Nimeshaelimisha jamii sana hapa JF ngoja Leo nijisifu,ofcoz ukiweza kuwa neutral kama Mimi jisifu

Beatrice Kamugisha

JF-Expert Member
May 18, 2019
762
6,980
Naitwa mwana wa Kamugisha, mzaliwa wa Bugandika nakukulia mtaa wa Pepsi Bukoba Town. Nikawa Mwalimu weee but no mafanikio. Nikaenda chuo kikuu kuongeza maarifa( SI unajua mhaya asifiwi wingi wa Mali anasifiwa Kwa ukubwa wa CV) nakufanikiwa kupata lower second in short sikuwahi kuwa na akili sana ila nikifanya mtihani nafaulu.

Miaka 1990 nikaenda kusoma diploma ya Nursing huko USA Ili nipate kujishikiza nitafute kuelewa Dunia inakwendaje. Usishangae wapo Mawaziri na wakuu wa mikoa sijui makatibu wakuu awajawahi kusafiri nje, Mimi siyo Kwamba nimesafiri Bali nimekaa Ulaya na Amerika. Nipigieni makofi.

Nimekaa huko weee but finally nikarejea Tanzania mwaka 2009 na kukaa Kidogo Kisha nikaenda kusoma ramani Ulaya. Ulaya nikagundua namna binadamu anavyobaguliwa kwa rangi, nikaelewa Kwamba wanachofanya wahaya waliowengi ni ubaguzi uleule wa Ulaya ila unafanywa Afrika. Ukitaka usibaghiliwe some tafuta pesa zunguka Dunia, wakikuuliza unapajua Newyork waambie mwaka 1996 nilipita Dubai kuelekea Afghanstani Kisha china nakuzungukia Dell kabla sijatinga Harizona kuangalia soko la bidhaa za asili. Mhaya unamziba mdomo

Tuachane na wahaya tuendelee, mwaka 2016 nikarejea home na umri nao ukawa umesonga ila nashukuru nilifanikiwa kujenga kibanda Bukoba na Masaki .So nikawa naishi Masaki na Bukoba go and return. Fedha ya kulisha Tumbo langu zipo so haba na uzuri Sina Mtoto Wala mjukuu anayenitegemea na Hii inatokana na ukweli Kwamba niliishi Marekani kwa malengo, familia yangu yote inajitegemea na nimshukuru MUNGU Kwamba alinifungua akili pamoja na kuwa na degree lakini akaniambia usife maskini jishushe kasome nursing upate nafasi ya kusomesha wanao elimu Bora na nzuri kuliko kukaa bongo ambapo hata madarasa Bado kukamilika kujengwa.

Nini nataka kusema, Kwa kipindi chote ambacho nimekaa hapa nchini nimegundua tunakwenda kutawaliwa siku si nyingi. Tunakwenda kutawaliwa Kwa sababu wapo viongozi wanaoamini Kwamba Dunia ipo imesimama ikisubiri tuelimike itubebe. No. Dunia inakwenda Kasi sana, wenye fedha na maarifa wapo njiani kuelekea mwezini sisi tunabishana kukopa au tusikope, tunabishana Uchaguzi 2025 bila kujua tutakuwa hai au tutakuwa kaburini, tunajisifu kujenga madarasa bila kujua wenzetu wanaangaika kwenda mwezini, tunaangaika kujadili udini wakati wenzetu wanaacha hata kwenda nyumba za ibada baada ya kutambua Dini sahihi haipo kanisani wala msikitini, Dini ni maisha binafsi ya mtu ambayo yakiwapendeza wanadamu yamempendeza MUNGU na yakimchukuza Mwanadamu yamemchukiza MUNGU; ndipo inapozaliwa dhana kwamba ametuumba kwa mfano wake.


Niwaombe Watanzania hasa vijana tokeni mkasake maisha nje ya mipaka Hii, tokeni mkasake maisha Ili wakitaka kuteua basi waone CV zenu huko kwenye mashirika makubwa Duniani. Tokeni mwache roho mbaya yakusema mbona wanaoteuliwa ni wahaya na Wachaga TU? Hakuna namna utafundisha mzizima ukajulikana Duniani,tembea. Ntatoa mfano wa makabila yaliyofanikiwa na ambayo hayatawaliki kirahisi na utagundua huko ndipo upinzani hata wa Kisiasa ulipo.

