Mimi kinachoniboa sio bill ila ni ile kukosa nafasi ya kuongea mambo yetu, sasa unapokuja na mtu inamaana hutaki tuongee mambo yanayotuhusu sisi kama wapenzi, au unabana nisikutongoze.
Na ukiona dem anakufanyia hizo mambo ujue huwezi kumpata, atakuzungusha huku anakula vyako, dawa ni kujitoa mapema.
Kwa hiyo nikiacha kulipa bill ni kwa sababu nimeona sina changu na siwezi kuliwa bure (naliwa bila kula), ila kama ni dem wangu na vyombo napataga sioni tatizo yeye kuja na rafiki yake japo sio kila mara.