Nimenunua laptop Amazon.com

Nimenunua laptop Amazon.com

Kang

JF-Expert Member
Joined
Jun 24, 2008
Posts
5,692
Reaction score
2,576
Nimefanikiwa kununua laptop kutoka Amazon.com kwa kutumia hatua zifuatazo natumaini itawasaidia wengine.

Amazon hawatumi bidhaa nyingi Tanzania hasa electronics so unahitaji kampuni ya shipping itakayokutumia vitu vyako kutoka US kuja bongo kuna kampuni nyingi zinafanya hili mimi nilitumia USGoBuy.com kwa kuwa ndo niliona ina bei ndogo na unaweza kutumia USPS (Posta ya Marekani) sio lazima utumie DHL/UPS ambazo zina gharama zaidi.

Utahitaji kadi ya Visa/MasterCard inayofanya kazi mtandaoni.

Hatua
  1. Nenda USGOBuy.com na fungua account hauhitaji kulipa kwa sasa.
  2. Watakupa address ya marekani hii ndo utaitumia wakati unanunua Amazon.
  3. Nenda Amazon weka vitu unavyotaka kununua kwenye kikapu, lipia kwa kutumia kadi kisha wakati wa kuweka address weka address uliyopewa na USGoBuy ya marekani, shipping ni bure Amazon->USGoBuy.
  4. Unaweza kununua duka lolote sio Amazon tu kisha ukatuma vitu vyote address yako ya USGoBuy wao watavishika kwa hadi siku 60 bila gharama na wanaweza kuviunga kwenye mzigo mmoja na kupunguza size weight ya mzigo kwa kutupa mabox yasiyohitajika.
  5. Subiri vitu vyako vifike USGoBuy kutoka Amazon.
  6. Vitu vikifika utataarifiwa na utaweza kuona kupitia tovuti ya USGoBuy. Pia kuna huduma ya kupigiwa picha hii ina gharama $5.
  7. Ukiwa tayari kuvituma vitu kuja bongo utajaza anuani yako ya TZ pamoja na kampuni unayotaka kutumia kuna DHL, UPS, USPS.
  8. Watakuhesabia gharama kutokana na uzito na size ya mzigo.
  9. Unaweza kulipia kwa kadi au PayPal.
  10. USPS ndo posta ya Marekani na ndio inagharama nafuu na nadhani ndo pekee wanaokubali PO Box.
  11. Jihadhari na kampuni za DHL/UPS hawa wanakuwa na fee za ziada kuukomboa mzigo ukifika bongo juu ya kodi "Shiping and Handling charges".
  12. Ukichagua USPS Priority mzigo unakuja kwa EMS so una tracking all the way.
  13. USGoBuy watakuomba ujaze gharama ya mizigo yako, hii ndo itaandikwa juu ya boxi, watakuuliza kama unataka original invoice za amazon ziwekwe kwenye boxi au waitupe.
  14. Mzigo ukifika bongo utapigwa kwanza 1,500 gharama za posta.
  15. Halafu kuna VAT 18% na kodi ya reli 1.5%
  16. Kwa laptop ndo hizo tu kodi, kwa vitu vingine kuna kodi zaidi ambazo sizijui kwa bahati mbaya.
  17. Pale posta wanapokokotoa kodi wanataka ile original invoice ya Amazon otherwise wanazama mtandaoni wanaanza kutafuta bei wenyewe, maelewano juu yako.
Kwa ujumla imechukua siku 10 tangu kuagiza Amazon hadi mzigo kufika bongo.
 
Hongera mkuu.


Kuna ile nadhalia imesambaa sana kuwa Amazon.com bidhaa zao huwa ni ghali japo zina ubora mdogo kuna ukweli juu ya hili?
 
Hongera mkuu.


Kuna ile nadhalia imesambaa sana kuwa Amazon.com bidhaa zao huwa ni ghali japo zina ubora mdogo kuna ukweli juu ya hili?

Hapana, Amazon wanauza hasa bidhaa za makampuni mengine so ubora unategemea na kampuni unaweza kununua Apple au Samsung Amazon bei zao ni nzuri kwa Marekani tatizo ni shiping bongo.
Kuna vitu vingi ambavyo ni cheaper AliExpress lakini AliExpress kuna vitu havipatikani hasa vya brand kubwa.
 
Ok nataka kujua hyo laptop uliyonunua Amazon mpka kufika hapa gharama zake zikoje ukilinganisha na kama ungenunulia hapahapa

Tatizo ni kwamba laptop niliyonunua bongo haipatikani, ila shipping ilikuwa $130 kwa laptop nzito kidogo 6kg ndani ya box so unaweza kufanya mahesabu kama unachotaka kununua bongo kipo, price + shipping + kodi.
 
Hapana, Amazon wanauza hasa bidhaa za makampuni mengine so ubora unategemea na kampuni unaweza kununua Apple au Samsung Amazon bei zao ni nzuri kwa Marekani tatizo ni shiping bongo.
Kuna vitu vingi ambavyo ni cheaper AliExpress lakini AliExpress kuna vitu havipatikani hasa vya brand kubwa.
Nimekuelewa mkuu
 
Tatizo ni kwamba laptop niliyonunua bongo haipatikani, ila shipping ilikuwa $130 kwa laptop nzito kidogo 6kg ndani ya box so unaweza kufanya mahesabu kama unachotaka kununua bongo kipo, price + shipping + kodi.
Laptop 6kg mkuu? Inafaa kupakata kweli? Kg 6 uzito wake ni sawa mtu amekupa furushi castle milk kubwa 12 au safari ndogo 16!
 
Hiyo nunua AliExpress.
Shida ya aliexpress na alibaba inasumbua kwenye njia ya kulipia kwani weng wanataka TT,pili nmehisi kuna matapeli wengi kwani tangu nijiunge napata matangazo na oda za vitu toka kwa wauzaji ambao sijafanya oda kwao,tatu wengi wao wanatumia majina ya mmilikiwa wa huo mtandao Jack Ma
 
Shida ya aliexpress na alibaba inasumbua kwenye njia ya kulipia kwani weng wanataka TT,pili nmehisi kuna matapeli wengi kwani tangu nijiunge napata matangazo na oda za vitu toka kwa wauzaji ambao sijafanya oda kwao,tatu wengi wao wanatumia majina ya mmilikiwa wa huo mtandao Jack Ma

AliExpress wanapokea kadi za kawaid, payment ni through aliexpress wenyewe so iko salama hakuna muuzaji anayepata details zako.

Nununua kupitia site only usideal na mtu kwenye email.

Angalia idadi ya orders na reviews AliExpress utamjua muuzaji mzuri, sijawahi kupata shida, nimeagiza vitu zaidi ya mara 20 now kuanzia camera, laptop hadi soksi!

Usiende alibaba ukiwa logged in Aliexpress au alibaba otherwise wanapata email yako, fungua incognito tab au private tab kabla ya kwenda. Ali Express hawatumi email na muuzaji hapati email yako, mawasiliano ni through AliExpress only.
 
Back
Top Bottom