Nimeichoka 'Samahani' Yako (sorry is a Sorry Word)

Nimeichoka 'Samahani' Yako (sorry is a Sorry Word)

Pole sana....ila huwa inatokea sana katika mahusiano na haswa pale mmoja kati ya wapenzi anapoona amependwa zaid.
Mfuate umwambie ukwel na kumuomba msamaha ila kibarua unacho hapo maana moyo bhana unakinaigi ukichoka.
 
ndugu yangu mbona unataka kuleta majanga hapa bure sina majonzi yoyote yale basi tu nimeona nijifurahishe kwani mm ni mtu wa furaha siku zote, kwani wewe utakuwepo kwenye shindano la waimbaji wa chitchat tarehe 6 pls naomba uwepo ili uchujwe na anza kuandika songi lako kuleeee
Naona unalazimisha furaha ingawa moyoni una majonzi....
 
kagina, Mnama, Goodluck hammy J naomba mshiriki kwenye kinyang'anyiro cha kumtafuta mwimbaji bora wa chitchat na mtunzi bora wa wimbo wenye hadhi za kichitchat anzeni sasa kuandika mashairi yenu
 
Last edited by a moderator:
Mentor yani mtu anasoma hii stori mpaka anasinzia hapohapo punguza maneno mengi kwenye thread zako unazotuma best
 
Last edited by a moderator:
Sasa kwanini unakuwa sio mwaminifu jamani? Ona umempoteza Anitha, mtafute umuombe msamaha kwa uliyomfanyia

Jambo gani tena

Ya Mary ni ya mwingine..ya Anitha ni yangu!

halafuuu kuna jambo hujanijibu hadi leo...
 
Kwa raha zako Mentor



duh mkuu kama kasema hivyo basi tena..sina mbinu nyingine zaidi!!
vipi nikimjimbu, "I KNOW - ALAINE"

Yes I know, yes I know, I know
That there will never be a love like this again
Like this again

hapa sitamani @Fp, sakapal na Karucee wapaone wanavojua kudadavua nyimbo...
 
Last edited by a moderator:
Sasa kwanini unakuwa sio mwaminifu jamani? Ona umempoteza Anitha, mtafute umuombe msamaha kwa uliyomfanyia

Jambo gani tena

My dear ram, hiyo ni past tense sasa...! nmeacha uhuni...ata njoo unione!!!:roll:

Kwa raha zako Mentor



Shukran kaka..vipi amekuPM nn sasa!?? nmesamehewa?
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: BAK
kagina, Mnama, Goodluck hammy J naomba mshiriki kwenye kinyang'anyiro cha kumtafuta mwimbaji bora wa chitchat na mtunzi bora wa wimbo wenye hadhi za kichitchat anzeni sasa kuandika mashairi yenu

Lol ! sasa ladyfurahia mitihani mingine lazima uanze na tuisheni kwanza, itabidi tukutane unipe tuishen kisha ndio hilo zoezi la kuandika mashairi lianze.😛opcorn:
 
Sorry is a sorry word…(inspired by Tarrus Riley)


11[SUP]th[/SUP] March 2012 Sunday:

Nilirudishiwa funguo…na tag imeandikwa, “Sorry is a sorry word”

Your words have no meaning
Cause you continue to do the same thing
Now sorry is a sorry word
Look at all I’ve done for you.
Am sorry that you’re sorry but sorry is not enough for me baby
Am sorry that you’re sorry but sorry can’t dry my tears Mentor…

2010 Mbagala, Kijichi

Ni katika purukushani za kukimbilia daladala..

Nilimaliza chuo 2008 kule Moshi, MUCCoBS. Baada ya kumaliza tu nilibahatika kupata kazi kwenye tawi moja la kampuni moja ya BIMA kule kule Moshi. Nilifanya kazi kule mpaka mwaka 2009 May nikahamishiwa makao makuu ya kampuni huku Dar es salaam.
Kama kawaida unapoanza kazi na ulitoka familia za kiporo asubuhi na ugali chumvi usiku lazima uanze na kushikishwa chuma kila siku. No..sina maana hiyoooo…namaanisha kusimama kwenye daladala.
Nilipata kachumba kamoja kule Kijichi wanapaita njia panda ya Neluka…nisiseme sana majirani wasijenijua. Life was good kwa kweli kwani kama ni kazi nilikuwa nafanya kazi nzuri na I gave my all kwa kazi. Nilipata vijisafari vya mara kwa mara kwenda kwenye branch offices mikoani kiasi kwamba salary yangu ilikuwa inatumika kiasi sana kwa mwezi.


