maisha itaimalika pale watawala (maana viongoz ni adimu) wetu watazipa kipaumbele sekta zinazowagusa wananchi moja kwa moja kama matibabu, elimu bora, kilimo na tunashukuru awamu zilizopita kwa sasa sekta ya usafirishaji imeimarika barabara zinapitika.


Watanzinia walio wengi ni wakulima, hivyo mikakati ingewekwa kwanza kuongeza uzalishaji wa mazao ya kilimo na mifugo, upatikanaji wa masoko sambamba kujenga viwanda vya usindikaji wa mazao ya kilimo na mifugo. Selikari ina wajibu wa kuhakikisha inafanikisha hili kwa kuwawezesha wadau na ikizingatia kund kubwa la vijana halina ajira. Naamini watawala wetu wakiwekeza nguvu kama walizowekeza kwenye zoezi la uhakiki kwa watumishi, watafanikiwa.
 
43:26 "Unikumbushe, na tuhojiane; eleza mambo yako, upate kupewa haki yako".
Serikali Imetugeuka Mkuu Tunaikumbusha Tunahojiana Nayo Ila Imekuwa Mbogo Haitusikilizi Inajifanyia
Mambo Yetu Yametupwa Hasa Ahadi Ya Kuwasikiliza Masikini Na Wenye Mahitaji

"Mungu Anaiona Hii Serikali Ya Ccm"
 
Mkuu Quinine Nimekupenda bure! Maamuzi yako yanakutoa kwenye laana, ya kuombea vitu batili kwa Mungu, Bora ukaiombea Israel utapata baraka kwa Mungu, kuliko kupoteza muda kumwombea uchwara
Huo utakua ni umamluki waisraeli waliwahi lini kutombea?Kama unaamini waisraeli ndiyo bora kuliko Tanzania nenda kaishi huko.
 
Mtakuwa mnamuombea kwa shetani na wala sio yule muumba wa mbingu na nchi
 
Huo mda niliokuwa nautumia kumuombea mzee sasa hivi bora niutumie nikabetie kukimbiza mbwa huenda nikaondoka na chochote
 
Ngonipost: 18164328 said:
Mkuu Quinine Nimekupenda bure! Maamuzi yako yanakutoa kwenye laana, ya kuombea vitu batili kwa Mungu, Bora ukaiombea Israel utapata baraka kwa Mungu, kuliko kupoteza muda kumwombea uchwara
Wewe unadhani shetani anafurahia jinsi Mungu anavyobariki Tanzania? La hasha! Anafurahia anapoona akina Kwinini wanakata tamaa wakati wengine wanaendelea kutukuza taifa lisilo lao.
 
Hatuwezi kuendelea kumwombea mtu asiyemwamini Mungu mambo mengi anaigiza kuliko uhalisia.
 
nilimuona mapema bwana gomora a k a mzee wa kuwait na libya, kwamba hatoshi na hajui, na elimu yake ya maganda ya maembe haihusiani kabisa na uongozi wa gomora..
ndio maana kale ka tiki nilikaweka kwa wasiyempenda !
nadhani sihusiki na maafa ya gari bovu..

mimi ninavyojua jamaa ana mademu sita..
lol
sijui ni ukuwadi sijui ni umbea...

sijui bado nipo kwenye mada ?
 
Alipochaguliwa tu alitusihi Watanzania wote bila kujali itikadi zetu, makabila yetu na dini zetu tumwombee, kwa kile alichosema alichokikuta kule kilihitaji maombi.

Kweli kama Mtanzania nilianza maombi ya nguvu, nilitenga siku moja ya mwezi kufunga kwa ajili yake nikijua kazi aliyonayo ni ngumu na ya hatari.
Pamoja na kufanya hivyo, leo takriban mwaka unakwisha bila kuona faida ya maombi yangu. Maisha ndiyo yamezidi kuwa magumu afadhali ya mwaka jana.

Katika maombi yangu nilitegemea atakuwa rais wa wanyonge kama alivyoahidi.
Nilitegemea atakuwa rais wa vyama vyote, dini zote na makabila yote kama alivyoahidi. Nilitegemea rais atakuja kuwapata mikopo wanafunzi wote kama alivyoahidi.

Nilitegemea maombi yangu yatambadili na kutawala kwa haki kwa kufuata utawala wa sheria, rule of law. Nimesubiri ahadi yake ya ajira kwa vijana kama alivyoahidi, matokeo yake kaajiri vijana kwa kuangalia ukada na mbaya zaidi kaajiri vijana wenye ukakasi mbele ya jamii.

Matokeo ya maombi yangu ni kusitishwa kwa ajira, kunyanyaswa kwa watumishi wa umma kwa kisingizio cha kuhakiki wafanyakazi hewa.
Maombi yangu yamesababisha wafanyabiashara kunyanyaswa kwa kuongezewa kodi zisizo na ulazima.

Nilitegemea madawa yataongezeka mahospitalini, matokeo yake hata dawa ya chanjo kwa watoto imekosekana. Naona kama maombi yangu yanazidisha ugumu wa maisha kwa wananchi. Kwanini basi niendelee kuomba?

Kama mwaka jana niliishi vizuri, watoto walisoma bila kumwombea rais aliyekuwepo, ajira zilikuwepo wafanyakazi walipanda madaraja bila kumwombea rais aliyekuwepo, wanafunzi walipata mikopo tena wote bila kumwombea rais aliyekuwepo, kuna sababu gani basi kuendelea kumwombea aliyepo?

Nimestisha maombi.

Ni uamuzi wangu sijashinikizwa na mtu.

Quinine.






Maombi hayasusiwi!!
Omba na endelea kuomba bila kukoma!
Tukisusia wote, ataombewa na na nani?
La sivyo maombi yako yako njiani karibu yanajibiwa usisusie!
 
Huo utakua ni umamluki waisraeli waliwahi lini kutombea?Kama unaamini waisraeli ndiyo bora kuliko Tanzania nenda kaishi huko.
sasa kama unabishana na Neno la Mungu juu ya Taifa lake teule, wewe utakuwa shetan ambae anauwa watu kwa siri alafu anakuja kuomba aombewe!
 
Back
Top Bottom