kibol
JF-Expert Member
- Apr 24, 2012
- 4,512
- 2,730
Kwanza) .pole sana mdogo wangu kwa yaliyokutokea..
pili) nenda kachek afya yako maana umeshapita kavu kavu..
tatu) usirudie tena kufanya haya uliyofanya,siku hizi mwanaume hasifiwi kwa uhuni..
nne) mchukue huyo binti uliempa mimba mkapime DNA ujue kama hiyo mimba ni ya kwako..kama itakuwa siyo yako hongera sana maana utapata nafuu..na kama itakuwa yako...
tano).kaa chini na mchumba wako umwambie ukweli kuwa ulitembea nje na umempa mimba binti mwingine,mwambie ukweli kuwa humpendi huyo binti na umweleze wazi unampango gani na huyo binti pamoja na mwanao,halafu msikilize atasemaje na atakupa condition zipi kama atakuwa tayari kukusamehe.CHUNGA sana condition atakayokupa mchumba wako isiwe ya kumtupa mwanao,maan utakuwa umempa adhabu mtoto asie na hatia na pia huwezi jua kama MUNGU atakupa mwingine au yapi yatakutokea mbele,vyovyote itakavyokuwa usikubali kutupa mtoto ingawa mama humpendi.
sita).kama mchumba akikubali kukusamehe mwite huyo binti mwenye mimba yako umueleze ukweli mbele ya mchumba wako na mpango ulionao juu ya mtoto,na kama mchumba akigoma kukusamehe basi usimkere maana ndio utakuwa mshahara wa dhambi zako..kaa chini subiri mtoto wako ulee..
nane).sikushauri kabisa kumuo huyo mama mtoto wako wala kuishi nae sababu ya mtoto maana ni afadhali mateso utakayompa kwa kukataa kuishi nae kuliko ukiishi nae halafu ukamtenda ndivyo sivyo.
mwisho).kuwa na msimamo na maisha yako,kubali malipo yanayokuja baada ya makosa uliyofanya,na ujifunze kutokea hapo,SIMAMA mdogo wangu na usonge mbele maana kukosea ni sehemu ya maisha ya mwanadamu...kila la kheri na cheers..
watu km nyinyi ndio mnafanya ili jukwaa linaonekana nila ma-great thinkers.bro keep it up,wewe ni think tank,ni vile tu natumia simu ningekugongea like.