Nimemkumbuka Dr. Slaa

Nimemkumbuka Dr. Slaa

Hungeweza kuona Dr. Slaa akiokoteza maneno ya kihuni ya humu mitandaoni kama vile "jiwe, mshamba, chatle" nk kisha unaenda kuyaandikia hoja kama afanyavyo Lisu na wafuasi wengine wa chadema!

Slaa alikuwa anaibua hoja mpaka system inatetemeka.
Sujui alikua anapata wapi data? Na huyu katibu wa sasa sijui anafanya nini ofisini?
 
Alinyimwa kugombea ubunge akiwa CCM akahamia CDM,kanyimwa kugombea uraisi akiwa CDM akahamia CCM. Kwa hiyo yeye haoni wengine kufaa kugombea bali yeye tu!?
Shida yake kubwa hana maamuzi, maamzi hutoka kitchen.
Sijawahi kuona Askofu msaliti kama huyu!! Yeye anakula bata baada ya kuuza mechi na wenzake wanauguza majeraha ya marisasi....
 
Nliacha kushabikia siasa mwaka 2015 sina chama mpaka sasa ila sifurahishwi na haya yanayofanywa na ccm

Nliona wanasiasa ni wale wale hasa baada ya kumpitisha lowasa agombee uraisi

Siwezi elezea ghadhabu nlyopata ya ule unafiki

Ila nkaapa siwezi shabikia ccm maisha

Ila neutral mind
aaah weee.
 
Nliacha kushabikia siasa mwaka 2015 sina chama mpaka sasa ila sifurahishwi na haya yanayofanywa na ccm

Nliona wanasiasa ni wale wale hasa baada ya kumpitisha lowasa agombee uraisi

Siwezi elezea ghadhabu nlyopata ya ule unafiki

Ila nkaapa siwezi shabikia ccm maisha

Ila neutral mind
vipi yanayoendelea kwa sasa? Slaa aliondoka sababu lowasa na saiz lowasa yupo ccm ambako slaa yupo unadhani atatoka? Leo katiba ya nchi si lolote si chochite
rip nyerere

 
Nami toka moyoni nimemkumbuka Dr Slaaa ndani ya upinzani wa sasa. Wakati mwingine hua nafikiri upinzani wa sasa wamerogwa kwani kazi yao kubwa ni kudandia dandia hoja nyepesinyepesi tu. Kila siku wanalalamika bila kuja na suluhu ya matatizo. Wanatafuta huruma ya walio madarakani.
"Nitakapo apishwa kuwa rais wa JMT, mwakipesile ukatafute nchi ya kwenda" maneno ya ukali na gadhabu ya Dr wilbrod Slaa wakati wa kufunga kampeni za uchaguzi wa mwaka 2010 pale jijini mbeya. Itakumbukwa kuwa mkuu wa mkoa wa mbeya kwa wakati huo John mwakipesile, alifanya kila aina ya figisu kuhakikisha Dr slaa hafanyi mkutano mbeya, kwanza umeme ulikatika jiji zima na pia polisi walikua wanachelewesha kuanza kwa mkutano ilihali mwisho wa kampeni ulikua saa kumi na mbili jioni. CCM walimuogopa Dr slaa, alikua na ufuasi mkubwa wa vijana waliokua wakitaka new regime

Nakumbuka nilikua kidato cha tano wilayani Rungwe mkoani mbeya, hivyo niliruka ukuta na masela na kusafiri mpaka mbeya mjini kumsikiliza Dr. Slaa was a presidential material, alikua anajua kuhutubia, anajua kujenga hoja, na msimamo mkali kwa vile anavyoamini. "Nikiwa rais elimu Bure toka chekechea mpaka chuo kikuu, nikiwa rais sitaki kumuona mtanzania anaishi nyumba ya tembe..." Rafiki yangu mmoja alikua afande pale mjini alininon'goneza "hakika hili jamaa hata mie natamani lichukue nchi".Hakika Dr slaa aliijua siasa.

Hata baada ya kuukosa uraisi dr slaa alipania kukijenga chama mpaka kwenye ngazi ya shina, CHADEMA ilipata uungwaji mkono mkubwa sana kipindi hiki. Kila ukivaa kombati za kaki mtaani ulionekana kuwa shujaa tena kamanda kweli kweli.
Kwa wakati huo kua chadema ilikua ni sifa tosha, spirit ya Dr slaa ilienea kwa vijana wengi wadogo nchini. Ilikua ni nadra kumkuta kijana ccm, wazazi wangu wote ni CCM ila walishangaa jinsi mtoto wao nilipokua nawapa shule ya upinzani. Nakumbuka mama alinambia... " mwanangu siasa haitakiwi uwaamini watu kiasi hicho, hyo ni kazi ya kutafuta kula kama kazi nyingine tu". Wala sikua na habari.

