Hakukuwa na haja ya kuja kuomba ushauri hapa
Yaani alijua kabisa kuwa mazingira ni lazima yawe magumu
Mwanamke na mwanaume ndani ya room moja na kitanda kimoja na then unasema mwanamke ana pepo wa ngono kutoka wapi
Hata kama uzalendo ukikushinda huwezi kumsingizia shetani eti shetani alinipitia
Kuna sehem ambazo mpaka shetani anasingiziwa na mojawapo ni hii
atamsema vibaya sana ofcn kama asipolinda urijali wake
mwambie mkeo na yeye amwambie mumewe mjue kama mfanyacho ni chema mkuu!Hongera kwa kupitisha siku ya kwanza.Nakukumbusha tu kuwa Yesu aliwaambia wanafunzi wake kesheni mkiomba msije mkaingia majaribuni,nawe nakusihi ufanye hivyo.Maana lengo la kushea chumba ni zuri kama ulivyoeleza,ila tu ukiingia majaribuni yawezekana hata kile ulichokuwa unasevu kwa kushea chumba ukamuachia huyo mke wa mtu na kukawa hakuna maana tena ya kushea chumba ili kupunguza gharama.Kama unaona utaingia mtegoni ni bora uhame kabisa na kuchukua chumba chako mwenyewe.
yaan mpaka semina iishe najua na mimba itkuwa imepatikana!
hapo anadai kapitisha usiku mzima wakati tayari yule mwenzake kajiweka huru kubaki utupu mbele yake na yeye akavaa bukta na kulala ... angelala kweye kochi walau angeonyesha kweli hana dhamira isiyosahihi
hao toka mwanzo walishapanga nini kifanyike
Mko nchi gani? usipojali mnatoka wizara gani?
Mkuu wanawake ni viumbe wa ajabu sana. Jamaa anadhani anajizuia kulinda heshima yake na ya huyo mwanamke lakini kumbe anaimaliza heshima yake mwenyewe! . Time will tel.Hii imenichekesha na ina ukweli kiasi f'lani.
Mkuu nakuunga mkono
Au angechukua mito ya makochi au hata kwenye carpet akalala chini na kujifunika na shuka akimwacha mwanamke kulala kitandani
Kitendo cha kujikuta mmekumbatiana na bado mkaendelea kukaa namna hiyo hiyo hadi asubuhi mhhh (hii story haiaminiki maana ile asubuhi mzee mzima anapokuwa up na jamaa kaacha tuu mzee aendelee kuwa up mpaka mwanamke anaamka na kuvaa na kumwacha hivyo hivyo siiamini eti)
huyu anazuga tu.....walshapanga hawa
Nadhani hukumwelewa vizuri huyo mfanyakazi mwenzio. Aliposema msave gharama alimaanisha gharama za wewe kutafuta changudoa na gharama za yeye kutafuta kaboy ka kumsuuza.Ni mfanyakazi mwenzangu tumeenda nchi jirani kwa semina ya siku 5.Tulivyofika tu wakati tunacheki hotel ambayo ni nzuri bei kidogo ipo juu ila kampuni wametupa pesa za kutosha sana,Sasa wakati tunajadiliana jinsi ya kufanya yule sister akasema, Kwa nini tusichukue chumba kimoja tukashare ili tusave hizi pesa? Nilijua ananitania lakini akasisitisha kwamba yupo serious,Tukachukua chumba kimoja chenye kitanda kimoja tukazama ndani.Ile kuingia tu ndani yule sister akasema anataka kuoga sababu ya uchovu wa safari akjifunga taulo kavua nguo kazama bafuni.Picha nyingi sana zikanijia ifikapo usiku itakuwaje? Sababu yeye ni mke wa mtu na mimi nina mke home.
Nikajiapisha sintofanya chochote na huyu sister kwanza tunaeshimiana sana.
Nmimi nikaenda kuoga baada ya yeye kutoka nilivyorudi nikakuta ashavaa nguo.
Story story kidogo tukashuka chini tukaenda pata dinner mpaka kwenye saa 5 usiku tukarudi room.
Kufika tu yule sister kavua nguo zake hii sasa alivua mbele yangu akapiga night dressing kajitupa bed.
Na mimi nikajipa moyo nikavua nikapiga bukta nikazama bed.
Tukapiga story mbili tatu huku tukiwa tumejifunikia shuka moja.
Mara usingizi ukanipitia kushtuka nimemkumbatia ile mbaya nikijua ni wife home kuchek na yeye kanikumbatia na kaweka mguu juu yangu.Ki ukweli hali ilikuwa ngumu sana mpaka mapigo ya moyo yalibadilika.
Ki ukweli usingizi ulikata nikawa nimemkumabatia mpaka asubuh.
Palipokucha yaani yule sister hana time akazama zake bafuni katoka kapiga suti yake na mimi nikazama bafuni kutoka tukaelekea kwenye hotel inapofanylika semina.
Jamani hii ndio siku ya kwanza kweli niatweza maliza siku tano bila kuingiza ndoa yangu matatani kwa style hii kweli.
Ila nimeapa kutofanya chochote na huyu sister.
Ee mungu nipe ujasiri.