Anyway…


Siku hii nilitoka zangu kazini maeneo ya posta nikaelekea kituoni kuoneshana ubabe. Zilipitapita daladala kadhaa watu wakagombania sana. Nakumbuka siku ile kulikuwa na kamvua kiasi na ubrazameni wangu sikuwa na mwamvuli. Basi katika kuangaza angaza macho nikamuona mdada mmoja..

...Anitha...

She is a queen..royal. Ana sura ya upole. Well behaved. Unusually well adjusted. Every man’s dream girl.

Nilishtuka kwanza kuona sura ile pale stendi. Nilihisi naota. Nikafunga macho mara kadhaa na kufungua tena nikitegemea kutomuona tena nitapofungua macho. She was still there beautiful as ever… hehehe..na alikuwa na mwamvuli! ;-)

Nikajisogeza kimahesabu mpaka nikawa karibu naye. Nikamwambia, “Mambo…Natumai malaika wanajua kiswahili”

At first hakunielewa..ila aliponielewa akatabasamu..now wait a minute! Sio tabasamu la kipashkuna kama kina dada wengine siwataji hapa. Tabasamu lake kama ulikuwa na malaria inaisha. Melting smile..kama ushawahi kusikia.

Anitha: “Hahaha..najua.”

Mentor: “…mhh…aaa..” (honestly hapa siogopi kusema nilipatwa na kigugumizi…)

Mentor: “Naomba lift”

Anitha alikubali tukashare mwamvuli ule na kuanzia pale stori zikaanza..nikajua anafanya field kwenye law firm moja maeneo ya pale pale posta. Anaishi kijichi na dada yake. Tuliongea sana that day tukasahau hata kugombania daladala kwenda home. Ilifika hadi 06:30pm ndo tukagundua muda umekwenda.

Tukagombania pale tukapata vinafasi vya kushikilia chuma walau (wakazi wa G/mboto na Mbagala au Mwenge/Ubungo watanielewa hapa..ukipata nafasi ya kushika tu chuma unajisikia kama umepata seat yani).

Mimi na Anitha

Mahusiano yetu yalikuwa ki-automatically sana mpaka leo sijawahi kuelewa. We just matched and clicked. Mara nyingi tulikuwa tukikutana weekends na tulienjoy sana kuwa pamoja.
Anitha alinipa condition moja ili kuwa naye, ‘No sex till marriage’. I loved her and ofcourse nilikubali bila kipingamizi.

It was easy kwa siku za mwanzo za penzi letu koz maybe ndo nilikuwa nalibembeleza, au ni kweli nilipokuwa naye niliweza kuona beyond the wedding day, au ..au..ila nilikubali!

I must say…now that I think of it, sex is overrated. Nakumbuka the way we used to enjoy life na Anitha. We used to look forward to Fridays so we could be together. Tulienda movies, swimming, we played cards..tubishane weee ali mradi kila mtu awe mshindi au tutoke draw. Tuanze ushabiki wa mpira..mimi Chelsea, yeye Man useless!!!!

Them gone good old days...

Saloon…24 November 2010


Pepo lilianza kuniingia siku nimeenda kunyoa nywele. Wakati yule mdada wa kuniosha anafanya kazi yake tukaanza chit-chat.

Mary: “Vipi unafanya na scrub”

Mentor: “Aa hapana nawahi kupika”

Mary: “Mh! Huna mke?”

Nikamuonesha kidole changu..hata alama ya pete kwa mbali hakina…

Mary: “Mchumba? Girlfriend?”

Mentor: “hapana mrembo sina...”

Mary: “Du! Sasa uzito unapunguzaje?”

Mentor: “Ahahaha..sio siri, ni Revola!”

Mary akacheka baada ya ku-connect the dots..

