John Gregory
JF-Expert Member
- Jul 14, 2019
- 1,060
- 1,957
Watu tumekojoa sana boarding kuanzia form one,two mpaka three! Uzuri nilikuja kugundua kumbe sipo peke yangu, Kuna jirani yangu naye alitia fora! Tena bora mimi ilikuwa mara moja moja ili huyu jirani ilikuwa karibu kila siku!.Ukikojoa usiku unaamka chap chap unabadilisha nguo unatoa shuka unapanga nguo kavu mbili tatu kwenye eneo la godoro lililoloa kisha unatandika shuka lingine kwa juu ili nalo lisiloe! Chap unatafuta ndoo kisha unaloeka alafu unarudi kulala.Ukijijua una tatizo hilo usije ukalala kitanda cha juu! Utazua balaa!