Setfree
JF-Expert Member
- Dec 25, 2024
- 5,527
- 7,121
Kama kawa, nimekuwa nikiwaletea habari za kweli kabisa, bila kuchanganya hata tone la uongo. Leo tena napenda kuwahabarisha kuwa jana, ghafla tu, nilipata maumivu makali sana katika sikio langu la kushoto. Ni maumivu makali yaliyoenea mpaka upande wa juu wa kichwa changu. Kama hiyo haitoshi, nilihisi pia maumivu makali hata wakati wa kutafuna na kumeza chakula.
Dalili za ugonjwa huo zinafanana na za ugonjwa wa Otitis interna (inner ear infection / labyrinthitis).
Mimi, nikiugua, kimbilio langu la kwanza ni Yesu, kwakuwa uponyaji wa Yesu ni free of charge na mara nyingi ni instant healing. Mtu akikuambia utoe pesa kwanza ndio akuombee, mkimbie haraka, huyo ni tapeli mkubwa.
Hivyo nilifanya kama Yesu alivyoagiza: niliweka mkono wangu sehemu inayouma, nikakemea ugonjwa huo na kuuamuru utoke kwa Jina la Yesu. Niliendelea kumuomba Mungu aniponye na kuahidi kwamba nikipona, nitawashuhudia watu muujiza huo mkubwa.
Hivi ninavyoandika uzi huu, sisikii hata chembe ya maumivu. Hakika kuokoka na kuishi na Yesu ni kutamu.
Dalili za ugonjwa huo zinafanana na za ugonjwa wa Otitis interna (inner ear infection / labyrinthitis).
Mimi, nikiugua, kimbilio langu la kwanza ni Yesu, kwakuwa uponyaji wa Yesu ni free of charge na mara nyingi ni instant healing. Mtu akikuambia utoe pesa kwanza ndio akuombee, mkimbie haraka, huyo ni tapeli mkubwa.
Hivyo nilifanya kama Yesu alivyoagiza: niliweka mkono wangu sehemu inayouma, nikakemea ugonjwa huo na kuuamuru utoke kwa Jina la Yesu. Niliendelea kumuomba Mungu aniponye na kuahidi kwamba nikipona, nitawashuhudia watu muujiza huo mkubwa.
Hivi ninavyoandika uzi huu, sisikii hata chembe ya maumivu. Hakika kuokoka na kuishi na Yesu ni kutamu.