Nimesahau mzigo ndani ya basi

Nimesahau mzigo ndani ya basi

Nuksi huanzia kwenye mambo kama haya
Watu mna viimani imani vya ajabu sana. Eti nuksi, hv unajua yanayofanyikaga humo kwny mabasi usiku yakiwa yamepark? Skia,kama kweli kuna ktu knaitwa nuksi basi amini kwamba mabas yote yana nuksi,,,,kwny mabasi madem wanabanduliwa sana hasa hasa wale madem wageni kutoka mikoani wasiokua na mwenyeji
 
Usikae mbali na vitu kama pc hata kama unaweka kwenye sehemu za kuwekea mizigo ila pendelea kubaki na begi la pc yako kamwe.


"kusahau begi langu lenye computer na vitu vingine"



Narudi nyuma kidogo, ni kuwa baada ya kujua nimesahau begi nilipiga zile namba za simu za kwenye tiketi kama nne ndipo nilipompata muhusika kwani wengi walisema wameshaacha kazi kampuni ile.

"Muhusika alipokuja mida kama ya saa kumi tukaenda kwenye bus na kukuta dereva kalala kwenye bus na akajibu kupitia dirishani kuwa hajaona hilo begi"



Huenda huyu mhusika alifanya mchongo coz pc kama hizo si chini ya 300 000

Sent from my SM-A125F using JamiiForums mobile app
Kabisa mkuu
 
Sure,pia siku hizi kuna cloud service nyingi tena nyingine ni free kwa kiasi flani cha data,na unaweza kuziaccess data zako ukiwa papote,hizi ni njia salama za kuhifadhi data zako hasa ambazo ni za muhimu.
Kweli mkuu sema zingine unakuta mi kubwa mno.
 
Sure,pia siku hizi kuna cloud service nyingi tena nyingine ni free kwa kiasi flani cha data,na unaweza kuziaccess data zako ukiwa papote,hizi ni njia salama za kuhifadhi data zako hasa ambazo ni za muhimu.
Apart from Google drive, ni cloud storage gan nyngne nzuri kusave text?. Mana huku drive ukitaka kusev text fulan n lazma uwe na google word. Sasa kama smu ina storage ndogo ni changamoto asee
 
Mkuu nimemtafuta mpaka mmiliki wa Bus hizo lakini mpaka leo bila bila. Ni kama hawataki mmiliki kujui hii ishu. Mtu wa mwisho ambaye ni wakala yuko Dar akasema mmiliki ni mgonjwa hivyo hawezi ongea na simu, nikamwomba anitumid namba nijaribu bahati yangu lakini akakataa na kuishia kusema ni uzembe wangu
Hata Mimi nshawahi kusahau mizigo Mara nyingi tu kwenye mabus Cha kwanza napiga namba ya wakala aliyenikatia tiket namuomba namba ya konda au dereva !! Afu wao ndio nawaambia mzigo wangu uko sehem gani na ukoje !! Naukuta kwao
 
Pole kwa usahaulifu, kupotea, kusahau na kuibiwa ni jambo ambalo hutokea pasipo kutarajia (accident). Kama umefanya juhudi zote hizo na bado hujafanikiwa nikushauri tu jifunze kuachilia na kuendelea na maisha mengine.
 
Habari wakuu.

Moja kwa moja kwenye mada, Jumapili iliyopita ya tarehe 05/06/2022 mida kama ya saa 1 usiku kuelekea saa mbili nikiwa natoka Dar kwenda Morogoro ndani ya bus mali ya kampuni ya Frester nikaamua kushukia Chalinze na kusahau begi langu lenye computer na vitu vingine. Nikatafuta usafiri mwingine kwenda Moro ili kufatilia begi langu lakini mpaka nafika Moro nikakuta bus limefika muda mrefu sana na abiria wote wameshashuka na bus limepaki kimya kabisa.

Ikabidi niende ofisini kuulizia maana ilikiwa usiku tayari mida kama ya saa saba. Ofisini sikukuta mtu zaidi ya abiria waliolala wakisubiri kusafiri kesho yake. Narudi nyuma kidogo, ni kuwa baada ya kujua nimesahau begi nilipiga zile namba za simu za kwenye tiketi kama nne ndipo nilipompata muhusika kwani wengi walisema wameshaacha kazi kampuni ile.

Muhusika alipokuja mida kama ya saa kumi tukaenda kwenye bus na kukuta dereva kalala kwenye bus na akajibu kupitia dirishani kuwa hajaona hilo begi. Nikapata wazo la kwenda Polis, nikaja na Polis wa kike na dereva akafungua mlango tukaingia ndani kukagua, kweli hakukuwa na begi ila mkoba tu wa kike uliosahaulika pamoja na demu wa dereva kumbe walilala humo.

Hisia zangu zinaniambia kuwa dereva, demu wake na kondakta ndiyo wamechukua mbegi langu. Naombeni msaada wa kipi cha kufanya kupata begi langu kwani ni muhimu sana na niko tayari kwa njia yoyote ile na kulipa gharama.

Ikumbukwe pia kuwa mzigo wa ndani ni dhamana yako/yangu.
Fafanua kidogo uamuzi wa ghafla kushuka Chalinze ulitokana na nini?
 
Apart from Google drive, ni cloud storage gan nyngne nzuri kusave text?. Mana huku drive ukitaka kusev text fulan n lazma uwe na google word. Sasa kama smu ina storage ndogo ni changamoto asee
ukiwa na window 10 au 11 activate one drive inakuwepo ila ipo off, ukisave file kwenye my documents file linakuwa uploaded wkt huo huo au mda tu pc ikiwa kwenye net itapandisha file.
 
