Fursakibao
JF-Expert Member
- Dec 12, 2017
- 6,676
- 11,110
Habari za usiku huu wadau.
Nina rafiki yangu tumeshibana sana, siri zaje zangu zangu zake.
Sasa huyu mshikaji wangu ana demu wake wako kwenye mahusiano mwezi wa 8 sasa. Mwanzoni mapenzi yalianza vizuri baadae mambo yakabadilika. Kutokana na long distance kati yao kila kukicha ugomvi hauishi.
Kama rafiki wa karibu nilijitoa kabisa maana sikutaka kuwa mpatanishi, ika nyuma ya pazia nilikuwa mshauri wa rafiki yangu.
Kwa kifupi mapenzi yao yalikuwa yanabadilika kila wiki, wanaweza kugomvana ukajua hawa basi tena, kesho yake mapenzi yananoga. Mwisho wa siku walikaa wakashauriana waishi pamoja kwa muda wa mwezi na nusu ili waweze kusomana tabia.
Ndani ya mwezi moja wa kuishi pamoja, demu aliugua sana kwa muda wa wiki na zaidi hivyo jamaa akawa ndio mpishi na kufanya kazi zingine.
Baada ya demu kupona alimshukuru sana jamaa na akasema huyo ndio Mume aliyekuwa akimuomba Mungu ampatie. Hivyo basi walikuwa wameamua wiki ijayo amvalishe Pete ya uchumba.
Leo asubuhi wameamka vizuri, jamaa akampeleka saloon akalipa kama laki, wakarudi nyumbani, walipofika nyumbani demu akamwambia jamaa akatupe takataka, jamaa akamwambia amechoka, basi demu ketema povu si la nchi hii.
Baada ya kutema povu demu kaingia jikoni kapika, baada ya kumaliza kapakua kala bika kumpa jamaa msosi.
Jamaa hakusema kitu akapiga kimya. Sasa anafikiria kuhairisha mipango ya pete ameniuliza mi nikamwambia huyo demu hafai.
Ungekuwa wewe ndio jamaa ungefanya je? Au kama wewe ndio mimi ungempa ushauri gani?
Nina rafiki yangu tumeshibana sana, siri zaje zangu zangu zake.
Sasa huyu mshikaji wangu ana demu wake wako kwenye mahusiano mwezi wa 8 sasa. Mwanzoni mapenzi yalianza vizuri baadae mambo yakabadilika. Kutokana na long distance kati yao kila kukicha ugomvi hauishi.
Kama rafiki wa karibu nilijitoa kabisa maana sikutaka kuwa mpatanishi, ika nyuma ya pazia nilikuwa mshauri wa rafiki yangu.
Kwa kifupi mapenzi yao yalikuwa yanabadilika kila wiki, wanaweza kugomvana ukajua hawa basi tena, kesho yake mapenzi yananoga. Mwisho wa siku walikaa wakashauriana waishi pamoja kwa muda wa mwezi na nusu ili waweze kusomana tabia.
Ndani ya mwezi moja wa kuishi pamoja, demu aliugua sana kwa muda wa wiki na zaidi hivyo jamaa akawa ndio mpishi na kufanya kazi zingine.
Baada ya demu kupona alimshukuru sana jamaa na akasema huyo ndio Mume aliyekuwa akimuomba Mungu ampatie. Hivyo basi walikuwa wameamua wiki ijayo amvalishe Pete ya uchumba.
Leo asubuhi wameamka vizuri, jamaa akampeleka saloon akalipa kama laki, wakarudi nyumbani, walipofika nyumbani demu akamwambia jamaa akatupe takataka, jamaa akamwambia amechoka, basi demu ketema povu si la nchi hii.
Baada ya kutema povu demu kaingia jikoni kapika, baada ya kumaliza kapakua kala bika kumpa jamaa msosi.
Jamaa hakusema kitu akapiga kimya. Sasa anafikiria kuhairisha mipango ya pete ameniuliza mi nikamwambia huyo demu hafai.
Ungekuwa wewe ndio jamaa ungefanya je? Au kama wewe ndio mimi ungempa ushauri gani?