Nimesahau mzigo ndani ya basi

Kwenye basi mzigo unaoingia nao ndani ni dhamana yako isipokua ule wa kwenye buti ndio dhamana yao, unashukaje unasahau begi kwenye gari? Kama uliweka kwenye staff carrier kwa nini usijiandae na uandae mzigo ndio ushuke? Imekula kwako
 
Huyo dereva na konda unawaonea tu mwaisa.

Na dereva umemchongea kusema amelala na demu humo.

Sijui ni hasira za laptop. Ukute na wewe ulikuwa na kidemu kikakuchanganya.

🤭🤭🤣🤣
 
Sio rahisi mtu kuchukua begi ambalo hamjui muhusika wake ni nani!
Begi lako itakua lilichukuliwa mwishoni kabisa mwa safari baada ya abiria wote kushuka na begi lako kubaki peke yake,uchunguzi wa Polisi uanzie hapo.
Kabisa mkuu, maana wakati wa kupanda mimi nilikuwa abiria kama wa pili kupanda. Ndiyo maana siamini kuwa abiria ndiye kaiba hilo begi
 
Kwanini uliposhuka tu chalinze na kugundua umesahau begi hukufanya taratibu ya kuwasiliana na wakala wa frester hapo chalinze akupe mawasiliano ya hilo basi lao lililoelekea Morogoro wakuangalizie begi lako? Pole huna wa kumlaumu ila ww mwenyewe
Mkuu nilifanya hivyo ila kila namba niliyopiga muhusika alisema ameshaacha kazi kwenye hiyo kampuni. Mwisho nilimpata muhusika akasema yuko mbali kidogo.
 
angepiga simu mapema ingesaidia sana...!! ila kwenda na abiria washashuka hapo ni ngumu mno na alielibeba amedhamiria kuliiba
Kweli mkuu, lakini nilipiga simu kwa namba karibu zote bila mafanikio. Maana nililuwa na tiketi na kwenye tiketi kuna namba zao
 
Back
Top Bottom