Very correct, mi nina stori ila si kama ya jamaa ila yataka kufanana nayo. Manzi angu niko naye kwenye mahusiano almost 8 months hadi sasa. Sasa kitu ambacho nimekuja kuki notice kwa wadada au wachumba hawa, ukimzoeza kuwa unaosha vyombo na yeye yupo kakaa kuna siku atakuja kufoka kwanini hujaosha vyombo, hata kufua na majukumu mengine ambayo tumegawana kama Mama na Baba kwenye jamii yetu kulingana na nafasi zetu.
Mie huwa na kiutamaduni cha kufua nguo zangu na zake kama kuna nguo aliacha ghetto chafu anakuta nimezifua., sasa kuna siku yeye alipofika ghetto ile night akakuta sijafua nguo zake kama alivyozoea kukuta kwa sababu ya ubize wa kazi. Basi mdada alichukua nguo zake pekee ake akafua nikamuuliza kwani ukifua na zangu utapungukiwa na nini!!? Basi hakukubali kunisaidia kufua hizo nguo daah ila baadae sijui akili ikamjia akaenda kabatini akachukua nguo zangu akazifua..! Na hiyo ni baadae jioni kabisa mie sikutaka tuzozane kwa sababu ya kufua nguo