Pole kwa usahaulifu, kupotea, kusahau na kuibiwa ni jambo ambalo hutokea pasipo kutarajia (accident). Kama umefanya juhudi zote hizo na bado hujafanikiwa nikushauri tu jifunze kuachilia na kuendelea na maisha mengine.
Sawa mkuu sina jinsi zaidi ya kukubali matokeo
 
Kweli mkuu. Ila nimepata hasara sana. Kwani nina project za watu wengi na wengine walishalipa pesa zao. Sijui hata nasema/nafanya nini.
Pole sana aisee, ila jifunze kuwa na backup/external hard drive kuepukana na hiyo changamoto
 
Kikubwa begi lilishuka kabla yako, waliiwahi laptop.

Hali kama hii usitegemee kupata chochote.

Ripoti polisi upewe ripoti ya kukuwezesha kutengeneza vitambulisho vingine.

Mzigo mmoja na unausahau huo huo kwenye gari.

Pole mwanangu
Huna uhakika na hilo, hasa kwa kuwa mwenye mzigo kasema alipanda Bus akiwa mtu wa pili. Wezi wengi ili waibe lazima wamjue mwenye begi, hawawezi kamwe kuiba blindly. Ndiyo maana hata mimi nikiweka kibegi changu kwenye keria ya Bus naweka upande wa pili na sitaligusa, mimi napiga jicho tuu. Kiufupi begi limeibiwa stend Msamvu hapo..
 
Mtoa mada anasema alipiga namba za kwenye tiketi akakuta wengi washaacha kazi hiyo kampuni Mimi nijuavyo kwenye tiketi hua wanaweka namba za mmiliki wa bus au ofisi kiasi angepiga kwa muhusika begi lake ningepatikana
Daah ila hiyo kampeni iko very local aise.. Kuna siku nilitoka Mbeya kwenda Iringa na Shabiby Bus inayokwenda Dodoma.. Wao kila abiria ukikata tiketi wanaandika namba yako. Sasa baada ya mimi kushuka Iringa baadae nikapigiwa simu kwamba je sijashuka na begi ambalo siyo langu? Kuna abiria wameexchange mabegi (yaani mtu kachukua begi si lake). Nikawaambia no nimeshuka na la kwangu, so kiukweli hawa jamaa niliwaona wako very organized kwa sababu waliweza ku trace abiria wao.
 
Huna uhakika na hilo, hasa kwa kuwa mwenye mzigo kasema alipanda Bus akiwa mtu wa pili. Wezi wengi ili waibe lazima wamjue mwenye begi, hawawezi kamwe kuiba blindly. Ndiyo maana hata mimi nikiweka kibegi changu kwenye keria ya Bus naweka upande wa pili na sitaligusa, mimi napiga jicho tuu. Kiufupi begi limeibiwa stend Msamvu hapo..
Kweli mkuu, mwenye nahisia hizo kwani kwa abiria kuiba ni kazi sana mana hajui mzigo ni wanani
 
Computer/laptop, simu, vitambulisho, kadi za Benki, nk,
Unakuwanavyo bega kwa bega,
i.e, ukikaa viko mapajani, ukiamka viko begani(bila shaka ndani ya begi).
Kamwe usiweke hata ndani ya sanduku. Kama kupotea viwe detached forcebly from your body(unyang'anywe kwa nguvu)
ndio mimi siachag bag langu...
 
Habari wakuu.

Moja kwa moja kwenye mada, Jumapili iliyopita ya tarehe 05/06/2022 mida kama ya saa 1 usiku kuelekea saa mbili nikiwa natoka Dar kwenda Morogoro ndani ya bus mali ya kampuni ya Frester nikaamua kushukia Chalinze na kusahau begi langu lenye computer na vitu vingine. Nikatafuta usafiri mwingine kwenda Moro ili kufatilia begi langu lakini mpaka nafika Moro nikakuta bus limefika muda mrefu sana na abiria wote wameshashuka na bus limepaki kimya kabisa.

Ikabidi niende ofisini kuulizia maana ilikiwa usiku tayari mida kama ya saa saba. Ofisini sikukuta mtu zaidi ya abiria waliolala wakisubiri kusafiri kesho yake. Narudi nyuma kidogo, ni kuwa baada ya kujua nimesahau begi nilipiga zile namba za simu za kwenye tiketi kama nne ndipo nilipompata muhusika kwani wengi walisema wameshaacha kazi kampuni ile.

Muhusika alipokuja mida kama ya saa kumi tukaenda kwenye bus na kukuta dereva kalala kwenye bus na akajibu kupitia dirishani kuwa hajaona hilo begi. Nikapata wazo la kwenda Polis, nikaja na Polis wa kike na dereva akafungua mlango tukaingia ndani kukagua, kweli hakukuwa na begi ila mkoba tu wa kike uliosahaulika pamoja na demu wa dereva kumbe walilala humo.

Hisia zangu zinaniambia kuwa dereva, demu wake na kondakta ndiyo wamechukua mbegi langu. Naombeni msaada wa kipi cha kufanya kupata begi langu kwani ni muhimu sana na niko tayari kwa njia yoyote ile na kulipa gharama.

Ikumbukwe pia kuwa mzigo wa ndani ni dhamana yako/yangu.
Uliusahau kivipi?
 
Back
Top Bottom