2015 mwenyekiti alifanya kosa kubwa sana ambalo litakitafuna chama kwa mda mrefu sana. Ile gia alioibadilisha hewani ilifungua vichwa vya vijana wengi ikiwepo mimi na kuamini kuwa siasa ya upinzani ya Tanzania ilikua ni ya viongozi wenye njaa, wasio na misimamo, na wenye uchu wa madaraka, eti mtu aliye ndani ya chama kwa mda mrefu, mtu aliyeshiriki kueneza Sera, hoja na propaganda ashindwe kuaminiwa na badala yake aje mtu tuliemtusi na kumpa kila aina ya tuhuma!!!. Lahaula ilikua kituko. Hakuna kampeni ziliojaza watu za upinzani, kama kampeni za kukemea ufisadi!! Kumbuka oparesheni sangara, Ile list of shame ya Dr slaa ilifungua milango ya fahamu ya watanzania kuhusu nchi yao. Lakini mambo yote haya yalibadiliswa ndani ya wiki mbili tu baada ya mwenyekiti kubadili gia angani na kumchukua kamanda dhaifu ambaye hakuwahi hata kuvaa kaki, ilionyesha dhahiri alikuja kimwili tu ila kiroho alikua kule aliporudi saizi. makamanda hawakuongelea tena kuhusu ufisadi badala yake tulizungushwa mikono kuimba mabadiliko.. Walio jikoni wana siri nzito juu ya nani alifaidika na uzungushwaji mikono huu.

Leo hii CHADEMA hujui kama wana katibu mkuu, jamaa yupo yupo tu. Vijana wao na wabunge wao wanaendesha siasa kiujanja ujanja tu. Wanadandia kila hoja mitandaoni, hawana zile amsha amsha za Dr wengi wamekaa kipigaji pigaji tu kusubiri kuunga juhudi. Eti wanashabikia kiongozi wa ccm kumchallenge magufuri 2020, inaonekana hata adui yao saizi hawamjui.
Binafsi niliistaafu siasa za Tanzania 2015 nikijikita zaidi na kutafuta namna ya kulea kizazi changu kijacho, sasa nimeamua kuwa mtizamaji tu... Upinzani una safari ndefu kwenda kuishika dola, huu ni ukweli mchungu kuumeza.

The irreplaceable.
 
Ninauhakika kama nawe ulikuwepo ndani ya siasa wakati wa ukatibu wa huyo Dr Slaa, utakua ume mmiss sana.
Alinyimwa kugombea ubunge akiwa CCM akahamia CDM,kanyimwa kugombea uraisi akiwa CDM akahamia CCM. Kwa hiyo yeye haoni wengine kufaa kugombea bali yeye tu!?
Shida yake kubwa hana maamuzi, maamzi hutoka kitchen.
 
"Nitakapo apishwa kuwa rais wa JMT, mwakipesile ukatafute nchi ya kwenda" maneno ya ukali na gadhabu ya Dr wilbrod Slaa wakati wa kufunga kampeni za uchaguzi wa mwaka 2010 pale jijini mbeya. Itakumbukwa kuwa mkuu wa mkoa wa mbeya kwa wakati huo John mwakipesile, alifanya kila aina ya figisu kuhakikisha Dr slaa hafanyi mkutano mbeya, kwanza umeme ulikatika jiji zima na pia polisi walikua wanachelewesha kuanza kwa mkutano ilihali mwisho wa kampeni ulikua saa kumi na mbili jioni. CCM walimuogopa Dr slaa, alikua na ufuasi mkubwa wa vijana waliokua wakitaka new regime

Nakumbuka nilikua kidato cha tano wilayani Rungwe mkoani mbeya, hivyo niliruka ukuta na masela na kusafiri mpaka mbeya mjini kumsikiliza Dr. Slaa was a presidential material, alikua anajua kuhutubia, anajua kujenga hoja, na msimamo mkali kwa vile anavyoamini. "Nikiwa rais elimu Bure toka chekechea mpaka chuo kikuu, nikiwa rais sitaki kumuona mtanzania anaishi nyumba ya tembe..." Rafiki yangu mmoja alikua afande pale mjini alininon'goneza "hakika hili jamaa hata mie natamani lichukue nchi".Hakika Dr slaa aliijua siasa.

