Nimeshindwa, Nahama Chadema

Nimeshindwa, Nahama Chadema

Kenge kama wewe huwezi kuwa Chadema maana IQ iko down kishenzi labda useme wewe ni mwanachama wa TLP au UPDP
 
Kwanza kabisa ulivyojiunga haukutuambia, ulifanya hivyo kimya kimya nashanga sasa hv unajidai unaaga..! acha unafiki.
pili kama kweli wewe ni mwanamapinduzi kile kitendo cha wabunge wa chadema kutoka bungeni ungekifurahia caz ni cha kawaida sana kwenye politics kwa pande zinazopingana ama kutokubaliana kwa mambo flan, sio tu watu wanatokaga kwenye mabunge yao hata kwenye mikutano ya umoja wa mataifa wa maraisi watu wanatokaga wkt rais flan wasiekubaliana nae anapohutubui sa nashangaa wewe hili kukutoa kwenye chama me nadhani we umetumwa kama hauna kichwa cha PANZI ie mgumu wa kuelewa mambo....!
 
Hivi huo ukabila umekuja baada ya Chadema kususia hotuba za wachakachuaji? Hukuwa na lolote huna lolote na wala hutakuwa na lolote. Ua not among 'great thinkers' we ni kenge uliyedandia msafara wa mamba. Wote mtadrop, speed ya Chadema hamuiwezi. Hiki si Chama cha wakurupukaji. We analyse things and think critically b4 taking any decision.
 
huyu jamaa katumwa,na sasahivi hakuna mtu anayeweza kudanganyika.alaf wakati anachuka kadi hakuambia sasa mbona anakuja kuaga,kwanza huu mtandao ni wawajanja watu kama hawa sijui wanajichomeka humu kivipi,fukuza kabisa huyoo

Wewe ni mwanachama tu katika JF kama nilivyo mimi hata kama mimi si 'mjanja' kama wewe.

Toa hoja, acha chuki. After all, hii siyo forum ya Chadema.
 
Msimlaumu amelishwa unga wa ndele sasa inafaa apewe unga wa rutuba ili apate aikli na unapatikana cdm tu.
 
Haya mataahira mengine yanaharibu sana j-2 za watu . Toka na usiandike tena hapa jamvini

Jamvi hili ni mali yako? au umekaribishwa tu kama mimi?

Wewe ni mmoja wa watu wenye chuki mbaya bila sababu.

Badala ya kutoa hoja unamshambulia mtu.

Lakini sishangai sana, watu wa aina hii ndio waliojaa Chadema.
 
Kweli kabisaa waliotumwa na CCm wameshaanza kuumbuka mmoja baada ya mwingine
 
mchakato wa kuitafuta demokrasia ya kweli si lelemama, hongereni wabunge mlio kua na misimamo ya dhati kabisa kutetea kilichokua na maslahi kwa walio wengi .katiba mpya na tume huru ya uchaguzi
 
Nimeamua rasmi kukihama chama nilichokipenda kutokana na yaliyojiri bungeni. Narudisha kadi wiki ijayo.

Nilikipenda sana chama changu lakini kuendelea kuwa mwanachama nitakuwa siitendei haki dhamira yangu.

Nimeng'amua kwamba CCM ndicho chama makini chenye kuitakia mema nchi yangu Tanzania na kitakachoweza kuleta maendeleo ya kweli kwa kila mwananchi.

Chadema pamejaa ubinafsi na ukabila. Aidha viongozi wamekosa dira na ukomavu wa kisiasa.

Wenye mawazo kama ya kwangu juu ya Chadema mnakaribishwa CCM.

Kidumu Chama Cha Mapinduzi!

Zidumu fikra za Mwenyekiti na RAIS wetu JK.

ure makin me to through out,pls cut the crap!
 
ulifikiri huku kuna vyeo vya kupendeleana na uswahiba huku ni maslahi ya taifa tu, huku hakuna jino kwa jino wala uswahiba huku ni mapambano wala hatuna mchezo wala kujipendekeza , thread zetu zilivyo ndivyo tulivyo.

Mzee Gomezi
 
“MPAKA sasa, bado nashindwa kuelewa, ni vigezo gani hasa vilivyotumiwa na Chadema, kuwapata wabunge wa viti maalumu, maana, baadhi ya wanawake walioteuliwa ninawazidi elimu, muda wa kujiunga na chama, michango katika chama na hata nafasi za uongozi katika ngazi mbalimbali.”


Huyo ni Leticia Musori, aliyekuwa maarufu kwa jina la mama Bawacha. Alikuwa Mwenyekiti wa Taifa wa Baraza la Wanawake wa Chadema kabla ya kukihama chama hicho.


