Unajua Slim kuwa Mstaarabu,yaani Post ilikuwa nzuri sana na ndio maana watu walikupa Like wengi.
Ila hii ndio imeharibu na hata mie baada ya kuisoma post nilipenda ulichopost then kushuka chini ukaonyesha Dharau hii ndio umeniboa ile mbaya.
Kuna vitu vya kujifunza kwenye soko la Ajira,kwanza Tambua aliekupa ajira hiyo ni mungu,na mungu anapokupa njia ya ajira ni kutaka kujua utakuwa mtu wa namna gani kwa wenzio na kwake.
Watu wapekupa hongera nyingi bila kinyongo,then wewe umewarejesha kinyume chake.
Tambua kwamba kwa Soko la Ajira kwenye IT post Diploma Level ni la muda mfupi,la sivyo ukubali kuwa under paid.
Unaweza kukuta wewe mwenye Diploma unafanyakazi Miaka Mitano,inakuwa sawa na Mwenye Degree aliefanya kazi mwaka Mmoja na nusu au Mwaka mmoja tu.
Sasa hilo nalo ulitambue,kuwashinda wenye Degree kwenye Interview sio kigezo cha umahiri wako.
Interviewers wengi wanaangalia position husika kama inahitaji mtu wa namna gani kwa muda ule,na wakiona ni mtu wa kawaida basi ndio wanashuka hapo kwa nia ya kwamba hata mshahara ni mdogo pia.
Kuwa muungwana sana kwa Mungu aliekupa Ajira,usipende kumuudhi Mungu,anaweza hata kesho akaichukua nafasi hiyo kwa kukupa maradhi,ajali,au hata kuonyesha ufalme wake kwa kuachishwa kazi kwa namna ya uwezo wake Mungu.
Maana Mungu alitegemea kwamba utamshukuru na kufurahia na sie wenzio kwa njia njema,lakini sio Kubeza wenzio kwa namna hiyo.
Hivi unajua kwanini Mungu aliingiza ufalme wake ukapata kazi na wenye Degree wakabaki?basi pia anaweza kugeuza matokeo pia,maana ufalme na vyote vilivyomo Duniani ni mali yake.
Ulimuomba sana mungu kwa muda mrefu akakupa,sasa hayo ndio majibu unayomrejeshea mungu baada ya kukupa.Jua kwamba hao unawoaponda wenye Degree mungu aliwaona ila aliingiza ufalme kwako ili kukukubalia maombi yako.
Mungu hufurahia sana kulipwa wema na mungu hupenda sana huwa karibu sana na wanomshukuru kwa alichowajaalia na hupenda sana kwa wale wanaoamini kwamba yeye anaweza yote,muhim tu nikumuomba na kumkabidhi shida zako kwake nakufuata maamrisho yake,na mwisho yeye atakuonyesha ufalme wake na uwezo,na pia nguvu zake kwa wale wenye Moyo wa Subira.
Tambua kwamba Mtu anaweza kumuomba Mungu hadi miaka 5 au hadi kumi,huo ni mfano,na kisha mungu akampa anachotaka.Hapo ni kwamba mungu anataka kuona kwamba Je huyu atanikana kama mie sipo na sina uwezo?Sasa wale wavumilivu ndio huona faraja ya kuvumilia kwao.Na wasio wavumilivu ndio huishia kwa Wanganga,badla ya kumpa mungu kuwapa muda anaotaka yeye. Na huyo huyo Mungu ndio huweza kufanya uwezo wake ukamuomba leo mwezi ujao au kesho ukapata,na lengo ni lile lile,je utajifanya wewe ndio juhudi zako peke yako zimekupa ulichotaka na sio yeye?Hapa ndio upo wewe
Na nafasi kama hizo ndio mungu huweza kufanya lake kwa kurejesha hali na kukufanya urudi chini,na hapa duniani wamepita wengi sana ambao leo tunawaona hali zao ni mbaya sana kimaisha,baada ya mungu kuwapa na wao kuonyesha Jeuri kwa wenzio na kwa Mungu Pia.
Mungu husamehe,mie nimekusamehe kwa Dharau hiyo,ila kila mtu hujiombea mwenyewe.