Mentor: “Au ulitaka kunitua mzigo?”

Mary: “Usijali…ntakupa namba”

Mary akamaliza kuniosha akanikausha nikampa pesa akawa ametoka nje kuchukua chenchi. Nikamfuata huko nikawa nasoma messages tena nakumbuka moja ilitoka kwa Anitha. Aliponipa chenchi akanipokonya na simu akaandika namba yake akajibip.

From there tukaanza kuflirt na nini. Ikabaki kutafuta siku ya kupunguza uzito..Katika mbinu nilizokuwa nazifahamu ikawa moja ya kudanganya kuumwa ofisini na kudanganya safari kwa Anitha. Tena nilimwambia naenda tu branch ya Kibaha so the following day ningekuwa naye. Ijumaa ikafika sikuenda ofisini haooo …sipataji! Basi nikapunguza uzito na kesho yake tukarudi.

Nikakuta Anitha ashafika home anaangalia movie. She had the keys to my place. Tukasalimiana tukakaa tunaangalia ile movie.


Mistake:

Anitha akachukua simu yangu akawa ananipiga picha kiuchokozi tu. Daaamn! Ikanihit…I have pictures of Mary in my phone.!!!! Kunyang’anya nashindwa.
Alipomaliza kupiga kama kawaida akataka tuziangalie wote…previous..previous..previous..mwanaume raha yote na tabasamu lishanipotea…previous…mara kabaaaang!

Anitha alilia sana ile siku…niliomba msamaha hadi machozi. Hakunielewa akaondoka na hasira nikajua ndo nimemkosa Anitha hivihivi. Ilinichukua wiki mbili kuweza tu kupata nafasi ya kuongea na anitha na kumuomba msamaha. Baada ya ahadi nyingi na machozi ya kiume Anitha alinisamehe.
Little did she know huo ndo ulikuwa mwanzo tu wa kupunguza uzito…

Case 2:

Wiki moja tu baada ya kusamehewa..ama kweli kuna tabia ukizianza ni ngumu kuziacha
Rematch na mdada wa saloon..of course hii haikugundulika ndo nikapata courage kuwa nimeanza kubobea. Akilini mwangu nilijua Anitha ndo wife. Haniachi simuachi…pamoja na uhuni wote ila Anitha ndiye!

Case 3, 4, 5, ??...zote hazikugunduliwa

Case 7: Posta..lunch time. Hii mida mibaya sana…

Naingia kwenye kale kamgahawa pale shelly ya posta kabisa pale. Meza zimejaa. Napepesa macho kwenye kona kulee naona meza ina watu watatu. Nikawahi nikakaa pale nikaagiza chakula. Najifanya bize kweli. Mara watu wawili wakanyanyuka kwenye ile meza nikabaki mimi na dada mmoja, Dorah.

Kama kawaida tukawa tunachat huku tukila. Na mengine unaweza kumalizia…
Dorah alikuwa na tatizo moja! Msumbufu mno kwenye simu kila saa anataka kupiga na kujibiwa message. Ilifika hadi Anitha akagundua kuna jambo. Akasikitika sana na mimi nikamuambia ni Dorah mwenyewe ananitaka babes! Akaniambia kama ungemwonyesha humtaki unadhani angeendelea? Au unataka tena yale ya kwenda Kibaha? Nikaona hapa nimeharibu tena. Nikaomba msamaha pale kishingo upande nikasamehewa.

Case 8, 9…Hizi zilikuwa zinasamehewa tu koz hakukuwa na ushahidi wa kutosha. But Anitha never stopped loving me..Hakubadilika wala kupunguza mapenzi. Nikajua nimemweza…hapa hatoki! A few tear drops and I am forgiven.

Ila honestly, everytime nilikuwa najiambia, ‘this is the last time!’ Nafanya hii tu then I go back to loving my Anitha.

Infact, ukishamwaga tu yale maprotein basi raha yote na ile excitement inapotea. Unaona what a waste of time and energy! Sijui kama hii regret ni mimi tu nilikuwa nayo? Yani ukishapiga bao moja tu unaanza kujiuliza, ‘was she really worth all this struggle kweli?’