Hata baada ya kuukosa uraisi dr slaa alipania kukijenga chama mpaka kwenye ngazi ya shina, CHADEMA ilipata uungwaji mkono mkubwa sana kipindi hiki. Kila ukivaa kombati za kaki mtaani ulionekana kuwa shujaa tena kamanda kweli kweli.
Kwa wakati huo kua chadema ilikua ni sifa tosha, spirit ya Dr slaa ilienea kwa vijana wengi wadogo nchini. Ilikua ni nadra kumkuta kijana ccm, wazazi wangu wote ni CCM ila walishangaa jinsi mtoto wao nilipokua nawapa shule ya upinzani. Nakumbuka mama alinambia... " mwanangu siasa haitakiwi uwaamini watu kiasi hicho, hyo ni kazi ya kutafuta kula kama kazi nyingine tu". Wala sikua na habari.

2015 mwenyekiti alifanya kosa kubwa sana ambalo litakitafuna chama kwa mda mrefu sana. Ile gia alioibadilisha hewani ilifungua vichwa vya vijana wengi ikiwepo mimi na kuamini kuwa siasa ya upinzani ya Tanzania ilikua ni ya viongozi wenye njaa, wasio na misimamo, na wenye uchu wa madaraka, eti mtu aliye ndani ya chama kwa mda mrefu, mtu aliyeshiriki kueneza Sera, hoja na propaganda ashindwe kuaminiwa na badala yake aje mtu tuliemtusi na kumpa kila aina ya tuhuma!!!. Lahaula ilikua kituko. Hakuna kampeni ziliojaza watu za upinzani, kama kampeni za kukemea ufisadi!! Kumbuka oparesheni sangara, Ile list of shame ya Dr slaa ilifungua milango ya fahamu ya watanzania kuhusu nchi yao. Lakini mambo yote haya yalibadiliswa ndani ya wiki mbili tu baada ya mwenyekiti kubadili gia angani na kumchukua kamanda dhaifu ambaye hakuwahi hata kuvaa kaki, ilionyesha dhahiri alikuja kimwili tu ila kiroho alikua kule aliporudi saizi. makamanda hawakuongelea tena kuhusu ufisadi badala yake tulizungushwa mikono kuimba mabadiliko.. Walio jikoni wana siri nzito juu ya nani alifaidika na uzungushwaji mikono huu.

Leo hii CHADEMA hujui kama wana katibu mkuu, jamaa yupo yupo tu. Vijana wao na wabunge wao wanaendesha siasa kiujanja ujanja tu. Wanadandia kila hoja mitandaoni, hawana zile amsha amsha za Dr wengi wamekaa kipigaji pigaji tu kusubiri kuunga juhudi. Eti wanashabikia kiongozi wa ccm kumchallenge magufuri 2020, inaonekana hata adui yao saizi hawamjui.
Binafsi niliistaafu siasa za Tanzania 2015 nikijikita zaidi na kutafuta namna ya kulea kizazi changu kijacho, sasa nimeamua kuwa mtizamaji tu... Upinzani una safari ndefu kwenda kuishika dola, huu ni ukweli mchungu kuumeza.

The irreplaceable.
Ujumbe wako umenitia huzuni Sana. Tuliiamini chadema, wao wakacheza na mioyo yetu, wakatugeuza ma toy kwamba wao ndio wanaamua sisi tufikirie Nini na kwa muda gani.
Mara fisadi, ghafla kamanda wa mabadiliko. Na matusi yasiyo na idadi kwa Dr Slaa.
Ila ndio ivo tena bado Kuna manyumbu wanawaamini wapinzani wa bongo. Nilimpa Magu kwasababu ya kauli mbiu CHAGUA MAGUFULI SIO CCM. Bila gia ya angani CCM walikuwa hawatoki 2015. Penye uzia penyeza rupia.
 
Hungeweza kuona Dr. Slaa akiokoteza maneno ya kihuni ya humu mitandaoni kama vile "jiwe, mshamba, chatle" nk kisha unaenda kuyaandikia hoja kama afanyavyo Lisu na wafuasi wengine wa chadema!

Slaa alikuwa anaibua hoja mpaka system inatetemeka.
Hayo yote ni kwasababu awamu iliyopita iliruhusu kazi za siasa zifanyike,haikuogopa kukosolewa,kusemwa vibaya wala kutukanwa,walikuwa waungwana.sio siasa za sasa ambapo hata mikutano ya ndani ya chama inazuiwa kwa mitutu ya bunduki kinyume cha katiba.hata huyo DR Slaa mwenyewe angekuwepo kipindi hiki asingekuwa na lakufanya.