Tanzania Ina makabila mengi yaliyowekeza kulalamika kuhusu tatizo la ajira nchini na watasubiri watawala wawapige siasa mwisho watawatawala na ndicho kilichotokea kwenye Baraza jipya la Mawaziri Kwamba wamedhamiria kututawala. Lakini makabila yafutayo Wahaya, Wachaga, Wanyakyusa, Wameru, Wapare, Waha, Wamasai wakurya, wajaluo na Wapemba ni vigumu kwa umoja wao kulalamika ajira au kusubiri kutawaliwa maana walianza kujitawala miaka mingi. Mfano mzuri ukisoma historia unabaini Watu wa Kaskazini wakiongozwa na Mzee Japhet Crylo waliweza kuuza kahawa wakamtuma Mzee huyu wa Kimeru akawaombee Uhuru kabla hata ya Mwalimu nyerere. Tunalalamika wakina mtei n Msuya kujenga Barbara kwao , tunalalamika wakina na Waha kumiliki biashara nchini tukiwasingizia wachawi lakini ukweli nikwamba Hawa Watu wameachana na kuajiriwa . Maana yake Hawa Watu wanazo akili za kujitawala kabla hata hatujapata Uhuru na wameshatambua umuhimu wa kujiandaa wasitawaliwe. Wachaga wamesambaa Duniani na JPM alishindwa kupambana nao Kwa sababu wapo Kila familia nchini na nje ya nchi. Sisi wahaya na makabila mengine ya mpakani tumesafiri nje na tunaelewa Dunia inakwenda wapi. Hivyo ni muda Sasa wakukubali kwamba familia zetu zitoe wawakilishi waende wakaishi Duniani , tutoe wawakilishi watupunguzie tatizo la ajira nchini, tutoa wawakilishi waende nje wakatuletee remittance. Wahaya tumechoka kukutana huko ulaya wenyewe Kwa wenyewe tunatamani na wagogo nao wakatembee ulaya wajifunze kuwa na misimamo na waache maisha yakujipendekeza hadi uchokwe.

Tusipokubali kutoka tukaamini katika sera ya JPM ya Tanzania ni tajiri ipo siku tutadanganywa na udongo wa mwezini tukauza rasilimali zetu. Hivi mnajua kwanini mikataba inakwenda kusainiwa nje, unajua kwanini Ndugai alitandikiwa red carpet china akazungukwa na wachina wakimpa huduma zaidi ya RAIS, ni kwa sababu walitaka kupitia Bunge wauziwe bandari ya Bagamoyo na alirejea akasifia kama limbukeni. Tunatakiwa tuwe na Mawaziri na makatibu wakuu waliotoka Duniani siyo waliotolewa jalalani. Tunataka Wabunge waliopita angalao nchi kadhaa siyo Watu wanajisifia kwamba wanaishi Dar wakitokea Mikoani. Mbunge kama Waitara anaishi Gongo la Mboto sijui Chanika atawaza sawasawa kuhusu biashara za Kimataifa? Tukubali kwamba ni muda Sasa wa kusambaa Kama tunataka kuwadhibiti watawala wasiuze nchi.

Nimetumia ukongwe wangu hapa JF kuwahimiza mtoke mkatafute Rizick, tunataka kuwa na Watu wenye Upeo wa akina Masele ambaye anaweza kupingana na spika huko South Kwa hoja Hadi spika akatumia wasio na akili bongo kumnyamazisha Kwa kivuli Cha utovu wa nidhamu. Tunataka vijana kama akina Nasari ambao pamoja na kupokwa fursa hawakukubali kubaki hapa walikwenda kwa Obama, tunataka wasomi kama akina Mhongo ambapo walipotumbuliwa walikwenda kupiga lecture south, tunataka vijana kama akina Lema ambao baada yakuona maisha yao yapo hatarini na wanapambana na wauaji waliamua kwenda nje, tunataka hoja zenye exposure kama za Lisu, tunataka wawekezaji kama MBOWE ambaye anarasimali Dubai sijui South ili kesho tukikwama huko tuwe na ndugu wakutupokea.

Tuachane na ushamba wakuiba fedha za nchi unazifungia chumbani au unachimba shimo unazifukia wakati ndugu zako hata nyumba Awana, unachukua fedha zetu unakwenda kuzificha bbenki Uswiz siku ukifa zinaozea huko huku sisi tunakufa njaa. Wahaya tunasema tutoke tukatafute tulete nyumbani tuendeleze nchi.

Kwa mwisho huu nategemea kusikia vijana wanamiminika Uhamiaji kutafuta pasipoti na Masauni anawaekeza vijana wake watoe pasipoti tukatembee , nategemea google vijana wanaitumia kusoma fursa nje na kuzifuatilia, nategemea website za mashirika ya Kimataifa zinavamiwa na watanzania wasaka fursa, nategemea mabalozi wetu akina Togolani waacha kutumia tweeter kuwa motivational speeker Badala yake wanatumia tweeter kutupa update za fursa za elimu na kazi.

Tunategemea mabalozi wetu wanalinda Watanzania bila kujali wametuhumiwa vipi na wakirejeshwa nchini Kwa wale watovu wa nidhamu basi Sheria za kuwashuguulikia zinatungwa badala ya kuwazuia Watanzania wengi kwenda nje kisa Binti mmoja huko Oman kawa mistreated.
Wakina Crylo walikwenda Ulaya 1950+ sisi Leo tunashindwa Nini?

Njooni huku sisi Wahaya tutawaonyesha njia.
 
Nilichoka tu kusikia umekufa then ukarudi JF, basi ndio nikaamini kuwa JF Kila kitu kinawezekana....yaani achilia mbali kuwa Kila mwana JF ana maisha mazuri kumbe pia baadhi Wana uwezo wa kufa na kufufuka. Happy Sabbath
 
Aiseee umenena mengi Sana mazuri ila Kwa sababu Mimi ni Mzee wa ramli chonganishi nasemaje

#Wagogommepigwadongohuku
#Mzeewajalalani
#Kimbungajobomzeewagalilaya

Nadanganya wadau?
😁😁😁😁
 
Kuna kakijana kameniuliza mwaka 2016 masaki palikuwa na viwanja? Naomba kumjibu kwamba hata Leo viwanja vipo ni pesa Yako tu? Hata kariakoo viwanja vipo wewe TU useme unatamani kubadiliasha kilicho juu ya ardhi uweke Nini..Sijui unanielewa?

Kuna anayesema alisikia nimekufa, Nadhani ukifa uwezi kuandika Ila ukiugua unaweza kuacha wosia. Sijui nimeeleweka

Kuna amesema nimewapiga wagogo madongo, hapana nataka kusema nikiwa Waziri nitamtumikia mwananchi na nikiwa spika ntamtumikia mwananchi sutatamani kukaa nyuma ya mkuu wa nchi masaa 24 ,kazi zangu nitafanya muda gani.

Dhima ya Uzi huu nikuanzisha kampeni ya TUKATEMBEE NJE TUJIONEE MAENDELEO YALIPO, ITATUSAIDIA KUACHA KUSHANGILIA DARAJA LA UBUNGO NA TAZARA KWENYE VYOMBO VYA HABARI,UKIELIMIKA UKATAMBUA DUNIANI MIUNDOMBINU IPO VIPI UTAONA HAYA KAMA MADARAJA TU NA UTOTHUBUTU KUTAMKA KWA KIINGEREZA.

JUZI NIMESIKIA KUNA DARAJA HUKO KIJIJI MBEZI LUIS NIKASHTUKA, KWAMBA WAKATI WANAJENGA BARABARA DARAJA HATUKULIONA? WAKANDARASI NA WATU WA TANROADS KATEMBEENI DUNIANI MWACHE KUTUTIA HASARA NA AIBU.
 
Nimejitahidi kusoma mpaka mwisho na ni ukweli mtupu atakae elewa na aelewa
Kutoka na kutembea katika mataifa mengine ni elimu tosha
Kweli mtu anapiga hela au tuache kuiba hata hela za halali unashindwa hata kupanga baada ya kila miaka 2 ukaenda kuburudika nje na kujifunza mengi
Kweli waliosafiri sana huwa na maendeleo kuliko waliojifungia ndani bila kujua kinachoendelea duniani


Ndio maana kina v8 wataishia kuonyesha sura za huruma badala ya kufungua viwanda watasubiri wapate tena vyeo serikalini shame

Hebu Wahaya na wachaga wapeni darsa hawa watu waliorogwa kuwa siasa eti iko kwenye damu na akitolewa huko au kufukuzwa kama paka mwizi hawezi hata kufungua biashara eti anaona aibu

Kuna watu wanaishi kwa kutaka kuonekana kwa hiyo holiday anaona ni kupoteza mda bora akae tu
 
"in short sikuwahi kuwa na akili sana ila nikifanya mtihani nafaulu"

Nimebaki natafakari hii kauli .....
 
Back
Top Bottom