Nimekutana na malaika

Nimekutana na malaika

Status
Not open for further replies.
Kwa hiki ulichokiandika kwanza nakupa pole sana, nyie ndo wanaume washabiki wa wanawake kama watu walivyo washabiki wa mpira wakati wao hawachezi. Hivi mwanamke kutokuambia mahitaji yake ndo unaona umepata malaika / jini?

Nakupa ushuhuda wa kweli .. jamaa yangu alipata mke wa hivyo, hata siku moja hakuwahi kuambiwa lolote. Mwanamke alijitahidi hadi akanunua kiwanja na kuandika documents Mr. & Mrs, jamaa akawa amevimba kichwa. Mwanamke akapata hela nyingine akajenga mjengo mwingine sehemu nyingine. Mwanamke akanunua gari akamkabidhi mwanaume - mwanaume akawa sasa anaonekana big boss ila ukweli tukijua kuwa hela sio zake.

Siku ya siku alikuta nyumba iko wazi; mwanamke ameamia nyumba mpya. Mwanaume kuuliza kulikoni - aliambiwa umefika wakati wa kila mtu kujitegemea. Mwanamke aliondoka na watoto wake + gari nyumbani aliacha documents za nyumba na ndoa basi.

Hadi naandika haya; huyo jamaa yuko kama kachanganyikiwa.
Chief bhana asante kwa mfano ...hiyo ni Ajali kazini " magari yanaua kila siku " lakini haimaanishi kwamba tuache kuyanunua " au kuyapanda "

Karibu sana "
 
Usimkatishe tamaa, wanawake wenye tabia nzuri wapo si wote wadangaji yawezekana katika hao wazuri huyo ndiye mmoja wapo
Hahaa You nailed it all " dada mkuu " nakupenda sana master wangu
 
Tatizo mazoea na mazingira anayokulia mtu
Hili. Nalo ni tatizo kubwa Sana " haswaa unapokutana na mwanamke ambaye ameamua kuyaendesha maisha yake kwa kupitia kiungo chake nyeti cha mwili ".... uzi kama huu lazima ataipinga vikali sana
 
Naona positive vibe only. Sema nini endelea kuenjoy na anachokuonyesha kama utagundua mengine ni baadae. Haimaanishi tumekwambia sie basi uanze kuishi kwa wasiwasi. Wewe enjoy mpaka utakapoona sasa hapa nimeridhika kabisa unaweka ndani. Maana mwingine akishaona kila baya analomuwazia halioni anaanza kujishtukia yeye.
Chief bhana asante kwa mfano ...hiyo ni Ajali kazini " magari yanaua kila siku " lakini haimaanishi kwamba tuache kuyanunua " au kuyapanda "

Karibu sana "
 
Umewahi kuvundika tunda?yaani unaangua afu unaliwwka ukisubiri liive?
Basi vuta subra....invoice utakayopigwa itakusababisha uchukie kabisa usipokua makini!JISHIKILIE BRUV.
Hahaa sawa
 
Chief bhana asante kwa mfano ...hiyo ni Ajali kazini " magari yanaua kila siku " lakini haimaanishi kwamba tuache kuyanunua " au kuyapanda "

Karibu sana "
Hujanielewa mkuu;
Nia yangu kubwa ni kumsaidia huyu dume asishabikie kupenda vya bure. Mwanamke ni msaidizi tu; si kila kitu unamwachia yeye. Ipo siku atakuja hapa analia; unapomfanya mwanamke akawa dume jike (kwenye kujitegemea) ujue unalea jibu, siku likitumbuka utalia kama nyau.
Nimeoa nina zaidi ya 25 years kwenye ndoa, nimeona mengi sana! Natoaushauri tu kwa sababu vijana wa siku hizi wanapenda dezo. Hiyo dezo sasa ... nisiandike mengi.
 
Naona positive vibe only. Sema nini endelea kuenjoy na anachokuonyesha kama utagundua mengine ni baadae. Haimaanishi tumekwambia sie basi uanze kuishi kwa wasiwasi. Wewe enjoy mpaka utakapoona sasa hapa nimeridhika kabisa unaweka ndani. Maana mwingine akishaona kila baya analomuwazia halioni anaanza kujishtukia yeye.
Mkuu wala usijali " naijua JF vyema kabisa " inshort "Jf ukileta mawazo yako hapa " unapaswa kujiandaa ki-psychology toka kwa michango ya watu " kuna watakao ku- support na watakao kupinga kwa fact na kuna wengine watakupinga tu ilimradi siku ziende " binafsi hii ndio sababu inayo nifanya niipende Jf " kwa sababu " unapopingwa unapata nafasi ya kujitazama upya " ... Yeah hivyo yaani "..
 
Hujanielewa mkuu;
Nia yangu kubwa ni kumsaidia huyu dume asishabikie kupenda vya bure. Mwanamke ni msaidizi tu; si kila kitu unamwachia yeye. Ipo siku atakuja hapa analia; unapomfanya mwanamke akawa dume jike (kwenye kujitegemea) ujue unalea jibu, siku likitumbuka utalia kama nyau.
Nimeoa nina zaidi ya 25 years kwenye ndoa, nimeona mengi sana! Natoaushauri tu kwa sababu vijana wa siku hizi wanapenda dezo. Hiyo dezo sasa ... nisiandike mengi.
Hahaha kwani kuna sehemu ambayo content inasema kuwa " mwanamke ameachiwa yeye kila kitu " Aisee " humu kuna watu ni wagumu wa kuelewa sijapata kuona
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom