naiman64
JF-Expert Member
- Nov 22, 2013
- 6,988
- 5,503
Wakuu,
Naomba mnisaidie kwa hili.
Nimempa mimba mdogo wa rafiki yangu kipenzi, namuambia aitoe hataki. sio kama sina uwezo wa kumuhudumia ila naogopa jinsi watu watakavyonichukulia kutokana na status yangu.
Naona aibu sana jamii inayonizunguuka ikija kufahamu hii habari. naombei mnisaidie wakuu nifanye nini kuondokana na aibu iliyo mbele yangu? Kuhusu kumpeda nampenda sana binti na nina mpago aje awe mama wa watoto wangu lakini sio kwa kuzaa nje ya ndoa.
Wakuu ebu nisaidieni katika hili, nimshauri vipi huyu mtoto akubaliane nami maana anakataa hataki kusikia kabisa habari hizo.
Hivi wewe mpuuzi huyo bint kwa sisi waafrika ni mdogo wako kabisa ukamdanganya na visenti uchwara vyako, ukamvulia nguo bila haya umemmimba, unaonaje aibu kwa jamii, hukuona aibu kumvulia nguo Leo unaionea aibu jamii!!? Wewe wewe Subiri huyo rafiki yako ajue, au mtoe kabla hajafa awe ameacha meseji ndio utaijua hiyo familia ikoje. Sina ushauri zaidi ya kuwaza kwa hasira kwamba ungekuwa jirani yangu ningekusagia hata chupa ufe.