Awamu hii imeamua CCM pekee ndio ifanye siasa,nafikiri wanavyofanya CHADEMA kukaa kimya kuwaacha CCM wafanye wanavyotaka wakati huo wakijipanga kwenda sawa na siasa za awamu hii ni sawa kabisa namimi nawaunga mkono,hakuna haja ya wanasiasa kujitolea kuumizwa,kuteswa,kuonewa,kwaajili ya watu ambao hawajatambua HAKI zao.
 
Nami toka moyoni nimemkumbuka Dr Slaaa ndani ya upinzani wa sasa. Wakati mwingine hua nafikiri upinzani wa sasa wamerogwa kwani kazi yao kubwa ni kudandia dandia hoja nyepesinyepesi tu. Kila siku wanalalamika bila kuja na suluhu ya matatizo. Wanatafuta huruma ya walio madarakani.
Ni kama wamepoteza Dira sijui kama wanajua wanapotaka kwenda...
 
Hayo yote ni kwasababu awamu iliyopita iliruhusu kazi za siasa zifanyike,haikuogopa kukosolewa,kusemwa vibaya wala kutukanwa,walikuwa waungwana.sio siasa za sasa ambapo hata mikutano ya ndani ya chama inazuiwa kwa mitutu ya bunduki kinyume cha katiba.hata huyo DR Slaa mwenyewe angekuwepo kipindi hiki asingekuwa na lakufanya.

Awamu hii imeamua CCM pekee ndio ifanye siasa,nafikiri wanavyofanya CHADEMA kukaa kimya kuwaacha CCM wafanye wanavyotaka wakati huo wakijipanga kwenda sawa na siasa za awamu hii ni sawa kabisa namimi nawaunga mkono,hakuna haja ya wanasiasa kujitolea kuumizwa,kuteswa,kuonewa,kwaajili ya watu ambao hawajatambua HAKI zao.
Unachekesha, au unataka tukuwekee picha za mke Slaa akivuja damu iliyotokana na kupigwa wakati wakiandamana?

Subiri ccm iwaambie sasa anzeni kufanya siasa
 
Ujumbe wako umenitia huzuni Sana. Tuliiamini chadema, wao wakacheza na mioyo yetu, wakatugeuza ma toy kwamba wao ndio wanaamua sisi tufikirie Nini na kwa muda gani.
Mara fisadi, ghafla kamanda wa mabadiliko. Na matusi yasiyo na idadi kwa Dr Slaa.
Ila ndio ivo tena bado Kuna manyumbu wanawaamini wapinzani wa bongo. Nilimpa Magu kwasababu ya kauli mbiu CHAGUA MAGUFULI SIO CCM. Bila gia ya angani CCM walikuwa hawatoki 2015. Penye uzia penyeza rupia.
Hakika mkuu, sie tuliwaza mabadiliko kumbe wenzetu ilikua fursa
 
Nliacha kushabikia siasa mwaka 2015 sina chama mpaka sasa ila sifurahishwi na haya yanayofanywa na ccm

Nliona wanasiasa ni wale wale hasa baada ya kumpitisha lowasa agombee uraisi

Siwezi elezea ghadhabu nlyopata ya ule unafiki

Ila nkaapa siwezi shabikia ccm maisha

Ila neutral mind
Kuna mwingine wanataka wampitishe tena.
 
Ila pia Dr Slaa ana kipaji cha kujieleza kwa level nyingine. Ule mdahalo ITV ambao CCM walimkimbia alisimamisha nchi kwa hoja zilizopangwa na zinaelezwa kwa utulivu bila matusi wala mihemko.

Hata hotuba ya Serena alipindua upepo wote na hadi kesho itabakia kuwa hotuba bora sana. Acha apumzike zake tu kwa zile sarakasi alizofanyiwa na watu aliowaamini sana unaweza kufa kwa pressure.
 
amini nakuambia,HAZIKUWA siasa za kupigana RISASI mchana kweupe ndani ya eneo la serikali linalolindwa na askari.
Nini risasi usisahau mkutano wa chadema ambao ulipigwa bomu huko Arusha! Basically wengine tulijua nini kingetokea kwa Chadema baada ya kupoteza uchaguzi hasa kupoteza ushawishi.

Hata Mbowe alijua matokeo yake ndio maana alisema atajiuzuru akishindwa!
 
Back
Top Bottom