Nimempa ujauzito mwanamke nisiyempenda!

Gardener

Member
Jun 8, 2011
37
8
Wakuu maji yamenifika shingoni,mwaka jana mwshoni,nlikutana na binti mmoja,mwanafunzi wa mwaka wa pili chuo kikuu kimoja dodoma,baada ya siku kadhaa,nikatembea nae,lakini sikuwa na mapenzi kwake,lakini yeye alinipenda sana,akanisumbua kwa muda mrefu,nikaamua kumweleza ukweli kuwa mimi nina mchumba,lakini yeye hakuridhika,siku moja akang'ang'ania kuja kwangu usiku,alipokuja kwa bahati mbaya siku hiyo akashika ujauzito,sasa anawasiliana na mpenzi wangu baada ya kuiba namba kwenye simu,na ameng'ang'ania anataka kuzaa na mimi,kweli sina mapenzi naye na ninamchukia sana kwa haya alotendea,kanitegea mimba akidhani ntamuoa,siwez kumpenda kamwe,jamani nisaidieni kunishauri.
 
Peleka message kwenye magazeti ya udaku utajibiwa, hapa si mahala pake.
Wakuu maji yamenifika shingoni,mwaka jana mwshoni,nlikutana na binti mmoja,mwanafunzi wa mwaka wa pili chuo kikuu kimoja dodoma,baada ya siku kadhaa,nikatembea nae,lakini sikuwa na mapenzi kwake,lakini yeye alinipenda sana,akanisumbua kwa muda mrefu,nikaamua kumweleza ukweli kuwa mimi nina mchumba,lakini yeye hakuridhika,siku moja akang'ang'ania kuja kwangu usiku,alipokuja kwa bahati mbaya siku hiyo akashika ujauzito,sasa anawasiliana na mpenzi wangu baada ya kuiba namba kwenye simu,na ameng'ang'ania anataka kuzaa na mimi,kweli sina mapenzi naye na ninamchukia sana kwa haya alotendea,kanitegea mimba akidhani ntamuoa,siwez kumpenda kamwe,jamani nisaidieni kunishauri.
 
Si umesema huwezi kumpenda kamwe!
Wewe una mchumba halafu unatembea na Mdada mwingine, sijui maana ya mchumba ni nini?
 
Hivi mbona hueleweki? Title na habari vitu viwli tofauti
 
Mtafute na mama yake pia umpe mimba, si wewe unajidai hodari?
 
Hiyo ndio faida ya kutembeza kidudu wako kwa kila mwanamke!! Ulitegemea nini baada ya kuingiza!! UKOME!!
 
hahaha wewe hukusoma mchezo...demu aking'ang'ania kuja kwako na kukupa mzigo kuwa chonjo. sasa la msingi ni kukubaliana na situation hii. huyo hawezi kukulazimisha umuoe lakini mwana ujiandae kwa vituko.
 
Pole ndugu yangu.. Jamani yaani mpaka ukakubali kufanya nae mapenzi bila kutumia kinga!! Ulimwaminije kama yuko salama kwanza? Tuwe waangalifu ndugu zangu.! Kuoa si lazima umuoe mtu ambaye humpendi lakini jua ya kwamba ameshatia doa uhusiano wako na huyo umpendae..
 
Kwanza) .pole sana mdogo wangu kwa yaliyokutokea..
pili) nenda kachek afya yako maana umeshapita kavu kavu..
tatu) usirudie tena kufanya haya uliyofanya,siku hizi mwanaume hasifiwi kwa uhuni..
nne) mchukue huyo binti uliempa mimba mkapime DNA ujue kama hiyo mimba ni ya kwako..kama itakuwa siyo yako hongera sana maana utapata nafuu..na kama itakuwa yako...
tano).kaa chini na mchumba wako umwambie ukweli kuwa ulitembea nje na umempa mimba binti mwingine,mwambie ukweli kuwa humpendi huyo binti na umweleze wazi unampango gani na huyo binti pamoja na mwanao,halafu msikilize atasemaje na atakupa condition zipi kama atakuwa tayari kukusamehe.CHUNGA sana condition atakayokupa mchumba wako isiwe ya kumtupa mwanao,maan utakuwa umempa adhabu mtoto asie na hatia na pia huwezi jua kama MUNGU atakupa mwingine au yapi yatakutokea mbele,vyovyote itakavyokuwa usikubali kutupa mtoto ingawa mama humpendi.
sita).kama mchumba akikubali kukusamehe mwite huyo binti mwenye mimba yako umueleze ukweli mbele ya mchumba wako na mpango ulionao juu ya mtoto,na kama mchumba akigoma kukusamehe basi usimkere maana ndio utakuwa mshahara wa dhambi zako..kaa chini subiri mtoto wako ulee..
nane).sikushauri kabisa kumuo huyo mama mtoto wako wala kuishi nae sababu ya mtoto maana ni afadhali mateso utakayompa kwa kukataa kuishi nae kuliko ukiishi nae halafu ukamtenda ndivyo sivyo.
mwisho).kuwa na msimamo na maisha yako,kubali malipo yanayokuja baada ya makosa uliyofanya,na ujifunze kutokea hapo,SIMAMA mdogo wangu na usonge mbele maana kukosea ni sehemu ya maisha ya mwanadamu...kila la kheri na cheers..
 