Kama ambavyo wahenga husema, Mchovya asali hachovyi mara moja na za mwizi arobaini au kamba hukatikia pabaya…au <insert yours here>


Case n[SUP]th[/SUP]…9[SUP]th[/SUP] March 2012, Friday:

Anitha aliniambia kuwa atachelewa kumaliza kazi na angepitiliza home kwani alijisikia kuchoka hivyo angekuja kwangu asubuhi.

Now, kulikuwa na binti mmoja wa kiarabu, Punim, na yeye alikuwa akiishi maeneo ya Mbagala Zakheim. Huyu dada bana nilikuwa nimefukuzia muda mrefu sana. Kabla hata ya kumjua Anitha. Akawa amentolea nje kabisa. Nikawa nimempotezea mazima.

Sasa Hii wiki yote kuanzia 5[SUP]th[/SUP] alianza tu from nowhere kunitafuta. Nikaona isiwe shida let me play along. Si akaniomba series ya Nikita kama ninazo episodes mpya. Nikamwambia ninazo ila zipo home kwenye external hard disk. Akaniambia nikitoka nimpitie twende wote akakopi kwa laptop yake then akaangalizie kwake. Nikakubali.

So mchana nikawa namtania kwangu pako rough akifika asishangae. Akasema anataka aone mpaka chumbani. Mh!

Fast forward to uhondo time..na hii siku hata hatukupata shida ya daladala…very straight..na tukakaa…shetani bana!

Nikafika home kweli nikamkaribisha na a cane of cold redds huku akiendelea kukopi series zake. Mimi wala wasiwasi sina ndo kwanza bebii Anitha ananambia wanafinalize draft sijui ya kesi gani kachoka balaa. And she was anticipating heavy jam barabarani.

Baada ya muda akahitaji kwenda washroom/chooni/maliwatoni..iko ndani ya chumba cha kulala. Akasema ehee tena ndo nikaone na kitanda chako kisichotandikwa. Tukaelekea chumbani. Akachojoa ki-light sweater alichokuwa amevaa na top…mh! Nikajiuliza mkojo gani huu. Akaingia, kutoka akagoma kuvaa kisa joto..akajilaza kitandani huku akiniambia mbona kitanda kimetandikwa vizuri hivyo and its calling. Nikamwambia kiitikie karibu kama unaona kinakuita. Kama mzaha akajinyosha vizuri na visketi mnavyovaaga kwenda kazini mwavijua wenyewe…nikasema potelea mbali kama hakumaanisha hivyo asingentega kiivi.

Now now now..najua humu hakuna under 18..kwani yaliyoendelea sintoyaandika…

Kilichonishtua ni sauti ya mlango ukifungwa kwa nguvu, kubamizwa! Tukashtuka..nikakimbilia mlangoni nikihisi labda mwizi ashaiba anakimbia hivyo. I was shocked kuona mgongo wa Anitha huyo akiondoka kwa haraka mwendo wa nusu kukimbia nusu kutembea..

Kumbe Anitha alirudi na kwa mapenzi tele aliyonayo kwangu alinitumia message kuwa, “baby dada kaniambia hayupo home so nitakuja kwako nikitoka kazini.” Nilikuwa bize nikipunguza uzito..sikuisikia ikiingia labda ningeweza kuokoa penzi langu kwa Anitha. Nikamuacha mpaka akanikuta, akaniona…akashuhudia…live bila chenga.

Nilimkimbilia kumuomba msamaha kwa hasira akaanza kuongea kwa nguvu jinsi gani alivyonipenda na kunithamini lakini nikamtenda kiasi kile. Kwa jinsi gani amenisamehe mara nyingi ila bado sikujifunza..in short she created a scene pale. Akaondoka akilia. Huku nyuma kumbe naye Punim alitoka nje. Ukimuangalia wala hafiki hata robo ya Anitha basi tu ni ile “I want this taste syndrome” ilinisumbua. Ya muarabu ikoje??

From that day majirani wakawa wananicheka wengine wananidhihaki live live yani nikakosa amani…ilipofika mwisho wa mwezi tu nikahama Kijichi nikahamia zangu Kigamboni.