Musori anasema uamuzi wa kujiondoa Chadema unatokana na kuchoka kuimba wimbo aliouita wa zidumu fikra za Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe ambaye anasema amekuwa akiwadhibiti wanawake na kuwazuia kufanya maamuzi yoyote wenyewe bila kuwaingilia.

Anadai akiwa Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake, Mbowe alikuwa akishinikiza Katibu wa Baraza hilo kuwa na mamlaka ya kiutendaji zaidi yake licha ya kuwa ndiye aliyekuwa bosi wake kiuongozi.



Anadai kwamba hali hiyo ilikuwa ikilalamikiwa na wanawake wengi lakini hawakusikilizwa na badala yake anasema aliahidiwa kuwa suala lake litajadiliwa na Katibu Mkuu bila mafanikio.


Baada ya kuona danadana, yeye na wenzake waliipuuza na kuamua kuchapa kazi lakini uvumilivu wao uliwatumbukia nyongo baada ya wanawake wa umoja huo kuingiliwa katika mchakato wa kuwachagua wanawake wanaoona wanafaa kuwawakilisha bungeni na badala yake jukumu hilo likapelekwa kwa wataalamu. Anaamini kwamba huo ulikuwa ni ujanja wa wakubwa kutaka nafasi ya kuteua watu kwa maslahi yao.

Vigezo vya kuteuliwa
“Wametaja vigezo vyao vyote, nimeangalia mimi ninavyo. Kama ni muda wa kutumikia chama nimejiunga na Chadema tangu mwaka 2004, tena nimeanza katika ngazi ya chini ya uongozi mpaka nikafikia hatua ya kuaminika na wanawake wenzangu na kunipa nafasi ya uenyekiti wa Taifa. Nimekuwa diwani kwa miaka mitano, nimekuwa mweka hazina wa madiwani wote wa Chadema.”



Mbali na uongozi ndani ya chama, anasema amekuwa katibu wa mitandao ya asasi zilizo za kiserikali katika Wilaya ya Tarime, Mwenyekiti wa Wanawake wa Kanisa Katoliki Jimbo la Ukonga, Mratibu wa Asasi ya Mkamilishano Trust Fund iliyokuwa na makao makuu yake Ujerumani na Mwenyekiti wa Tukamilishane Women Association.

Elimu
Ni mhitimu wa kidato cha nne aliyepata pia mafunzo ya uuguzi nchini Ujerumani kwa muda wa miaka minne katika ngazi ya stashahada.
“Naweza kuzungumza vyema lugha tatu, Kiswahili, Kiingereza na Kijerumani, najiuliza kati ya wabunge wote wa viti maalumu kwa nini waniache wakati wapo wabunge waliochaguliwa ambao nawazidi elimu, michango katika chama, uwezo na hata muda wa kukitumikia?” anasema.

Mchango katika Chama
"Nimetoa michango mingi ndani ya chama. Mwaka 2006 nililipia pango la ofisi ya chama kwa pesa zangu mwaka mzima. Nilitoa pesa zangu nikanunua kiwanja kwa ajili ya kujenga ofisi ya chama huko Tarime. Kiwanja hicho kilikuwa katika Kata ya Nyanungu. Sasa hivi hiyo kata imegawanywa na kipo katika Kata ya Ikiryo."



Anasema ingawa anaweza kuonekana kuwa na hasira baada ya kunyimwa ubunge, anaamini kuwa waliopo ndani ya Chadema ndiyo wanaojua ubovu wa viongozi na udhaifu walionao.
“Chadema imeendeleza uozo na udikteta katika kufanya maamuzi, bado kinaendeshwa kama kampuni ya wakubwa katika maamuzi mbalimbali. Hili la kuteua viti maalumu kwa misingi ya undugu, ubinafsi na mahusiano ya vigogo ni mfano tu wa malalamiko ya wanawake wengi” anasema.

Anasema kinachomkera ni kuwa uchaguzi halali wa baraza hilo ulivunjwa kwa makusudi na viongozi wa taifa wa chama hicho ili kutoa nafasi kwao kuingiza wanawake wanaowataka badala ya kuwaachia wenyewe wajiamulie na kujichagulia wawakilishi wanaowataka kama inavyoelekezwa katika kanuni za katiba ya baraza hilo.

Anasema katika uchaguzi wa wanawake wa baraza hilo uliofanyika PTA Temeke, alishika nafasi ya tano huku wabunge wote wa viti maalumu wa mwaka 2005-2010 wakiambulia kura mbili mpaka tano hali iliyokuwa ikiwazuia kuendelea kuwa wabunge.

Lakini anasema kwa nafasi yake na kwa wingi wa kura alizopata ameshindwa kuwa miongoni mwa wabunge 25 walioteuliwa jambo ambalo anasema mbali na kumshangaza na kumhuzunisha, limeonyesha kuwa chama hicho kina wenyewe.

Musori anasema uchaguzi wowote ni kipimo cha demokrasia siyo tu kwa serikali iliyopo madarakani, bali hata taasisi zote za kiraia pamoja na vyama vya siasa. Anasema Ndani ya Chadema demokrasia ni wimbo unaoimbwa kwa ajili ya watu wa nje na si wa ndani ya chama hicho.

Anatoa wito kwa Watanzania na wafuasi wa chama hicho kuacha ushabiki na kukitazama chama hicho kwa umakini mkubwa. “Ndugu zangu, mnaweza msinielewe, lakini iko siku mtaelewa, acheni ushabiki wa kisiasa, angalieni viini vyanzo vya vyama kabla ya kujiunga navyo,” anasema.

Source: Gazeti Mwananchi Tuesday 30 November 2010.




Comment: This is loud and clear!...THOSE ARE TRUE COLOURS OF CHADEMA!
 
Kumbe kukosa ubunge vitu maalumu ndicho kulichomweka chadema, kukosa tu alichotaka, basi anabweta. Hafai kuwa kiongozi ana tamaa tu ya vyeo
 
"MPAKA sasa, bado nashindwa kuelewa, ni vigezo gani hasa vilivyotumiwa na Chadema, kuwapata wabunge wa viti maalumu, maana, baadhi ya wanawake walioteuliwa ninawazidi elimu, muda wa kujiunga na chama, michango katika chama na hata nafasi za uongozi katika ngazi mbalimbali."


Huyo ni Leticia Musori, aliyekuwa maarufu kwa jina la mama Bawacha. Alikuwa Mwenyekiti wa Taifa wa Baraza la Wanawake wa Chadema kabla ya kukihama chama hicho.


Musori anasema uamuzi wa kujiondoa Chadema unatokana na kuchoka kuimba wimbo aliouita wa zidumu fikra za Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe ambaye anasema amekuwa akiwadhibiti wanawake na kuwazuia kufanya maamuzi yoyote wenyewe bila kuwaingilia.

Anadai akiwa Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake, Mbowe alikuwa akishinikiza Katibu wa Baraza hilo kuwa na mamlaka ya kiutendaji zaidi yake licha ya kuwa ndiye aliyekuwa bosi wake kiuongozi.



Anadai kwamba hali hiyo ilikuwa ikilalamikiwa na wanawake wengi lakini hawakusikilizwa na badala yake anasema aliahidiwa kuwa suala lake litajadiliwa na Katibu Mkuu bila mafanikio.


Baada ya kuona danadana, yeye na wenzake waliipuuza na kuamua kuchapa kazi lakini uvumilivu wao uliwatumbukia nyongo baada ya wanawake wa umoja huo kuingiliwa katika mchakato wa kuwachagua wanawake wanaoona wanafaa kuwawakilisha bungeni na badala yake jukumu hilo likapelekwa kwa wataalamu. Anaamini kwamba huo ulikuwa ni ujanja wa wakubwa kutaka nafasi ya kuteua watu kwa maslahi yao.

Vigezo vya kuteuliwa
"Wametaja vigezo vyao vyote, nimeangalia mimi ninavyo. Kama ni muda wa kutumikia chama nimejiunga na Chadema tangu mwaka 2004, tena nimeanza katika ngazi ya chini ya uongozi mpaka nikafikia hatua ya kuaminika na wanawake wenzangu na kunipa nafasi ya uenyekiti wa Taifa. Nimekuwa diwani kwa miaka mitano, nimekuwa mweka hazina wa madiwani wote wa Chadema."



Mbali na uongozi ndani ya chama, anasema amekuwa katibu wa mitandao ya asasi zilizo za kiserikali katika Wilaya ya Tarime, Mwenyekiti wa Wanawake wa Kanisa Katoliki Jimbo la Ukonga, Mratibu wa Asasi ya Mkamilishano Trust Fund iliyokuwa na makao makuu yake Ujerumani na Mwenyekiti wa Tukamilishane Women Association.

Elimu
Ni mhitimu wa kidato cha nne aliyepata pia mafunzo ya uuguzi nchini Ujerumani kwa muda wa miaka minne katika ngazi ya stashahada.
"Naweza kuzungumza vyema lugha tatu, Kiswahili, Kiingereza na Kijerumani, najiuliza kati ya wabunge wote wa viti maalumu kwa nini waniache wakati wapo wabunge waliochaguliwa ambao nawazidi elimu, michango katika chama, uwezo na hata muda wa kukitumikia?" anasema.

Mchango katika Chama
"Nimetoa michango mingi ndani ya chama. Mwaka 2006 nililipia pango la ofisi ya chama kwa pesa zangu mwaka mzima. Nilitoa pesa zangu nikanunua kiwanja kwa ajili ya kujenga ofisi ya chama huko Tarime. Kiwanja hicho kilikuwa katika Kata ya Nyanungu. Sasa hivi hiyo kata imegawanywa na kipo katika Kata ya Ikiryo."



Anasema ingawa anaweza kuonekana kuwa na hasira baada ya kunyimwa ubunge, anaamini kuwa waliopo ndani ya Chadema ndiyo wanaojua ubovu wa viongozi na udhaifu walionao.
"Chadema imeendeleza uozo na udikteta katika kufanya maamuzi, bado kinaendeshwa kama kampuni ya wakubwa katika maamuzi mbalimbali. Hili la kuteua viti maalumu kwa misingi ya undugu, ubinafsi na mahusiano ya vigogo ni mfano tu wa malalamiko ya wanawake wengi" anasema.

Anasema kinachomkera ni kuwa uchaguzi halali wa baraza hilo ulivunjwa kwa makusudi na viongozi wa taifa wa chama hicho ili kutoa nafasi kwao kuingiza wanawake wanaowataka badala ya kuwaachia wenyewe wajiamulie na kujichagulia wawakilishi wanaowataka kama inavyoelekezwa katika kanuni za katiba ya baraza hilo.

Anasema katika uchaguzi wa wanawake wa baraza hilo uliofanyika PTA Temeke, alishika nafasi ya tano huku wabunge wote wa viti maalumu wa mwaka 2005-2010 wakiambulia kura mbili mpaka tano hali iliyokuwa ikiwazuia kuendelea kuwa wabunge.

Lakini anasema kwa nafasi yake na kwa wingi wa kura alizopata ameshindwa kuwa miongoni mwa wabunge 25 walioteuliwa jambo ambalo anasema mbali na kumshangaza na kumhuzunisha, limeonyesha kuwa chama hicho kina wenyewe.

Musori anasema uchaguzi wowote ni kipimo cha demokrasia siyo tu kwa serikali iliyopo madarakani, bali hata taasisi zote za kiraia pamoja na vyama vya siasa. Anasema Ndani ya Chadema demokrasia ni wimbo unaoimbwa kwa ajili ya watu wa nje na si wa ndani ya chama hicho.

Anatoa wito kwa Watanzania na wafuasi wa chama hicho kuacha ushabiki na kukitazama chama hicho kwa umakini mkubwa. "Ndugu zangu, mnaweza msinielewe, lakini iko siku mtaelewa, acheni ushabiki wa kisiasa, angalieni viini vyanzo vya vyama kabla ya kujiunga navyo," anasema.

Source: Gazeti Mwananchi Tuesday 30 November 2010.




Comment: This is loud and clear!...THOSE ARE TRUE COLOURS OF CHADEMA!
Na wenyewe ni wanachama
 
Kumbe kukosa ubunge vitu maalumu ndicho kulichomweka chadema, kukosa tu alichotaka, basi anabweta. Hafai kuwa kiongozi ana tamaa tu ya vyeo
Namtazama kwa picha hiyo...............kama nia ni ubunge............. basi angegombea na kushinda........ viti maalumu vina vigezo na kama mtu hujavifikia basi ujuwe huwezi kupata
 
Sio kila mwanachadema anaweza kuwa mbunge nafasi chache jamani khaa.
Aende CCM watampa 2015
 
Nashangaa hivi ilikuwaje kwa uelewa anaouonyesha huyu mama kwenye taarifa zake alikuwaje Mwenyekiti wa Wanawake Taifa wa Chadema?

1. Kama alikuwa na vigezo vya kuwa mbunge, kwa nini asingeenda kugombea jimboni?

2. Alikuwa wapi kufanya maamuzi ya kukihama chama siku zote mpaka asubiri akose ubunge ndio ang'ake kwamba chama kimejaa upendeleo na hakina demokrasia?

3. Je kuzungumza kwa ufasaha lugha ya Kiingereza na Kijerumani ni sifa 'kubwa' ya kuwa mbunge mpaka anainadi hadharani?

4. Je haya malalamiko yake toka huko nyuma amewahi kuyafikisha kwenye vikao rasmi vya chama?

5. Je amefanya utafiti kuwa huko anakokwenda kuna hiyo 'demokrasia' anayoitaka?

Kweli wahenga walisema funga domo lako kuficha ujinga wako!!
 
Back
Top Bottom