Kama bahati ipo ipo tu. niliwahi kutendewa vibaya na masekretari wa UDOM Kwa kushindwa ku submit document yangu ya TRANSCRIPT niliyowakabidhi after interview. Matokeo yake wenzangu wote wakaitwa kazini baada ya wiki mbili na Mimi sikuitwa na nilipoulizia nikaambiwa siku-submit transcript alhali nilii-print ofisini Kwa Mlacha na kumkabidhi sekretari wa paneli ya interview ili akabidhi Kwa mwenyekiti wa paneli. Nilikata tamaa na kushukuru Mungu Kwa walichonifanyia. Baada ya muda nikapigiwa SIMU toka Open University Kwa ajili ya interview wakati huo Nikiwa mkoani na nilikuwa safarini toka Tarime kwenda Musoma (ku-submit application ya UDSM), simu iliita Mara mbili na sikusikia Sababu ya muungurumo wa gari. Nilipotoa simu mfukoni na kukuta missed call ya ofisi 022- nikapiga hiyo namba na aliyepokea akaanza Chenga Chenga Mara ngoja ntakuunganisha na fulani ndo aliyekupigia blaa blaaaaa nyingi. Finally sikupata response yoyote. Mungu si Athumani baada ya miezi kadhaa mmoja wa directors wa centre za OUT akaenda Dar na kufuatilia issue yangu na kuniambia kuna mtu aliingizwa kinyemela kwenye orodha na Mimi jina langu lilikuwepo Nikiwa targeted kupelekwa kituo cha Mwanza.
Ninapokupa experience hii nikujulishe tu kuwa baada ya muda fulani nilipokea miito ya ajira toka UDSM (main campus), DUCE, MUCE, Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto na nikabaki njia panda wapi nichague. Kwa sasa niko Kati ya Taasisi hizo hapo juu na nashukuru Mungu Kwa kudhihirisha kuwa ridhiki ya mtu haifungwi, inacheleweshwa tu.
Sali sana na Mungu atajibu maombi yako.