Nimekata tamaa ya kuolewa

Nimekata tamaa ya kuolewa

hahaaaaa..ni sheeedahh!!bora nicolewe coz nitakua free kuchange ladha
 
Aisee huyu mtu anaitaji ushauri

Nimekata tamaa ya kuolewa kabisa kwani niliedhan kuwa ndo mume wangu kanigeuka vibaya sana
umri wangu miaka 28 nimejitunza siku zote nikiamini na kumuomba mungu anipe mme mwema nimekua katika maadili ya kidini nimepoteza wachumba wengi baada ya kutofautiana yote ni baada ya kukataa kufanya mapenz kabla ya ndoa.
mwaka jana nikapata mchumba tukatambulishana kwa wazazi alinionesha mapenz kiukwel mpaka nikashawishika kufanya mapenz kabla ya ndoa ( najutia sana) ikapelekea kupata ujauzito gafla mwenzangu ananiambia anamchumba doct mwenzie .....
kweli nimekata tamaa ya kuolewa kabisa
1. umri unaenda tayar ninakikwazo mtoto wanaume wengi kuoa mwanamke mwenye mtoto ni kubahitisha. ukizingatia na umri mbaya... cjui inawezekana mungu hakunipangia kuolewa.

( nibaada ya kupotezana kwa mda mrefu na rafik yangu leo tumekutana ndo ananipa story jinsi alivyo katamaa ya kuoelewa)

Usikate tamaa!!!! Maana tupo wengi tunaohitaji mke wa aina yako!

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
Nahitaji kuoa mwanamke kama wewe ila tu ikiwa utaingia mzima mzima kwenye ndoa isiwe unaendelea na mahusiano mengine hasa na aliyekuzalisha maana haya mambo ya kijinga yapo. Mtoto nitamlea na kumsomesha sio shida. Ila tu ikiwa utaingia mzima mzima.

NB: niliwahi kuwa na mke tukate gana na sina mtoto.

Mtoa mada muunganishe rafiki yako na fursa hii hapa
 
Kwani nani anaoa siku hizi. Wenyewe ni kero tupu. Bora hata uambulie mtoto shukuru Mungu. Wanawake wameharibu wanaume wote.
 
Natasha kaolewa na miaka 50+ alikuwa na mtoto na wajukuu 2 asikate tamaa mapema na asione huyo mtoto kama kikwazo as long as alikubali kuibeba mimba yake na kuzaa kwa uchungu hiyo ni baraka

unajitahidi kutia moyo waliokata tamaa....
 
Nahitaji kuoa mwanamke kama wewe ila tu ikiwa utaingia mzima mzima kwenye ndoa isiwe unaendelea na mahusiano mengine hasa na aliyekuzalisha maana haya mambo ya kijinga yapo. Mtoto nitamlea na kumsomesha sio shida. Ila tu ikiwa utaingia mzima mzima.

NB: niliwahi kuwa na mke tukate gana na sina mtoto.


sio mimi ndugu ni story ya rfk yangu ila kama upo serious nimfikishie ujumbe
 
Naitaji kuoa. Lakini nina watoto 8 kila mtoto ana mama yake na nuna umri wa miaka 36 kazi yangu ni Daktari (MD) kama yuko tayari tuwasiliane. Naishi Kibaha.

Huyo Daktari mwenzio ndo kamtenda hivooo...kwani haogopi..?
 
Nilijua wewe yamekukuta kumbe rafikiyo.

Mwambie aondoe mawazo ya wasi wasi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom