Negongo Mtu mzito kila jambo unapotaka kuacha au kuanza ni maamuzi ya ndani yanahusika .Mwili ni kasha tuu ambalo unaamua upeleke wapi na ufanyishe nini mwili wako .Kwakuwa uzinzi ni dhambi iliyo juu ya miili yetu basi ni wakati wa kumkana ibilisi na mambo yake yote pasipo kujali wewe ni mtu wa imani ipi .Kuwa karibu na Mungu wako omba mara kwa mara kwa kumaanisha ikiwezekana funga kabisa mwambie ibilisi amekutumia mara nyingi kama mfuasi wake sasa umechoka unataka kuwa huru na unataka kuacha, kataa kwa kumaanisha hiyo roho na tamaa
Mshirikishe mtu wako wako wa karibu kama wewe
Mtu mzito mkeo anajua tabia yako ni wakati wa kumwambia kwa kinywa chako kiri mwambie unajambo unataka kumshirikisha . mwambie umekuwa unatabia mbaya ya kutamani wanawake wengine umechoka na unataka kuacha unahitaji msaada wa maombi yake na hii itakusaidia wewe kujisikia mkosaji na kujuta kila utakapokuwa unataka kutenda hayo lakini la msingi MAOMBI ,MAOMBI ni muhimu mnoo