Unataka yeye akatoe hiyo mimba ok kama ulikuwa huna mpango naye kwa nini hukutumia kinga ..lea mimba yako mtunze mtoto uliyempenda na huyo mwenye mimba wana tofauti gani wote wanawake wapo sawa acha mawazo ya kitoto wewe mshukuru Mungu amekuambia ukwl angeenda kuitoa ingekuwa kama vp waoe wote kama una uwezo wa kutunza.
 
Wakuu maji yamenifika shingoni,mwaka jana mwshoni,nlikutana na binti mmoja,mwanafunzi wa mwaka wa pili chuo kikuu kimoja dodoma,baada ya siku kadhaa,nikatembea nae,lakini sikuwa na mapenzi kwake,lakini yeye alinipenda sana,akanisumbua kwa muda mrefu,nikaamua kumweleza ukweli kuwa mimi nina mchumba,lakini yeye hakuridhika,siku moja akang'ang'ania kuja kwangu usiku,alipokuja kwa bahati mbaya siku hiyo akashika ujauzito,sasa anawasiliana na mpenzi wangu baada ya kuiba namba kwenye simu,na ameng'ang'ania anataka kuzaa na mimi,kweli sina mapenzi naye na ninamchukia sana kwa haya alotendea,kanitegea mimba akidhani ntamuoa,siwez kumpenda kamwe,jamani nisaidieni kunishauri.

kumbe ule usemi wa kwamba "A man can sleep with 1000 women and love none among them" ni wa kweli dah inauma sana , huyo dada naye mayai yake yako juu juu kama ya samaki ya day 1 tu kadaka mpira ni noumer , chakufanya wee lea hiyo mimba akishajifungua utamchukua huyo mtoto umpelekee mamako amlee si wewe wa kwanza kwa hili pole kaka ,punguza kufunguafungua sana zipu
 
uAMUZI upo mkononi mwako.
kama unampenda OA.
Kama humtaki ...mfukuzie mbali.
kuzaa naye sio tiketi ya ndoa, kama kuzaa ingekuwa tiketi ya ndoa, mbona waengi wangefaidi.
 
JF haiishi vituko ! sasa broda ulitegemea nini... mbegu ya kiume ikikutana na yai kitu na box simple biology
 
Wakuu maji yamenifika shingoni,mwaka jana mwshoni,nlikutana na binti mmoja,mwanafunzi wa mwaka wa pili chuo kikuu kimoja dodoma,baada ya siku kadhaa,nikatembea nae,lakini sikuwa na mapenzi kwake,lakini yeye alinipenda sana,akanisumbua kwa muda mrefu,nikaamua kumweleza ukweli kuwa mimi nina mchumba,lakini yeye hakuridhika,siku moja akang'ang'ania kuja kwangu usiku,alipokuja kwa bahati mbaya siku hiyo akashika ujauzito,sasa anawasiliana na mpenzi wangu baada ya kuiba namba kwenye simu,na ameng'ang'ania anataka kuzaa na mimi,kweli sina mapenzi naye na ninamchukia sana kwa haya alotendea,kanitegea mimba akidhani ntamuoa,siwez kumpenda kamwe,jamani nisaidieni kunishauri.

Eti kakutegea mimba!? Hukujua kama ungeweza kutumia protection kuondoa uwezekano wa kumpa mimba? Ulipokuwa unakula uroda uliona raha sana, sasa unadai unamchukia!?...Pumbavu kabisa. Jiandae na pesa za matumizi ya kichanga kitarajiwa na mama yake.
 
Ulipokuwa unagawa dozi ulilazimishwa?acha kuongeza watoto wa mitaani, take u'r responsibility, halafu kuwa serious ana ujauzito na ananga'nga'nia anataka kuzaa nawe, acha contradictions
 
alipokuja kwa bahati mbaya siku hiyo akashika ujauzito,
ameng'ang'ania anataka kuzaa na mimi
Hapa mi sijakuelewa....!
Kauli zako zinapingana...sasa kama ameshashika mimba utakataaje kuzaa nae?
Si tayari mshapata mimba au mi sijakuelewa?
Halafu cha ajabu pamoja na gonjwa la UKIMWI kuwepo bado nashangaa unafanya mapezi bila kinga tena siku ya kwanza lol halafu huyo siku hiyo tu anakwambia kashika mimba...Angalia usijelea watoto wa mwenzako!
Take care ufanyayo halafu kuna vitu vya kuuliza vingine ni aibu!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom