Nimekumbuka mbali sana leo

Nimekumbuka mbali sana leo

Pole sana mkuu; kwa uliyopitia kwanza
Waswahili wanadai yatima hadeki na kweli hadeki. Tuache kuwapa hawa mama mimba na kuwa acha ili kupunguza tatizo hili, natumai hutakuja mkimbia mwanamke utakayempatia mimba maana kama ni shule tiyari umeipitia vizuri

Hatuzungumzii single maza,tunazungumzia mama wa kambo asa kuwapa mimba hao na mada hewani vinahusiana nini

wengi wanalelewa na mama za kambo kwa sababu mama zao ni single mother then mshua kaowa mwanamke mwingine

kwahyo mdau hapo yupo sahihi tu
 
Daaah!! Mungu nijaalie moyo mwema wa kutomnyanyasa mtoto yeyote.
 
Ila wakati mwingine ni mentality tu ya watoto wanaolelewa na watu ambao sio wazazi wao. Kwanza anakuwa kishajiandaa kisaikolojia kuwa huyo sio mzazi wake, hivyo lolote litakalofanywa atachukulia kuwa anafanyiwa kwakuwa yeye ni mtoto wa kambo. Wakati mama yake mzazi angefanya the same angeona anafanyuwa kwakuwa anapendwa.

Kuishi na mtoto asie wako ni kipaji na inahitaji moyo wa ziada.
 
Mungu akusamehee bure, umeandika utumbo Tena ulioozaaaa,
Hivi unasikia Visa vingap watoto kuumizwa na mama zao wakambo? Kuchomwa Moto,kuchomwa bisibisi, kunyimwa kula, kupigwa Hadi kupoteza fahamu...are you a foolish?
Hakuna mama mzuri ka mama wa kambo. Jichunguze utakuta kuwa weye ndo ulikuwa mkorofi. Kulialia hovyo. Kujinyea na kujikojolea hivyo hovyo. Mama wa kambo huku akilea mimba zake weye unataka akupakate ka mamako alivyokufanyia.
Acheni kuwatukana bali muwashukuru. Mama wa kambo angekuwazia mabaya weye ungelifikia ulipo leo?? Shilingi ina pande mbili
 
Nimekumbuka enzi hizo naishi na mama wa kambo nilipitia shida sana kupigwa bila kosa ilikua kawaida sana kupitisha siku nzima dry bila kula ilikua normally sana

Nakumbuka ilikua nikifaulu napigwa naambiwa nimeigilizia na nikifeli naambiwa sina akili napigwa pia yaani nilikua naishi kisungura sungura sana

Manyanyaso gani ushawai kukutana nayo share experience
Huyo mama wa kambo bado yupo hai kama ndio una mawasiliano nae, au unamsaidia lolote?. Umeshawahi kumuuliza kwanini alikuwa akikupa azabu?


Nangatukaa 🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️
 
Zamani hakukua na mitandao ndo maana walikua hawasikiki tena walikua wakatili wa kutisha mnoooo
Nina dada yangu binamu aliwahi kulelewa na mama wa kambo miaka ya 90 mwanzoni, mama yao alifariki, mimi chozi lilinitoka kwa aliyokuwa akinisimulia. Kubwa aliloniambia ni hatowahi kuja kumsamehe kaka yake kwa mama huyo na hilo pengine ndio linaloweza msababisha asiingie Mbinguni.

Worse enough, yule mnyanyasaji sasa hivi ana maisha mabovu ya kusikitikia, hao watoto wake wana msaada mdogo mno kwa wazazi wao. Majirani walipoona hali hiyo ananisimulia ilibidi wajichange wawasafirishe kurudi Mwanza kwa baba yao mdogo.
 
Wale tuliolelewa na mama wa kambo miaka ya 90 hadi 2000 gonga like hapa maana tulilelewa kwa malezi bora
 
Back
Top Bottom