From that day kila nikimkumbuka Anitha najiuliza kama nitaweza kumpata tena binti mzuri aliyeniheshimu na aliyejiheshimu na kunipenda kama yeye.

Msinione bado nipo nipo sana…uhuni wangu uliniponza.

Wasalaam Wapendwa,
Mentor.
Next time jaribu ku-summarize mkuu!!!
 
andika hapahapa kwanza majaji waone kisha ndo tuonane kwani inakuwa vigumu kuona na na mm ni teacher wa wengi ila ngoja nikutumie wimbo wa chitchat 2013 uukariri ngoja nikauchukue kule nikuletee ili uanze kusoma na kukariri
Lol ! sasa ladyfurahia mitihani mingine lazima uanze na tuisheni kwanza, itabidi tukutane unipe tuishen kisha ndio hilo zoezi la kuandika mashairi lianze.😛opcorn:
 
pole sana Mentor Anitha wako ,moyo wake unaweza ukawa na kanafasi kadogo cha kukusamehe.

ila mkuu a real player hafumaniwi , enzi zangu................... bila fumanizi hata siku moja
 
Last edited by a moderator:
nimeshakuletea hili hapa likariri na uanze kulizoea kisha nawe ufuatishe namna ya kuandika mashairi ila usisahau kuweka vina kila mwisho wa ubeti halafu jaji atakuja kufanya vitu hapa hapa unalingine la kunieleza?

soma hili hapa songi la chitchat 2013 ambalo mshindi apatikana kama yuko serious soma:

1. Ni wakati wa furaha, nderemo na vifijofijo,
wakati wa kujiachia kwa raha zetu,
tukumbukapo huko nyuma tulikotoka na cc jf
viongozi imara walishika hima, kuongoza cc yetu daima
na leo tuko pamoja tukifurahia, uwepo wako na jirani yako
wauonaje best, isingekuwepo chitchat ungemjuaje,
Invisible robot kaza buti mwana, kuimarisha na kuwapa ban
kwa wale wasio na walio wagomvi, wenye kuleta mafarakano
na malumbano yasiyo na msingi wowote, kazi kwako twakupa,

chorus: Tumekuweka mbele yetu, wewe shujaa kiongozi wetu,
endeleza mapambano dhidi ya wale wasumbuao wenzao
huimarishe cc yetu kwa upendo na furaha tele
nasi tufurahi na kuwa pamoja daima x2

2. Rafiki mpendwa wangu wa moyo, niliyekuchagua wewe pekee,
ona jinsi ninavyojitolea kukutumia pm nyingi kwa ajili yako,
Ninaacha kazi na shughuli zangu, nakaa na ipad, laptop yangu,
kukukumbuka na kuchat nawe, kila saa na kila wakati,
nionapo jinalako na avatar yako, macho hujawa na upendo mwingi,
na pale nikuonapo ukinicomment kwenye yangu post,
nabaki kujawa na furaha isiyopimika wala kuwa na mfano.
Napend unapoitikia wito wa kuwa karibu yangu, na kuniona wapekee,
Sina la cha kukulipa basi pokea upendo wangu kwako
Lol ! sasa ladyfurahia mitihani mingine lazima uanze na tuisheni kwanza, itabidi tukutane unipe tuishen kisha ndio hilo zoezi la kuandika mashairi lianze.😛opcorn:
 
mentor, sasa hivi Anitha yuko wapi??
Aisee nenda tena kaombe msamaha..........anaweza kukusamehe...yaani kaa nimeona kabisa...
this was ment to be your wife...na akikubali saa hii usizingue tena...!
watu kma hawa ni adim kinumar.
 
Haya niPM unikumbushe hilo jambo

Done n done...!


Duh Mnama na BAK mmeamua leo kuniumiza moyo sio...


LoL!! Mentor....still waiting 🙂 🙂

Waiting too...on you!


Salute bro Mentor. I appreciate the work

Thanks Mokoyo, msaada wako kwenye kuomba msamaha unahitajika!

Next time jaribu ku-summarize mkuu!!!

Next time jaribu kuto-quote the whole thread mangi!

Kumbe ana kibamia... ndiyo maana ni rahisi kukitembeza

Ahahaha Ngalikihinja, never trust a woman... Cc: awp
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom