Kuna siku nilikwenda saloon kuzipunguza urefu kidogo sasa jamaa akazikomba, aliniudhi sana na sikumlipa kabisa......tangu siku hiyo naona bora zibaki hivi hivi

Hahaha,fisi kakosa zoga....!,anaumiiia,bro karibu kwenye team Ndevu ila ziwe zinamuonekano wakigentleman sio zile kama mwarabu wa wapi cjui,na we ni fisi kama fisi wengine sasa usiwaze,wenzio akakikosekana swala mmoja we go to the next one!,so be On to the Next one!,

Pole sana Mkuu, siku nyingine uvae kofia.Hapana mkuu ila si unajua tena ujana wendawazimu, nimeweka madevu na imeshakuwa mazoea kwangu yaani hata nikienda saloon jamaa akizigusa tunagombana.
Basi nenda kawatafute wale wa Masjid wao wameyazoeaSasa kumbe wewe pia hupendi mh! Ila kuondoa hii kitu kwangu ni vigumu rabda nikutwe na tukio zito zaidi
hajakubagua bali amepata hofu kutokana na matukio yaliyotokea.....elewa hali halisi tu pole kwakukosa mtoto mzuri katoka mdomoi mwakoHabari ndugu zangu
Mimi ni mkazi wa Dar ila wiki hii nilipata fursa ya kikazi kwenda Jijini Tanga, hakika nilifurahi haswa nikizingatia kuwa sijakwenda huko tangu enzi ya Kalembo.
Nilifika salama katika jiji hilo tulivu na nikakutana na stori za mwembe 'uliogeuka' Nyerere pamoja na story mbali mbali za matukio mengine, nikafanya kilichonipeleka na nilipomaliza nikaona si vibaya nikatafuta mwenzangu katika mji huu wa stara na mahabati.
Usiku nilipokuwa katika ukumbi mmoja nikipata muziki mororo huku nikiburudika na chaza, pweza nk, mara ghafla macho yangu yakagongana na ya binti mmoja matata sana.
Haikuchukua mda kumfuata na kumueleza matatizo yangu ya moyoni na alionyesha kama kunielewa hivi na kuwa karibu na mimi japo alikuwa akiniangalia usoni sana, tukaafikiana kutoka na kwenda sehemu nyingine na tulipofika nje nikamfungulia mlango wa gari (Vx la ofisi ambalo ni matata sana) ili tuende tulipopanga ila aligoma ghafla.
Akaniambia basi ameghairi na nisimfuate tena na huyo akatokomea!!! Pembeni kuna kijana mmoja ambae alikuwa akiona yote hayo, nikamfuata kama mwanaume mwenzangu tujadili, akaniambia broo umekosea hayo madevu mwanangu, hapa kuna watu walichinjwa sasa wasichana wana hofu sana na watu wa aina yako tena bora mngekwenda na miguu kuliko unaleta mambo ya vioo vyeusi tena.
Nikavuta picha na nikakumbuka ni kweli yule dada alikuwa ananiangalia sana usoni na kweli nina madevu kama urembo toka kubalehe na nimeshazoea hivyo.
Ndugu zangu tumefikia huko kweli? Yaani tubaguane kisa ndevu!!!
Imeniuma sana
haha eti kama bongo flavourTumeshakuwa watu wazima mkuu, promo za nini tena kama bongo flavour
Kwani Mama rai yukwapi? Kakumwaga au..Wanaume tunavutiwa upesi kuliko nyinyi na si ajabu pengine angekuwa mama yenu yule kama sio hiyo dhahma iliyonikumba
Kifo mkuu kinaogopwa sana. Mtu akiona viashiria hata kama siyo vya ukweli lazima hofu imjae.Habari ndugu zangu
Mimi ni mkazi wa Dar ila wiki hii nilipata fursa ya kikazi kwenda Jijini Tanga, hakika nilifurahi haswa nikizingatia kuwa sijakwenda huko tangu enzi ya Kalembo.
Nilifika salama katika jiji hilo tulivu na nikakutana na stori za mwembe 'uliogeuka' Nyerere pamoja na story mbali mbali za matukio mengine, nikafanya kilichonipeleka na nilipomaliza nikaona si vibaya nikatafuta mwenzangu katika mji huu wa stara na mahabati.
Usiku nilipokuwa katika ukumbi mmoja nikipata muziki mororo huku nikiburudika na chaza, pweza nk, mara ghafla macho yangu yakagongana na ya binti mmoja matata sana.
Haikuchukua mda kumfuata na kumueleza matatizo yangu ya moyoni na alionyesha kama kunielewa hivi na kuwa karibu na mimi japo alikuwa akiniangalia usoni sana, tukaafikiana kutoka na kwenda sehemu nyingine na tulipofika nje nikamfungulia mlango wa gari (Vx la ofisi ambalo ni matata sana) ili tuende tulipopanga ila aligoma ghafla.
Akaniambia basi ameghairi na nisimfuate tena na huyo akatokomea!!! Pembeni kuna kijana mmoja ambae alikuwa akiona yote hayo, nikamfuata kama mwanaume mwenzangu tujadili, akaniambia broo umekosea hayo madevu mwanangu, hapa kuna watu walichinjwa sasa wasichana wana hofu sana na watu wa aina yako tena bora mngekwenda na miguu kuliko unaleta mambo ya vioo vyeusi tena.
Nikavuta picha na nikakumbuka ni kweli yule dada alikuwa ananiangalia sana usoni na kweli nina madevu kama urembo toka kubalehe na nimeshazoea hivyo.
Ndugu zangu tumefikia huko kweli? Yaani tubaguane kisa ndevu!!!
Imeniuma sana